|
|
| Wanawake Songea
kuandaa maonesho
Na. Jumah Mbwana, Songea VUGUVUGU la maonesho ya mavazi ya Wanawake wa Kiislamu (Hijab) mjini Songea linazidi kupamba moto. Maonesho hayo ambayo yatafanyika Julai 25, 1998 mjini Songea ni ya aina yake na ya kwanza kufanyika hapa nchini. Waandaaji wa maonesho hayo Ofisi ya AL-MALLID Kanda ya Kusini yenye Makao yake mjini hapa wamesema maonesho hayo yatawashirikisha Wanawake kutoka mikoa mbalimbali ya Tanzania ambapo idadi yao inakadiriwa kufikia elfu ishirini (20,000/-). Wanawake wengi mkoani hapa wamekuwa wakifurika katika ofisi hizo ili pamoja na kutaka kujua utaratibu wa maonesho hayo pia washoneshe vazi hilo. Wanawake waliohojiwa na Mwandishi wa Habari hizi wamesema wamefurahishwa kwa kuandaliwa maonesho hayo ambayo wameyaita kuwa ni ya kihistoria hapa nchini kwani vazi la Hijab machoni mwa watu linaonekana kuwa ni vazi ambalo limepitwa na wakati. "Vazi la Hijab ni la lazima kwa mwanamke kwani ni amri ya Mwenyezi Mungu hivyo anasema kuwa vazi hilo limepitwa na wakati basi yeye mwenye kusema maneno hayo ndiye aliyepitwa na wakati", wamesema wanawake hao. Maonesho ya Songea yanafanyika huku kukiwa na wimbi la maonesho yanayoshusha hadhi ya mwanamke nchini kote na hasa katika jiji la Dar es Salaam. Imeelezwa kuwa maonesho hayo ya Songea ni changamoto kwa vikundi na jumuiya za wanawake zenye kupigania hadhi ya mwanamke. Katika maonesho hayo pia kutakuwa na kongamano ambalo litajadili haki za mwanamke wa Kiislamu na miradi mbalimbali ya wanawake itazinduliwa. Ili kufanikisha maonesho hayo, wanawake wa mkoa wa Ruvuma wameunda jumuiya yao ya wanawake wa Kiislamu na kuchagua viongozi watakaoongoza jumuiya hiyo. Waliochaguliwa kuongoza jumuiya hiyo ni kama ifuatavyo:- Bi Hidaya Haji, Mwenyekiti, Bi. Mwanaidi Saidi, Makamu Mwenyekiti, Bi
Zalia A. Gaula, Katibu, Bi Sophia Mdoka, Katibu Msaidizi na Mwajuma Tafai,
Mweka Hazina.
|
Maoni yetu: Prof. Juma Kapuya, vipi Muislamu usijue agenda za Waislamu? Hatimaye Mzee Katambo, Chata waachiwa
Sheikh Bafadhil aitaka Bakwata iwe
mtetezi wa Waislamu
Makala: Uinjilisti wa Mbuni haufai
Mussa Katambo: Mzee aliyewekwa rumande kwa kuandaa mihadhara Makala: Elimu ya ngono yapenyezwa
tena Zanzibar
Arusha wasema: Hongera Mhe. KK kwa
kuwa mfano mwema
Wanawake Songea kuandaa maonesho
Kesi ya mgogoro wa Ardhi
AN-NUUR marufuku
gerezani?
Waislamu Karagwe wadai kusalishwa
na imamu asiyejua kutawadha
Ofisi mpya za Rabita
|