AN-NUUR
Na.167 Jamadul Awal 1419, Septembe 17 - 24, 1998

Home Links Islam Tanzania Matoleo yaliyopita

 

Sherehe za wiki ya usalama barabarani:

Kauli nzito za waheshimiwa zimekalia kuti kavu

Na Said Omar

MATAMSHI mbalimbali yaliyotolewa na waheshimiwa wenye nyadhifa mbalimbali katika kuadhimisha "wiki ya usalama barabarani" wiki hii yafaa Watanzania wote tuyaenzi. Lakini

Wengine wameasa kuwa sheria za matumizi ya barabara ni lazima na muhimu kuzingatiwa na watembeao kwa miguu hadi waendeshao vipando vikubwa vikubwa. Hili ni muhimu kwani ni mara nyingi sana waendao kwa miguu wamekuwa ni vyanzo vya ajali mbaya sana barabarani.

Nasaha zingine zimegusa suala zima la umakini katika utoaji wa leseni, maadili ya udereva, maadili ya uaskari katika kusimamia sheria za barabarani n.k. Yote haya ni mazito kulingana na ufafanuzi uliotolewa na wasemaji wetu wakuu.

Katika mazungumzo baada ya habari asubuhi ya Septemba 9, 1998, RTD wanasema kuwa ajali nyingi na mabaya zinazotokea barabarani zinaua au kumaliza watu kama magonjwa ya Ukimwi, malaria n.k. yanavyomaliza watu. Yote haya mimi nasema ni muafaka kabisa.

Kama wasemaji walivyoainisha sababu kubwa zinazosababisha ajali ni kule kutozingatia sheria za barabarani kwa watumiaji wote wa barabara, mwendo kasi wa madereva na kubwa zaidi ulevi wa madereva.

RTD wanaendelea kusema kuwa "Pamoja na sheria ya kuwa dereva asiendeshe gari hali ya kuwa amelewa, ndio kwanza kabla dereva hajaanza safari, atapata "Safari" zake tisa, zikishakaa kichwani anakali usukani".

Pia wanaendelea kusema kuwa amepatikana Musa akaja na fikra ya magari yafungwe gavana. Mimi ninasisitiza kuwa Musa aliyepatikana akataka magari yafungwe vidhibiti mwendo(Gavana) anafaa kupongezwa. Ajabu ni kuwa badala ya kupungua kwa ajali ndio kwanza zimeshamiri. Lakini ni kwa nini? Ni bayana kuwa vishawishi vya kwenda kasi havijadhibitiwa miongoni mwao ikiwa ni ule unaolazimishwa kuwa urithi wa watanzania, "Safari".

Tusidhani kuwa tunaweza kuondoa tatizo hili kwa kutamani tu, lazima tuwe tayari kuvitoa muhanga tuvipendavyo ili zoezi la Musa lifanikiwe Tusisahau kuwa wana wa Israil baada ya kuishi jangwani wakifafadhiliwa na Mwenyezi Mungu kwa Manna na Sal'wa , tamaa mbaya iliyosukumwa na matashi ya nafsi zao na kibri walimtaka Musa amuombe Mola wake awatolee vile vinavyooteshwa katika ardhi kama mboga zake, matango, thaumu na adesi zake na vutunguu vyake. Ndipo Allah akawauliza " Mnabadilisha vitu duni kwa vile vilvyobora? Na ikapigwa juu yao chapa ya dhila na umaskini na wakastahiki ghadhabu za (2:6).

Hivi leo tunamtamani Musa atakayetanczua tatizo hili wakati huo huo hatuko tayari kuyafuata maelekezo yake kwani yatuondoa katika yale yanayotamaniwa sana na nafsi zetu. Tuna haja gani ya kujisumbua? Suala la kujiuliza ni kuwa; je, maneno yatangazwayo na RTD kila moja linajitegemea au yanategemeana?

