|
|
| Sheikh Omar
Bashir ataka Waislamu waimarishe mshikamano
Na Said Sharif SHEIKH maarufu Jijini, Sheikh Omar Bashir amewataka Waislamu wote nchini kuimarisha mshikamano kwa ajili ya Mwenyezi Mungu (sw) na matukio ya kuuawa Waislamu na kuteswa ndani ya magereza yasiwe chanzo cha kurudi nyuma na kupoteza msimamo katika dini, kwa sababu hayo si mambo mageni katika historia ya Uislamu. Amesema matukio hayo yanapotokea huwa ni uthibitisho wa kuuelekea Uislamu. Sheikh Omar Bashir ameyasema hayo alipokuwa akizungumza na Waislamu Septemba 11, mwaka huu baada ya swala ya Ijumaa katika Masjid Mujahiduun. Amesisitiza kwamba Waislamu wana wajibu wa kuutangaza Uislamu na kumtakasa Mwenyezi Mungu (sw) na kazi hiyo itakuwa ni yenye mafanikio mshikamano utakapo kuwa imara. Katika hotuba hiyo fupi, Sheikh Omar Bashir amesema kwa kufahamu hatari ya migongano katika jamii, Uislamu umeweka adhabu kali kwa yule anayebainika kuleta migongano na kufarakanisha jamii ya Kiislamu. |
YALIYOMO
TAHARIRI Hakuna Muislamu aliyekufa kutokana na vurugu Mgogoro wa kiwanja Duma: Wakatoliki wasema kuna njama za Waarabu Same Na Mwandishi Wetu Wanawake wakutana Mwanza na kusema: Kunyanyaswa sasa basi Na Mwandishi Wetu, Mwanza Sheikh Omar Bashir ataka Waislamu waimarishe mshikamano Na Said Sharif Ustaadhi Abdallah Mfoyi afariki Na Muhibu Saidi Baraza Kuu halina Katibu Nguruka - Sheikh Kilima Na Abu Adli Viongozi Msikiti wa Ubungo Darajani waitwa polisi Na Kassim Juma Marekani `ilivyosaidia' Mujahidiin Barua ya mtoto wa miaka minne toka Lebanon kwa Bibi Hillary Clinton Ujumbe wa waandishi kwa Bw. Batendi, Wakristo Na Muhibu Saidi Waislamu wanadhalilishwa au wanajidhalilisha Tusiwe Jogoo wa Esopo na Almasi Na MAALIM ALI BASSALEH Sherehe za wiki ya usalama barabarani: Kauli nzito za waheshimiwa zimekalia kuti kavu Na Said Omar Mwanasayansi Avicenna: Tabibu bingwa. Na Dk. A. A. Amur Ujenzi wa Msikiti wa Ijumaa Mriti waanza Na Nasib A. Mziray Kutoweka kwa hazina adimu za kimazingira Na Yassir Salim Mfalme Najashi ni mfano bora wa kuigwa kwa watawala Na Idi Kikong'ona Waislamu Moro wasaidia wagonjwa Na Mwandishi Wetu, Morogoro KUFUATIA KUTISHIA MAGAZETI: Sheikh Ayoub amjibu Askofu Rajab Rajab Na Mussa Ally TAMSA Tanga waahidi kuendeleza mema Na Ibn Mohammed, Tanga Ufugaji, uuzaji nguruwe wakera wananchi Dar Na Mwandishi Wetu Mafundisho ya Quran Kuwepo kwa ufufuo Barua za wasomaji
|
Kutoa maoni yako kuhusu ukarasa huu:
Bonyeza hapa
Au
Andika barua kwa: webmaster@islamtanzania.org