AN-NUUR 
Na.178 Shaaban  1419, Desemba 4 - 10, 1998 
 
Home Links Islam Tanzania Matoleo yaliyopita
 
Tunahitaji ‘UN’ ya Waislamu!
 

Na Twahir Rashid 

Upande! 

Mungu Mkubwa, Mungu Mkubwa, Mungu Mkubwa. Neno "Upande" ni lugha ya Kiswahili ambapo Kiarabu ni "Kibla" (2:177). Nalo neno hili kibla (upande wa kuelekeza nyuso zetu) limebatizwa na huitwa (Capital City) mji mkuu. 

Kibla! 

Mungu Mkubwa, Mungu Mkubwa, Mungu Mkubwa. Kauli hii "tunahitaji "UN" ya Waislamu", labda tusema "UN-dhana" ni ya madume matano yenye Turufu (VETO). Bali tunahitaji "UN" ya walimwengu wote. 

Na hapa tuingize fikra hii. Kwamba Mwenyezi Mungu hakuna kitu alichokiacha bila kukiweka wazi ndani ya kitabu chake (Quran). "UN ya Mataifa yote ilishaundwa na Mwenyezi Mungu na kUtiwa zege na Mtume Muhammad (s.a.w.) pale alipogeuzwa katika kibla akipendacho (2:144) nao ni upande wa msikiti mtakatifu, kwa kuacha upande (kibla) (kiini cha zamani) Baitil -Magdis. Na ni kwa nini alekee Makka? Basi fahamu kuwa "Nyumba ya kwanza iliyowekwa kwa ajili ya watu ni ile iliyoko Makka, yenye baraka na uongozi kwa ajili ya walimwengu wote." (3:96) Basi yule atakayekuwa maongozi yake hutokea mji huu, kwa maana wale wanaoelekea Makka kwa ajili ya maongozi ya maisha ya dunia yao na baraka; hao ndio wafuasi wa Mtume Muhammad (s.a.w.) (2:143).Kwa hiyo shibe na amani (106:3-4) watapata. Ili hali watakaoelekea mji mwingine usiokuwa huu(k.m. New York); njaa na khofu zitawasibu (106:3-4). Ndio Khaswa Mwenyezi Mungu atufanyiza Kampeni (anatuita)katika Nyumba (Ikulu) ya amani (10’25) - lakini watu leo tumefikishwa katika nyumba (Ikulu) ya Maangamizo (14:28) humo tukaagizwa kuwa watoto na moja kwa moja dini kuvurugwa (6:137). 

Kwa hiyo kuwa na Katibu Mkuu (Khalifa) ndio sawa. Ila Kofi 

Anan ahame kutoka Ikulu ya Maangamizo (14:28) (New York), ahamie Ikulu Kongwe (22:29) (Makka), kwani Katibu Mkuu (Khalifa) hana lake jambo ila kufuata Buku atakalolikuta katika Nyumba atakayosimama (2:125). 

Kwa hayo jua basi, Waislamu ni wale ambao mji wao mkuu (mji wanaowatajia watoto wao) ni Makka kwa hiyo Kofi Anan wao makao (ofisi) yake yapo Makka (27:91).Kinyume na hivyo ni kushirikisha (6"148). 

Ndio hivyo tunapo ambiwa turejee kwa Menyezi Mungu maana yake ni kwamba sasa hivi tupo katika uongozi wa Majumba (Ikulu) ya shetani (UN-New York) (ambavyo Ikulu hii imeshikana Ikulu yote ya kila nchi mpaka ofisi za vijiji). Kwa hiyo tutoke humo turejee katika (Ikulu ) ya Mwenyezi Mungu (UN-Makka). Na tayari UN-Makka ina ofisi zake mpaka Vijijini nayo ndio misikiti (72:18). 

Misikiti! 

Mungu Mkubwa, Mungu Mkubwa, Mungu Mkubwa. Ndugu yangu Said Rajab swali lako. Je! Waislamu wa dunia nzima, wakati haujafika tu wa kuwa na "UN’ ya Waislamu.....? Basi fahamu kuwa kizazi cha Israel kilichukuwa ahadi (2:40) (lakini) waliificha haki (2:42, 2:146) nayo ni kuelekea Makka (2:144, 2:147) kwa maongozi ya dunia nzima (3:96). Wao wakaasi na kuruka mipaka pale walipokataa (maongozi)ya Mwenyezi Mungu na kuwaua manabii. Kwa hiyo wakapingwa juu yao chapa ya dhila na umasikini (2:61) mpaka leo hawana nchi. Wamepigwa chapa ya dhila popote wanapokuweka, ila (kwa kushika)kamba (dini) ya Mwenyezi Mungu (uogozi wa UN-Makka) au kamba ya watu (UN-New York) (Amerika Inawasaidia).... (3:112) na imewasimika Palestine. Kwa hiyo juhudi zimefanyika kuficha ukweli huu wa UN ya walimwengu wote (3:96) ambayo ndiyo tengenezo la maisha ya watu (5:97) baada ya kuharibiwa (2:12-11). Hivyo maongozi ya watu (Serikali) Majeshi, Mashule, na Nyumba za Mungu (Makanisa, Misikiti, Mapagoda n.k.)vyote vimehujumiwa (17:64) zimeshikwa na shetani. Na kutumiwa kupotosha ukweli. 