Ni siku chache zilizopita tulikuwa tukishawishiwa na Radio hii hii kuwa tununue hisa katika kampuni ya kutengeneza Safari . Si hivyo tu bali mara kwa mara tunaambiwa huu ndio urithi wetu. Vile vile tunaambiwa ni namna pekee ya kujipatia nguvu na kuondoa machovu tukitumia Safari au Kilimanjaro bia ya Mtanzania.

Tunamlaumu nini anayeipata Safari kabla ya safari? Anatumia urithi, anatumia alichokizalisha, maana na yeye anahisa, anahitaji nguvu na kujiondoshea machovu kabla ya safari, kwanini asipate Safari.

Askari wa usalama barabarani anahitaji Safari ili afanye kazi yake. Akizingatia maadili ya kazi yake hatapata Safari . Mtoaji wa leseni za udereva halikadhalika.

Aliyepata Safari na akatembea kwa mguu hujiona mfalme na kuyumba barabara nzima. Aliyepata Safari akikaa kwenye usukani mwendokasi KM 120 kwa saa huona kama anacheza. Niambie watakapokutaka wenye Safari za vichwani mmoja juu ya kipando na mwingine akitembea kwa mguu safari zao vipi.

Kwa msingi huu, mimi naona kuwa nasaha za waheshimiwa wote zemeketishwa kwenye kuti kavu kwani mzizi wa tatizo hauguswi ila lawama zinatolewa kuwa kwanini majani hayakauki. 

Juu 
 

YALIYOMO  
 
TAHARIRI 
Hakuna Muislamu aliyekufa kutokana na vurugu

Mgogoro wa kiwanja Duma: Wakatoliki wasema kuna njama za Waarabu Same Na Mwandishi Wetu

Wanawake wakutana Mwanza na kusema: Kunyanyaswa sasa basi
Na Mwandishi Wetu, Mwanza

Sheikh Omar Bashir ataka Waislamu waimarishe mshikamano
Na Said Sharif

Ustaadhi Abdallah Mfoyi afariki
Na Muhibu Saidi

Baraza Kuu halina Katibu Nguruka - Sheikh Kilima
Na Abu Adli

Viongozi Msikiti wa Ubungo Darajani waitwa polisi
Na Kassim Juma

Marekani `ilivyosaidia' Mujahidiin

Barua ya mtoto wa miaka minne toka Lebanon kwa Bibi Hillary Clinton

Ujumbe wa waandishi kwa Bw. Batendi, Wakristo
Na Muhibu Saidi

Waislamu wanadhalilishwa au wanajidhalilisha

Tusiwe Jogoo wa Esopo na Almasi
Na MAALIM ALI BASSALEH

Sherehe za wiki ya usalama barabarani: Kauli nzito za waheshimiwa zimekalia kuti kavu
Na Said Omar

Mwanasayansi Avicenna: Tabibu bingwa.
Na Dk. A. A. Amur

Ujenzi wa Msikiti wa Ijumaa Mriti waanza
Na Nasib A. Mziray

Kutoweka kwa hazina adimu za kimazingira
Na Yassir Salim

Mfalme Najashi ni mfano bora wa kuigwa kwa watawala
Na Idi Kikong'ona

Waislamu Moro wasaidia wagonjwa
Na Mwandishi Wetu, Morogoro

KUFUATIA KUTISHIA MAGAZETI: Sheikh Ayoub amjibu Askofu Rajab Rajab
Na Mussa Ally

TAMSA Tanga waahidi kuendeleza mema
Na Ibn Mohammed, Tanga

Ufugaji, uuzaji nguruwe wakera wananchi Dar
Na Mwandishi Wetu

Mafundisho ya Quran 
Kuwepo kwa ufufuo

Barua za wasomaji 

Masomo ya dini ya Kiislam 

Chakula na Lishe 
Haja ya maji ya kunywa

 

 

   Kutoa maoni yako kuhusu ukarasa huu: Bonyeza hapa
Au
Andika barua  kwa: webmaster@islamtanzania.org  

Home Links Islam Tanzania Matoleo yaliyopita