AN-NUUR
Na.157 Rabi' Awal 1419, Julai 10 - 16, 1998
 
Home Links Islam Tanzania Matoleo yaliyopita
 
Polisi Newala wajenga Msikiti 

WAKATI polisi na askari Magereza jijini Dar es Salaam wakiua na kuwatesa Waislamu kana kwamba wao hawana dini au hawamtambui Mungu, hali ni tofauti katika baadhi ya mikoa na wilaya. 

Habari ambazo AN-NUUR imezipata kutoka Newala zimeeleza kwamba, askari polisi wakishirikiana na askari Magereza wamejenga Msikiti karibu na ofisi na makazi yao ili waweze kufanya ibada kikamilifu. Msikiti huo ambao wameujenga katika eneo la Nangwala upo katika hatua za mwisho tayari kwa kuswaliwa. 

Askari hao imeelezwa kwamba wamechukua hatua hiyo baada ya kuwa miskiti mikuu miwili ya mjini Newala kuwa mbali na maeneo yao na hivyo kuwa taabu kwao kuwahi kuswali swala za jamaa. 

Lakufurahisha na kutia moyo ni kuwa, askari hao wamejenga msikiti huo kwa nguvu zao wenyewe za hali na mali. 

Habari za hivi karibuni zimeeleza kwamba msikiti huo hivi sasa unahitaji milango, madirisha na mazulia tayari kwa kuanza kuswaliwa. 

Waislamu wameombwa kuunga mkono juhudi za askari hao kwa kusaidia vifaa hivyo. Msaada wowote waweza kupitishiwa kwa uongozi wa Masjid Hidaya wa mjini Newala. 

Juu 
 

YALIYOMO
 

TAHARIRI 

Maoni yetu: Prof. Juma Kapuya, vipi Muislamu usijue agenda za Waislamu? 

Hatimaye Mzee Katambo, Chata waachiwa
Na Mwandishi wetu

Polisi Newala wajenga Msikiti 

Sheikh Bafadhil aitaka Bakwata iwe mtetezi wa Waislamu
Na mwandishi wetu

Makala: Uinjilisti wa Mbuni haufai
Na Rajabu Mbambwa, Kigoma

Mussa Katambo: Mzee aliyewekwa rumande kwa kuandaa mihadhara

Ukweli usiachwe 

Makala: Elimu ya ngono yapenyezwa tena Zanzibar 
Na Saidi Mzee 

Arusha wasema: Hongera Mhe. KK kwa kuwa mfano mwema 
Na Hussein M.,  Arusha 

Wanawake Songea kuandaa maonesho 
Na. Jumah Mbwana, Songea 

Kesi ya mgogoro wa Ardhi
Na. Mustafa Adam 

AN-NUUR marufuku gerezani? 
Na Mwandishi Wetu 

Waislamu Karagwe wadai kusalishwa na imamu asiyejua kutawadha 
Na. Abu Abdallah 

Ofisi mpya za Rabita 
Na Mwandishi Wetu

Barua za wasomaji

Habari za Madrasa

Masomo

 

 

 
 Kutoa maoni yako kuhusu ukarasa huu:
Bonyeza hapa
Au
Andika barua  kwa: webmaster@islamtanzania.org
 
Home Links Islam Tanzania Matoleo yaliyopita