|
|
|
Kwa wale waliokuwa wakifuatilia makala hizi, nadhani wameelewa kiasi kikubwa maana ya mtu kuwa na maradhi ya kisaikolojia, hususan yale yanayoambatana na kukithiri kwa zinaa katika jamii. Napenda kusisitizia kuwa kuenea kwa maradhi haya kunatokana na kukithiri kwa gonjwa kubwa la zinaa. Gonjwa hili baya linapoachiwa, na kupewa uhuru, kama ilivyo katika jamii zetu za "kisasa", basi haya maradhi mengine yote huja kama ziada. Qur’an inawataja watu wenye maradhi haya: "Ndani ya nyoyo zao mna maradhi, na Mwenyezi Mungu akawazidishia maradhi". (Qur’an 2:10) Kwa hiyo kwa vile gonjwa kuu limeingia ndani ya mioyo ya watu, basi ziada ya gonjwa hilo ni haya maradhi tuliyokuwa tukiyachambua ya Paraphilia za aina mbalimbali. Leo napenda kuongelea uwezekano wa mtu mmoja kuwa na mchanganyiko wa maradhi ya kisaikolojia zaidi ya moja. Mtu anapokuwa na Paraphilia nyingi, basi tunasema mtu huyu anaugua gonjwa kubwa la kisaikolojia linaloitwa Multiparaphiliasis. Huyu kichwa chake kinakuwa na vurugu zote za kimawazo tulizozidhambua huko nyuma. Kwa mfano, Mwendawazi (mtu anayependa kwenda wazi kwa viguo vifupi) mara nyingi huwa na Voyeur (kozimeni), anayependa kukodolea macho watu walio wazi. Mtu huyu pia kwa asilimia kubwa anaweza kuwa mminyaji (Fratter), anayependa miminyano na watu wa jinsia tofauti na yeye. Vilevile, mwanaume yeyote aliyekubuhu katika uchafu wa zinaa ana hatari ya kuwa na maradhi haya ya Multiparaphiliasis. Utamkuta kote. Voyeur yeye, kwenye Sexual sadism yumo, Fratteurism yumo, kwenye Fetishism utakumta na wengi wao wanaweza wasiwe na maradhi ya Transexualism ( kutamani kuwa wanawake), lakini wengi wao utawakuta kwenye Transvestims (kupenda kujipamba kike) hasa kuvaa mikufu ya dhahabu na kubadili nywele ziwe laini na kujipulizia mafuta uzuri yenye harufu kali ili wanukie. Pia utawakuta wanafuga kucha ndefu mithili ya wale wanawake wanaopenda kujipaka marangi kama nyumba, au gari ya mashindoni. Sasa jamii ikishafikia kuwa na watu wenye msetu wa maradhi ya kisaikolojia, basi huwa inasubiri gharika. Na gharika sio lazima iwe kama ya wakati wa Nabii Nuhu, bali hata gonjwa linaloua kama ukimwi pia ni gharika. Labda tu leo nisiseme mengi. Maradhi haya huwapata watu wenye UKIMO (ukosefu wa Kinga Moyoni). Hii ina maana kwamba moyoni mwao hamna chembe ya hofu ya Mwenyezi Mungu. Kwa hiyo, mtu akiwa hana chembe ya ucha Mungu, amri za Mungu zinazoweza kumsaidia, haziingii katika moyo wake, kwa mfano ile amri ya: "Wala msikaribie zinaa, Hakika hiyo ni uchafu (mkubwa) na ni njia mbaya (kabisa)". (Qur’an 17:32) Hakuna daktari wa kutibu maradhi haya, bali tiba inapatikana kwa mtu kuwa Muislamu mtimilifu, ambaye hana UKIMO. |
YALIYOMO
Tahari
Mwaka mmoja wa mauaji ya Mwembechai:
Waliouawa ni wanne
Waasisi wa TAA waibuka kupigania haki zilizoporwa Kuhujumiwa Waislamu kielimu: Mzazi adai mwanafunzi Adam Rashid kafelishwa Maoni yetu: Tuondoleeni wenye mikono ya damu MARADHI YA KISAIKOLOJIA: MULTIPARAPHILIASIS Askari wa Tume ya Jiji wapora mkaa Kuchangia Radio Kheri Broadcasting Station Yesu Kristo na Yohana Mbatizaji
Wakereketwa CCM wawakosha
wauaji wa Mwembechai
Ufugaji holela wa nguruwe
waikumba Dodoma
Watembelea na kusaidia wagonjwa Arusha Mkuu wa wilaya awatimua Masheikh
ofisini kwake
Sayansi na Teknolojia
Chakula na Lishe
Kumbukumbu ya mauaji Mwembechai
|