AN-NUUR 
Na.178 Shaaban  1419, Desemba 4 - 10, 1998 
 
Home Links Islam Tanzania Matoleo yaliyopita
 
‘White Paper ni ulaghai wa Serikali ya CCM’

• Moto utalipuka wananchi waking’amua 

• Rais asiwe muweza wa yote 
 

Na Mwandishi Wetu 

MWANASIASA mkongwe nchini Bw. Christopher Kassanga Tumbo amesema kwamba utaratibu wa kuifanyia marekebisho Katiba kupitia White Paper huku wananchi wakitakiwa watoe maoni yao ni kuleta ulaghai. 

Akifafanua kauli yake hiyo, Balozi Kassanga Tumbo alisema kwamba ni kuwaghilibu wananchi kuwataka watoe maoni katika jambo ambalo hawatakuwa na kauli ya uamuzi. 

Alisisitiza kwamba maoni ya wananchi yangekuwa na maana kama hatimae pangekuwepo na kura ya maoni. 

Balozi Kassanga Tumbo ambaye alikuwa akizungumza katika kipindi cha Kiti Moto kama kilivyorushwa na ITV usiku wa Jumatano Desemba 3, mwaka huu, amesema kwamba White Paper kama utaratibu wa kuibadili Katiba una dosari kubwa mbili: Kwanza umevitenga vyama vingine vya siasa na pili wananchi wanaoulizwa hawana kauli ya uamuzi. 

Amesema utaratibu huu wa White Paper ni namna nyingine ya kuwaghilibu wananchi na akatahadharisha kwamba moto utakuja kulipuka pindi wananchi watakapotambua kwamba wamekuwa wakighilibiwa. 

Amezitaja ghilba nyingine ambazo zimekuwa zikifanywa na serikali kwamba ni pamoja na kuwaundia wafanyakazi vyama ambavyo haviwakilishi matakwa yao wala kutetea maslahi yao. 

Ametaja majina ya NUTA, JUWATA, OTTU na TFTU kwamba ni majina tofauti lakini yanayowakilisha vyama vilivyodhibitiwa na CCM na serikali yake na hivyo kukosa nguvu ya kutetea maslahi ya wafanyakazi. Amehoji inakuwaje chama cha wafanyakazi kiongozwe na kada wa CCM. 

Bw. Kassanga Tumbo ambaye ni miongoni mwa waasisi na wapigania mfumo wa siasa wa vyama vingi nchini, amesema kwamba nao hivi sasa kama kambi ya upinzani wanawaelimisha wananchi na wana mapendekezo yao ya Katiba. 

Amesema yeye binafsi anapendekeza mfumo wa Shirikisho kwani ndio mfumo pekee unaozuia madikteta. Amesema kama wakuu wa mikoa na wilaya watachaguliwa na wananchi basi watawajibika kwao zaidi kisiasa kuliko hivi sasa. 

Aidha, alisema kwamba haifai Rais wa nchi kuwa na mamlaka makubwa na kumfanya kuwa muweza wa yote. Hali hiyo amesema kwamba huzaa udikteta. 
 
 

Juu 
 

YALIYOMO 
 
 
'White Paper  ni ulaghai wa  Serikali ya CCM' 
Na Mwandishi wetu 

Sheikh Omar Bashir awekwa rumande 
Na Mwandishi Wetu 

Mpango wa 'Kupindua' uongozi wa  Bakwata: Masheikh Dar waitwa polisi kuhojiwa 
Na Mwandishi Wetu 

Zahrau Day yatikisa Tanga 
Na Mwandishi Wetu 

MAKALA: Hatuna haja ya maelekezo ya yule aliyetufikisha hapa  
Na Alhaj Yusuf Kalala, Washington DC USA 

Huduma za afya Kondoa haziridhishi 
Na Abu Zubeir 

Wasemavyo wanaharakati 

Tunahitaji 'UN' ya Waislamu! 
Na Twahir Rashid 

Hoja binafsi: Wawekezaji watuondokesha makwetu 

Jamii inapokuwa soko huria...  
Na Said Rajab 

Someni kwa ajili ya Allah - Sheikh Baruti  
Na Muhibu Said 

Madrasa Al-Ii'Tiswamu Al-Umaahaati Fiisabiililillah - Moro 
Na Rajab Rajab, Morogoro 

Madrasat Hidayat Mbagala 
Na Mussa Salum  

Hali ya Uislamu Moro Vijijini yazidi kuwa mbaya  
Na Rajab Rajab, Morogoro 

Sheikh Masoud Mwinyi awaonya Waislamu kuacha migogoro Babati  
Na Abu Zuberi - Babati 

Tusikaribishe mfungo wa Ramadhani kwa Vunja Jungu  
Na Abeid Poyo 

'Acheni zinaa muepukane na ukimwi'  
Na Mussa Salum 

Wavunja jungu watahadharishwa 
Na Mwandishi Wetu, Morogoro 

Hoja/Uchambuzi: 
Je, hivi tuendelee kushika amri za Mungu tena? 
Na Mwinjilisti Bunga E. Dettu 

Njia ya uzimani ni nyembamba,  waionao ni wachache 
Na Yasin Valerian Massawe 

Habari: 
Semina ya Maimamu Tanga yadai: Maimamu wanapuuzwa  
Na Mwandishi Wetu 

Kesi ya Waislamu Mwembechai yaahirishwa kwa mara nyingine  
Na Muhibu Saidi 

Kongomano la wanawake wa Kiislamu Bagamoyo 
Na Mwandishi Wetu 

Sayansi na Teknolojia 
[Kuongeza RAM kwenye Kompyuta] 
 
Masomo ya Dini ya Kiislamu 

Barua za Wasomaji 

Mashairi 

Chakula na lishe 
[Madini ya Zinc] 

   Kutoa maoni yako kuhusu ukarasa huu: Bonyeza hapa
Au
Andika barua  kwa: webmaster@islamtanzania.org
 
Home Links Islam Tanzania Matoleo yaliyopita