|
|
|
• Barabara nazo zitaabani
Na Abu Zubeir Wakati nchi ikijiandaa kuingia karne ya 20 ambayo hutajwa kuwa ni ya Sayari na teknolojia, hali ya huduma za afya kijiji cha Berera tarafa ya Bereko Wilayani Kondoa ni mbaya. Uchunguzi unaonyesha kwamba wananchi wa kijiji hicho wamekuwa wakipata usumbufu wa kusafiri kwa miguu kwa umbali wa kilometa tisa hadi kijijicha Kikiri kwa ajili ya kupata matibabu. Wanakijiji wa Bereko walimfahamisha mwandishi wa habari adha wanayoipata pale mgonjwa anapkuwa katika hali mbaya. Wamesema hulazimika kumpeleka Kondoa mjini ambako ni umbali mkubwa kutoka kijijini hapo. Kijana mmoja aliyejitambulisha kwa jina la Idrisa ambaye ni mfanyabiashara alimweleza mwandishi kuwa wanawake waja wazito hulazimika kusafiri hadi Kondoa mjini kwa tahadhari ya matatizo yanayoweza kutokea wakati wa kujifungua. Wakati huo huo, hali ya barabara Wilayani Kondoa ni mbaya sana kiasi cha kutishia kusimama shughuli mbali mbali za wakazi wa wilaya hiyo katika kipindi cha mvua. Maeneo ambayo huenda yakaathirika zaidi katika kipindi hicho ni Bakulu na Nasawi Kichangani (Kisangani). Wakazi wa sehemu hizo wamemweleza mwandishi kuwa ingawa hivi sasa yamemwagwa malori saba ya changarawe kwa ajili ya ukarabati, wana wasi wasi wa kudumu kwa mawe hayo wakati wa mvua. Akiongea na mwandishi, mkazi mmoja wa vijiji hivyo Bwana Ilovya alisema wafanya kazi wa idara ya ujenzi hufika mara kadhaa sehemu hizo lakini hakuna matengenezo yoyote waliyofanya katika barabara hizo. "Tunaiomba Serikali itupie jicho barabara hizi hivi sasa kwani mvua zikianza hakutakuwa na mawasiliano kabisa hasa pale yanapotokea magonjwa ya milipuko", alisisitiza Bwana Ilovya. Wakati wa kampeni za uchaguzi mwaka 1995 aliyekuwa mgombea wa chama
tawala (Rais Benjamin Mkapa) aliahidi kuimarishwa kwa miundo mbinu ili
kuchochea maendeleo ya wananchi katika sehemu mbalimbali za nchi. Tangu
wakati huo imeelezwa kuwa hapajafanyika lolote lenye kuashiria kutekelezwa
ahadi hiyo.
|
YALIYOMO
'White Paper ni ulaghai wa Serikali ya CCM' Na Mwandishi wetu Sheikh Omar Bashir awekwa rumande
Mpango wa 'Kupindua' uongozi
wa Bakwata: Masheikh Dar waitwa polisi kuhojiwa
Zahrau Day yatikisa Tanga
MAKALA: Hatuna haja ya maelekezo ya
yule aliyetufikisha hapa
Huduma za afya Kondoa haziridhishi
Tunahitaji 'UN' ya Waislamu!
Hoja binafsi: Wawekezaji watuondokesha makwetu Jamii inapokuwa soko huria...
Someni kwa ajili ya Allah - Sheikh
Baruti
Madrasa Al-Ii'Tiswamu
Al-Umaahaati Fiisabiililillah - Moro
Madrasat Hidayat Mbagala
Hali ya Uislamu Moro
Vijijini yazidi kuwa mbaya
Sheikh Masoud Mwinyi awaonya
Waislamu kuacha migogoro Babati
Tusikaribishe mfungo wa Ramadhani
kwa Vunja Jungu
'Acheni zinaa muepukane
na ukimwi'
Wavunja jungu watahadharishwa
Hoja/Uchambuzi:
Njia ya uzimani ni nyembamba,
waionao ni wachache
Habari:
Kesi ya Waislamu Mwembechai
yaahirishwa kwa mara nyingine
Kongomano la wanawake wa
Kiislamu Bagamoyo
Sayansi na Teknolojia
Chakula na lishe
|