AN-NUUR
Na.157 Rabi' Awal 1419, Julai 10 - 16, 1998
 
Home Links Islam Tanzania Matoleo yaliyopita
 
Sheikh Bafadhil aitaka Bakwata iwe mtetezi wa Waislamu 
  • Asema Waislamu ni yatima
  • Azungumzia kufa kwa maadili 
Na Mwandishi Wetu 

SHEIKH Mkuu wa Mkoa wa Morogoro na Mjumbe wa Kamati ya Maulamaa Taifa, Sheikh Omar Bafadhil ameitaka Bakwata kuwa mtetezi wa Waislamu badala ya kuwa mbali nao. 

Aidha, Sheikh huyo aliitaka Bakwata kufungua ukurasa mpya wa mahusiano baina yake na Waislamu inaodai kuwaongoza kwa kutetea haki mbalimbali kwa mujibu wa katiba ya nchi. 

Sheikh Omar aliyasema hayo katika sherehe za Maulid zilizofanyika kitaifa wilayani Bagamoyo mkoa wa Pwani usiku wa Jumatatu Julai 6, 1998. 

Huku akisindikizwa kwa takbira toka kwa Waislamu waliofika katika Maulid hayo, Sheikh Bafadhil alisema kwamba hivi sasa Waislamu nchini Tanzania ni kama watoto yatima, hawana mtetezi na Bakwata ambayo ingepaswa kuwa na jukumu hilo imekuwa mbali nao. 

"Wakati umefika Bakwata kufungua ukurasa mpya ili iwe mtetezi wa haki za Waislamu kwa mujibu wa Katiba ya nchi", alisema Sheikh Umar huku akisisitiza kwamba kuyasema hayo si kuleta fitina katika jamii. 

Akizungumzia mmomonyoko wa maadili nchini, Sheikh Bafadhil alisema kwamba, jamii ya Watanzania imekumbwa na wimbi la maovu ambapo ulevi na zinaa vimeshika kasi. 

Aliwataka wazazi kusimamia kikamilifu suala la malezi ya vijana ambao alisema wao ni uti wa mgongo wa Taifa. 

Huku akirejea makaripio ya Mtume Muhammad (s.a.w) kuhusu pombe, aliitaka serikali iache kutengeneza na kugiza pombe kwani kwa kufanya hivyo inajenga taifa la walevi ambalo halitakuwa na hadhi. 

"Hao wanaotuletea makontena ya ulevi waelezeni watuletee chakula", alisisitiza Sheikh Bafadhil. 

Aidha, aliwashutumu wale wanaoshajiisha matumizi ya kondomu kwamba wanachochea uzinifu katika jamii ya Watanzania hivyo kuipeleka katika maangamizi ya ukimwi. 

"Mtu asiwadanganye eti muwape watoto kondomu ili wajikigne na ukimwi, huko ni kuwachochea wafanye ufuska", alisema kwa ukali huku akiwatakawazazi wasimamie malezi pamoja na kuwataka wanawake wavae mavazi ya stara. 

Katika hotuba yake hiyo iliyoonekana kuvuta masikio ya wengi, Sheikh Omar aligusia pia shutuma zilizotolewa na kiongozi mmoja hivi karibuni dhidi ya Rais Mstaafu, Mzee Ali Hassani Mwinyi. 

Sheikh Omar alisema kwamba, aliyoyasema Mzee Mwinyi kuhusu vyombo vya Waislamu na umuhimu wa umoja miongoni mwao hayana budi kufanyiwa kazi na wahusika badala ya kushutumiwa. 

"Lazima tuwaheshimu viongozi wetu wastaafu, Mzee Ali Hassan Mwinyi na Mzee Jumbe, alisema Sheikh Omar huku akikazia aliyoyasema katika hotuba yake ambayo ilisikika nchi nzima kupitia RTD kuwa fursa hiyo aliyoipata ni kama amenawa mikono, akimaanisha amefikisha ujumbe. 

Akimalizia hotuba yake aliwataka Watanzania kudumisha amani nchini na kujiepusha na matendo yote yanayoweza kuvuruga amani hiyo. 

"Siku zote tumekuwa tukipokea wakimbizi wa nchi jirani, tusije nasi tukawa wakimbizi, fumbo mfumbie mjinga, mwerevu atambue". 

Sherehe hizo za Maulid zilihudhuriwa pia na Makamu wa Rais, Dk. Omar Juma na viongozi wengine wa serikali. 
 

Juu 
 

YALIYOMO
 

TAHARIRI 

Maoni yetu: Prof. Juma Kapuya, vipi Muislamu usijue agenda za Waislamu? 

Hatimaye Mzee Katambo, Chata waachiwa
Na Mwandishi wetu

Polisi Newala wajenga Msikiti 

Sheikh Bafadhil aitaka Bakwata iwe mtetezi wa Waislamu
Na mwandishi wetu

Makala: Uinjilisti wa Mbuni haufai
Na Rajabu Mbambwa, Kigoma

Mussa Katambo: Mzee aliyewekwa rumande kwa kuandaa mihadhara

Ukweli usiachwe 

Makala: Elimu ya ngono yapenyezwa tena Zanzibar 
Na Saidi Mzee 

Arusha wasema: Hongera Mhe. KK kwa kuwa mfano mwema 
Na Hussein M.,  Arusha 

Wanawake Songea kuandaa maonesho 
Na. Jumah Mbwana, Songea 

Kesi ya mgogoro wa Ardhi
Na. Mustafa Adam 

AN-NUUR marufuku gerezani? 
Na Mwandishi Wetu 

Waislamu Karagwe wadai kusalishwa na imamu asiyejua kutawadha 
Na. Abu Abdallah 

Ofisi mpya za Rabita 
Na Mwandishi Wetu

Barua za wasomaji

Habari za Madrasa

Masomo

 

 

 
 Kutoa maoni yako kuhusu ukarasa huu:
Bonyeza hapa
Au
Andika barua  kwa: webmaster@islamtanzania.org
 
Home Links Islam Tanzania Matoleo yaliyopita