|
|
| Chakula na lishe
Haja ya maji ya kunywa Na Mujahiid Mwinyimvua MAJI ni moja ya virutubisho muhimu sana kwa ukuaji na maendeleo ya mwili wa mwanadamu. Katika mwili wa mwanadamu maji yana kazi nyingi, baadhi yake ni: Maji ni sehemu ya mwili wa mwanadamu na pia kazi nyingi mwilini zinafanyika katika mazingira ya umajimaji. Mwili wa mwanadamu hupoteza maji kila siku kwa njia mbalimbali. Miongoni mwa njia hizo ni kutokwa na jasho, kupumua, kutokwa na damu, na kwenda haja ndogo na haja kubwa. Ukizingatia umuhimu wa maji mwilini na kiasi cha maji kinachopotea kila siku katika mwili, itakubainikia wazi haja ya kunywa maji mara kwa mara. Wataalamu wa tiba na wale wa lishe wanatuambia kuwa wasichana, wavulana na watu wazima wanywe angalau glasi nne za maji kila siku. Kiasi hicho cha maji kisipungue, lakini kinaweza kuongezeka kwa kutegemea hali ya hewa (mfano wakati wa majira ya joto) au aina ya kazi anayofanya mtu. Mtu mwenye kufanya kazi ngumu hupoteza maji mengi, hivyo lazima anywe maji mengi ili kuziba pengo. Baadhi ya watu hunywa maji pale tu wanapojihisi kuwa wana kiu. Kiu ni njia ya asili inayomwezesha binadamu kunywa maji. Hata hivyo, njia hiyo haifanyi kazi vizuri katika mazingira ya baridi. Kwa hiyo, jambo la kuzingatia ni kiwango kinachotakiwa mtu kunywa maji kila siku. Hasa katika kila mlo, mtu lazima anywe maji. Hii ni kwa sababu kazi ya usagaji wa chakula inahitaji mazingira ya umaji maji. Mwili wa binadamu pia hupata maji kwa njia ya chakula au vinywaji vingine zaidi ya maji. Kwa mfano matunda kama vile matikiti (Watermelon), mananasi na machungwa ni viongezo vizuri vya maji mwilini. Vile vile maziwa, chai, uji, togwa, soda, n.k. vinaupa mwili kiasi kikubwa cha maji. Zaidi ya vyanzo hivyo, baadhi ya kazi mwilini pia huupa mwili maji. Haja ya kunywa maji au vinywaji vingine lazima iambatane na kanuni za afya. Yaani lazima watu wanywe maji (au kinywaji kingine) yaliyo safi na salama. Katika baadhi ya miji ya Tanzania (likiwemo Jiji la Dar es Salaam) kuna vijana wanaouza maji ya kunywa barabarani ambayo usafi na usalama una mashaka. Kwa hiyo, mwananchi ajihadhari na maji hayo. Na kwa upande wa serikali na vyombo vyake, viheshimu Katiba ambayo inasisitiza utunzaji wa uhai wa raia |
YALIYOMO
TAHARIRI Hakuna Muislamu aliyekufa kutokana na vurugu Mgogoro wa kiwanja Duma: Wakatoliki wasema kuna njama za Waarabu Same Na Mwandishi Wetu Wanawake wakutana Mwanza na kusema: Kunyanyaswa sasa basi Na Mwandishi Wetu, Mwanza Sheikh Omar Bashir ataka Waislamu waimarishe mshikamano Na Said Sharif Ustaadhi Abdallah Mfoyi afariki Na Muhibu Saidi Baraza Kuu halina Katibu Nguruka - Sheikh Kilima Na Abu Adli Viongozi Msikiti wa Ubungo Darajani waitwa polisi Na Kassim Juma Marekani `ilivyosaidia' Mujahidiin Barua ya mtoto wa miaka minne toka Lebanon kwa Bibi Hillary Clinton Ujumbe wa waandishi kwa Bw. Batendi, Wakristo Na Muhibu Saidi Waislamu wanadhalilishwa au wanajidhalilisha Tusiwe Jogoo wa Esopo na Almasi Na MAALIM ALI BASSALEH Sherehe za wiki ya usalama barabarani: Kauli nzito za waheshimiwa zimekalia kuti kavu Na Said Omar Mwanasayansi Avicenna: Tabibu bingwa. Na Dk. A. A. Amur Ujenzi wa Msikiti wa Ijumaa Mriti waanza Na Nasib A. Mziray Kutoweka kwa hazina adimu za kimazingira Na Yassir Salim Mfalme Najashi ni mfano bora wa kuigwa kwa watawala Na Idi Kikong'ona Waislamu Moro wasaidia wagonjwa Na Mwandishi Wetu, Morogoro KUFUATIA KUTISHIA MAGAZETI: Sheikh Ayoub amjibu Askofu Rajab Rajab Na Mussa Ally TAMSA Tanga waahidi kuendeleza mema Na Ibn Mohammed, Tanga Ufugaji, uuzaji nguruwe wakera wananchi Dar Na Mwandishi Wetu Mafundisho ya Quran Kuwepo kwa ufufuo Barua za wasomaji
|
Kutoa maoni yako kuhusu ukarasa huu:
Bonyeza hapa
Au
Andika barua kwa: webmaster@islamtanzania.org