Wanaostahiki kuamirisha misikiti (ofisi za Mwenyezi Mungu) kwa ajili ya uongozi khaswa (2:120) ni wale 

1. Wanaomuamini Mwenyezi Mungu 
2. Na siku ya Mwisho 
3. Husimamisha swala 
4. Hutoa zaka 
5.Hawamuogopi yeyote ila Mwenyezi Mungu (9:18). 

Eh! Mola wangu, mimi ni mja wako 
Mikono nimekunyoshea 
Thelathini na sita miaka, tangu kijijini eti nini? nikatafute elimu. 

Na hivi imetimu ishirini na tano 
Miaka, tangu wanibwage mjini (2:61) 
Kufanya kazi ndiyo dini yangu 
Yote hayo wanisumbuliani? Tumbo? 

Unyonge umekithiri, umasikini ndio usiseme. Manabii wa leo (Mbwechai) wauawa (2:61) neno la Mwenyezi Mungu kosa. 

Ilivyokuwa kwa mfalme wa Yemen ndivyo hivi leo. Mfalme wa Marekani kafanya aliyoshindwa Mfalme wa Yemen na watu wote hata Saudia na Iran wana wajumbe wa kudumu katika Kibla cha New York Wamegeuzwa bila kujua (40:63). Ni nguvu ya mkono wako sasa tunayoienzi. Kwa sababu mfalme hupambana na mfalme mwenzake. Watu wanakutaka sasa uwaongoze uwatoe katika giza uwapeleke katika Nuru (2:257). 
 

Juu 
 

YALIYOMO 
 
 
'White Paper  ni ulaghai wa  Serikali ya CCM' 
Na Mwandishi wetu 

Sheikh Omar Bashir awekwa rumande 
Na Mwandishi Wetu 

Mpango wa 'Kupindua' uongozi wa  Bakwata: Masheikh Dar waitwa polisi kuhojiwa 
Na Mwandishi Wetu 

Zahrau Day yatikisa Tanga 
Na Mwandishi Wetu 

MAKALA: Hatuna haja ya maelekezo ya yule aliyetufikisha hapa  
Na Alhaj Yusuf Kalala, Washington DC USA 

Huduma za afya Kondoa haziridhishi 
Na Abu Zubeir 

Wasemavyo wanaharakati 

Tunahitaji 'UN' ya Waislamu! 
Na Twahir Rashid 

Hoja binafsi: Wawekezaji watuondokesha makwetu 

Jamii inapokuwa soko huria...  
Na Said Rajab 

Someni kwa ajili ya Allah - Sheikh Baruti  
Na Muhibu Said 

Madrasa Al-Ii'Tiswamu Al-Umaahaati Fiisabiililillah - Moro 
Na Rajab Rajab, Morogoro 

Madrasat Hidayat Mbagala 
Na Mussa Salum  

Hali ya Uislamu Moro Vijijini yazidi kuwa mbaya  
Na Rajab Rajab, Morogoro 

Sheikh Masoud Mwinyi awaonya Waislamu kuacha migogoro Babati  
Na Abu Zuberi - Babati 

Tusikaribishe mfungo wa Ramadhani kwa Vunja Jungu  
Na Abeid Poyo 

'Acheni zinaa muepukane na ukimwi'  
Na Mussa Salum 

Wavunja jungu watahadharishwa 
Na Mwandishi Wetu, Morogoro 

Hoja/Uchambuzi: 
Je, hivi tuendelee kushika amri za Mungu tena? 
Na Mwinjilisti Bunga E. Dettu 

Njia ya uzimani ni nyembamba,  waionao ni wachache 
Na Yasin Valerian Massawe 

Habari: 
Semina ya Maimamu Tanga yadai: Maimamu wanapuuzwa  
Na Mwandishi Wetu 

Kesi ya Waislamu Mwembechai yaahirishwa kwa mara nyingine  
Na Muhibu Saidi 

Kongomano la wanawake wa Kiislamu Bagamoyo 
Na Mwandishi Wetu 

Sayansi na Teknolojia 
[Kuongeza RAM kwenye Kompyuta] 
 
Masomo ya Dini ya Kiislamu 

Barua za Wasomaji 

Mashairi 

Chakula na lishe 
[Madini ya Zinc] 

   Kutoa maoni yako kuhusu ukarasa huu: Bonyeza hapa
Au
Andika barua  kwa: webmaster@islamtanzania.org
 
Home Links Islam Tanzania Matoleo yaliyopita