|
|
|
Na Mujahid Mwinyimvua Ili mwili wa mwanadamu uweze kukaa na kunawili vizuri lazima upate virutubisho vinavyoitwa madini. Katika makala iliyopita tulianza kuzungumzia dhana hii ya madini kwa kutazama madini ya chuma. Makala yetu ya wiki hii inatazama madini ijulikanayo kwa kimombo kama madini ya zinc (Zinki). Madini ya zinc ni moja ya madini inayohitajika mwilini kwa kiasi kidogo lakini ina umuhimu mkubwa, kwa wastani mtu mzima ana madini ya zinc kiasi cha gramu 2.5 (mbili na nusu) sawa na nusu ya kijiko cha chai. Utafiti wa miaka ya hivi karibuni umedhihirisha umuhimu wa madini hii kwa afya ya binadamu. Hivyo basi, watu wasiidharau kwa hoja tu kuwa inahitajika kwa kiasi kidogo mwilini. Madini ya zinc ina kazi nyingi mwilini, baadhi yake ni kuuwezesha mwili kukua na kunawili vizuri, kulinda mwili usipate magonjwa, kufanya vidonda kupona haraka, kusaidia macho kuweza kuona vizuri, inapunguza harufu mbaya kutoka mwilini, inasaidia milango ya fahamu ya kunusa na kuonja kufanya kazi vizuri, n.k. Ukosefu au upungufu wa madini ya zinc nao unasababisha madhara kadhaa kwa mfano, ukuaji kwa watoto unakwenda kwa kasi ndogo, mtu anakosa hamu ya kula chakula, ubongo (akili) unaweza kuathirika, vidonda haviponi kwa haraka, viungo vya uzazi kwa wavulana havikui kwa haraka, uzito wa mtu unapungua, milango ya fahamu (kunusa na kuonja) haifanyi kazi vizuri, macho hayao ni vizuri hasa usiku, na ngozi haiwi katika hali nzuri. Kila binadamu anahitaji madini ya zinc lakini watoto, kina mama wajawazito na wale wanaonyonyesha wanahitaji zaidi madini hayo. Yaani mahitaji yao ni makubwa kuliko watu wengine. Vyakula vingi vya Kiafrika vina madini ya zinc. Hata hivyo, mtu anaweza kuwa na upungufu wa madini ya zinc kama hatakula mlo kamili. Vile vile ikumbukwe kuwa, kama ilivyo madiniya chuma, uwezowa mwili kuweza kunyonya madini ya zinc kutoka katika vyakula tunavyokula unategemea sana aina ya vyakula mtu anavyokula, wakati huo anapokula vyakula vyenye madini ya zinc. Kwa mfano, vyakula vya nyuzi nyuzi na nafaka zisizokobolewa hupunguza uwezo wa mwili kunyonya madini ya zinc kutoka katika vyakula tunavyokula. Vyakula vyenye madini ya zinc kwa wingi ni kama vile nyama, samaki, nafaka, mboga, jamii ya kunde (maharage, njegele, kunde, n.k.) na maziwa ya mama. Jambo la kuzingatia ni kwamba kila mlo (wa asubuhi, mchana au usiku) lazima uwe mlo kamili. Yaani uwe na makundi yote sita ya virutubisho kama tulivyoona katika makala za nyuma. |
YALIYOMO
'White Paper ni ulaghai wa Serikali ya CCM' Na Mwandishi wetu Sheikh Omar Bashir awekwa rumande
Mpango wa 'Kupindua' uongozi
wa Bakwata: Masheikh Dar waitwa polisi kuhojiwa
Zahrau Day yatikisa Tanga
MAKALA: Hatuna haja ya maelekezo ya
yule aliyetufikisha hapa
Huduma za afya Kondoa haziridhishi
Tunahitaji 'UN' ya Waislamu!
Hoja binafsi: Wawekezaji watuondokesha makwetu Jamii inapokuwa soko huria...
Someni kwa ajili ya Allah - Sheikh
Baruti
Madrasa Al-Ii'Tiswamu
Al-Umaahaati Fiisabiililillah - Moro
Madrasat Hidayat Mbagala
Hali ya Uislamu Moro
Vijijini yazidi kuwa mbaya
Sheikh Masoud Mwinyi awaonya
Waislamu kuacha migogoro Babati
Tusikaribishe mfungo wa Ramadhani
kwa Vunja Jungu
'Acheni zinaa muepukane
na ukimwi'
Wavunja jungu watahadharishwa
Hoja/Uchambuzi:
Njia ya uzimani ni nyembamba,
waionao ni wachache
Habari:
Kesi ya Waislamu Mwembechai
yaahirishwa kwa mara nyingine
Kongomano la wanawake wa
Kiislamu Bagamoyo
Sayansi na Teknolojia
Chakula na lishe
|