AN-NUUR 
Na.171 Jamadul Akhir 1419, Oktoba 16 - 22, 1998 
 
Home Links Islam Tanzania Matoleo yaliyopita
 
 
Upimaji huu mpya ni wa nini 
  

Na Mwandishi Wetu 

ZOEZI la kuchoma nyumba za wananchi huko Nzasa limekuwa likienda sambamba na upimaji wa eneo hilo na kuweka mpaka mpya. 

Upimaji huo unajumuisha kuchimba mashimo makubwa, kupaka rangi miti na kuweka maboya (beacon) mapya.  

Baadhi ya maboya mapya yaliyoyashuhudiwa Mwandishi wa Habari hizi yamepewa Namba. FD KZ 76 na FD KZ 77. Nyingine ni FD KZ 68, FD KZ 120, FD KZ 121 na FD KZ 122. 

Ambacho wanauliza wananchi ni je; upimaji huu mpya ni wa nini? Je, ni upanuzi wa mipaka ya Msitu, uandaaji wa eneo la amani au kinga (buffer zone) au ni kitu gani hasa. 

Kutaka kujua zaidi AN-NUUR iliwasiliana na Mkurugenzi wa Misitu na Nyuki (Wizarani), Prof. Idd Saidi. Hata hivyo Prof. Idd alikataa kabisa  

kuzungumzia suala hilo la upimaji na kumtaka Mwandishi awasiliane na Mkuu wa Mkoa wa Pwani au Waziri. 

Baada ya kuelezwa kwamba Mhe. Waziri Zakia Meghji kaenda Sumbawanga AN-NUUR iliwasiliana na Katibu Mkuu, Bw. Luhanjo ambaye naye hakuweza kufafanua upimaji huo mpya ni wa nini. 

Ila Katibu Mkuu huyo wa Wizara ya Maliasili na Utalii alisisitiza kwamba upimaji huo mpya hauwezi kuwa ni upanuzi wa mipaka (extension) ya msitu kwani itakuwa ni kinyume cha sheria. Alisema kwamb a upanuzi ni lazima ufuate sheria ya misitu inayoagiza kutangazwa upanuzi huo katika gazeti la Serikali na kufuatwa taratibu nyingine zote zinazohitajika kisheria. 

Baadhi ya wafanyakazi wa Idara hiyo walioongea na Mwandishi wa Habari hizi kwa "sharti" la kutowataja japo kwa ishara tu, wamesema kwamba zoezi linalofanyika sasa hivi ni kupima kuweka mipaka na wakati huo huo, kuchora ramani. Lakini na wao hawajui endapo ramani hiyo mpya itakuwa ndiyo ramani ya Kazimzumbwe au ni eneo jipya linalotengwa nje ya mipaka ya msitu wa Kazimzumbwe. 

Haikuweza kufahamika mara moja ni kwa vipi Mkurugenzi wa Idara ya Misitu katika Wizara; ambaye pia ni Profesa wa Misitu akatae kuzungumzia upimaji huu na aagize aulizwe Mkuu wa Mkoa. 

Hata hivyo, alisema Profesa Iddi ilikuwa kwamba chanzo cha habari ni lazima kiwe kimoja ama Waziri au Mkuu wa Mkoa wa Pwani. 

Kwa kuwa wananchi wanadai kwamba zilikochomwa nyumba zao ni nje ya mipaka ya msitu na upimaji na uwekaji mipaka mipya unaendelea kwa kasi, Serikali ieleze upimaji huu na mipaka hii ni ya nini? 

Juu 
 

YALIYOMO 
 
 
TAHARIRI 
Serikali iwahurumie wananchi wake 

KUCHOMWA MOTO NYUMBA ZA WANANCHI: Nzasa wamtaka Mkapa awaonyeshe pa kwenda 
Na Mwandishi Wetu, Nzasa 

Mishikaki ya nguruwe Moshi yachomwa mbele ya Msikiti 
Na Mwandishi Wetu 

MAONI YETU: 
Je; ni halali kuchoma Kidungu cha mtu? 

Upimaji huu mpya ni wa nini 
Na Mwandishi Wetu 

TANGAZO LA HIFADHI YA MSITU WA KAZIMZUMBWI 

Ndoa si lengo, ni wasila wa kufikia lengo 
Na Bi. Zuhura Tajiri, Shinyanga 
 
Teknologia:
Jifunze kuunganisha Kompyuta
Na Hassan Omar

Makala:
Nani atakayewahoji Waheshimiwa hawa

Goda Muslim School, Manzese
Na Mwandishi Wetu

Utabiri sahihi wa kuibuka kwa Uislamu
Na Sheikh Bernard P. Nyangasa

Historia ya mgogoro wa Nzasa
Na Mwandishi Wetu

DUMT watoa msaada kwa walioathirika Nzasa
Na Mwandishi Wetu

UCHOMAJI NYUMBA NZASA: Wafadhili wana mchango gani?
Na Mwandishi Wetu

Mafundisho ya Quran 
Kutoa pasipo masimango 

Barua za wasomaji 

Masomo ya dini ya Kiislam 

Chakula na Lishe 

 

   Kutoa maoni yako kuhusu ukarasa huu: Bonyeza hapa
Au
Andika barua  kwa: webmaster@islamtanzania.org
 
Home Links Islam Tanzania Matoleo yaliyopita