|
|
| . AN-NUUR
marufuku gerezani?
Na Mwandishi Wetu MAGEREZA ya Keko na Segerea yamedaiwa kuzuia gazet la ANU-NUUR kuingia gerezani kwa sababu zisizofahamika. Watuhumiwa walioachiwa hivi karibuni wamesema kwamba walipokuwa mahabusu katika magereza hayo waliruhusiwa kupokea magazeti yote kutoka kwa jamaa zao ispokuwa AN-NUUR . "Hata magazeti ya Kiongozi na Msema Kweli yanaruhusiwa gerezani lakini AN-NUUR haliruhuisiwi", wamedai watuhumiwa hao. Haikuelezwa sababu hasa za kuzuiliwa gazeti hili gerezani lakini habari ambazo hazikuweza kuthibitishwa zimefahamisha kwamba baadhi ya maaskari wamesikika wakisema kuwa AN-NUUR gazeti la uchochezi na kwamba linapigwa marufuku. Jitihada za kuwaona wahusika wakuu wa magereza hayo kuhusiana na suala hili, hazikuweza kufanikiwa.
Waislamu Karagwe wadai kusalishwa na imamu asiyejua kutawadha Na. Abu Abdallah WAISLAMU wa Kata ya Kituntu, Wilaya ya Karagwe, Mkoani Kagera wameilalamikia ofisi ya BAKWATA Mkoa wa Kagera kufuatia kitendo cha ofisi hiyo ikishirikiana na ofisi ya Wilaya kuwachagulia viongozi wanaodai hawajui hata kutawadha na kusoma suratul fatiha. Alipohojiwa na mwandishi wa habari hizi uchaguzi huo ulizingatia vigezo gani. Mmoja wa viongozi wa BAKWATA ajilibu kuwa waliochaguliwa ni BAKWATA damu. Waumini wa Karagwe wamedai wapo katika hatua za mwisho kuwakilisha malalamiko yao kwa Mufti wa BAKWATA Sheikh Hemed Bin Jumaa bin Hemed Jumaa. Na Mwandishi Wetu OFISI za Rabita - Muslim World League (Tanzania) zimehamia katika ofisi za International Islamic Releaf Organization (IIRO) MTAA WA Uhuru na Congo. Hatua hii inafuatia kuteuliwa kwa Alhaj Hassan Mnjeja kuwa mkurugenzi mpya wa Ratiba (T). Sheikh Muhammad Rukara Khalfan, mkurugenzi wa zamani amehamishiwa Gabon. |
Maoni yetu: Prof. Juma Kapuya, vipi Muislamu usijue agenda za Waislamu? Hatimaye Mzee Katambo, Chata waachiwa
Sheikh Bafadhil aitaka Bakwata iwe
mtetezi wa Waislamu
Makala: Uinjilisti wa Mbuni haufai
Mussa Katambo: Mzee aliyewekwa rumande kwa kuandaa mihadhara Makala: Elimu ya ngono yapenyezwa
tena Zanzibar
Arusha wasema: Hongera Mhe. KK kwa
kuwa mfano mwema
Wanawake Songea kuandaa maonesho
Kesi ya mgogoro wa Ardhi
AN-NUUR marufuku
gerezani?
Waislamu Karagwe wadai kusalishwa
na imamu asiyejua kutawadha
Ofisi mpya za Rabita
|