AN-NUUR
Na.157 Rabi' Awal 1419, Julai 10 - 16, 1998
 
Home Links Islam Tanzania Matoleo yaliyopita
 
Arusha wasema 

Hongera Mhe. KK kwa kuwa mfano mwema 

Na Hussein M. Arusha 

Pongezi kwa Mhe. Kitwana Kondo zimetolewa na wananchi mbalimbali wa mkoani Arusha kufuatia nasaha zake alizozitoa kwa serikali katika kikao cha Bunge la Bajeti ya Serikali kinachoendelea sasa hivi mjini Dodoma. Mhe. Mbunge wa Kigamboni aliituhumu serikali katika utendaji wake pale inapotoa upendeleo miongoni mwa wananchi. 

Akitoa mfano wa upendeleo, Mhe. Kondo alisema kwamba, "Mhe. Waziri Mkuu aliposhughulikia tatizo la wananchi wa Arumeru waliokataa kulipa kodi, alikwenda na lugha ya kuwabembeleza akitoa ahadi kwamba. Serikali haitakuwa tayari kupambana nao; japo walifanya ghasia; kuchoma nyumba ya Mwenyekiti wao na kuharibu mali. 

Lakini kwa suala la Mwembechai mhe. Kondo anasema Waziri Mkuu alitangaza vita dhidi ya Waislamu na kuahidi kwamba hapatakuwa na huruma bali wataadhibiwa vikali". 

Katika kutoa pongezi zake kwa mhe. Kondo, mzee Joachim Mollel alisema kwamba, "Mhe. Kitwana Kondo ametoa changamoto ya dhati kwa viongozi wengineo wanaoshindwa kusema kweli japokuwa wanaiona kwa kuhofia mambo mbalimbali kama, kunyang’anywa madaraka; kuambiwa wana udini, ukabila, n.k. Linalotakiwa kwa viongozi wetu ni kuongea kweli kwa kutumia hoja zenye nguvu na kwa lengo la kutengeneza na kuelimisha na wala si kutumia jazba, uzuishi, hila aya uchochezi",alingeza mzee Mollel. 

Naye Mzee Hashim Issa alisema kuwa kiongozi maana yake ni kufanyaUadilifu. Na Uadilifu unamaana pana sana ikiwa ni pamoja na kutoa hukumu bila upendeleo; kutoa haki sawa bila kuongozwa na hisia zozote za kubagua". 

Kijana Mustafa Omari alisema kuwa, "Wabunge na viongozi wetu wasisahau kuwa walikula kiapo cha kulitumikia taifa letu kwa uaminifu. Kutumikia kwa uaminifu ni pamoja na kutobagua au kutopendelea baadhi ya wananchi. Hisia zozote katika kuhukumu au utendaji zinazoelekezwa dhidi ya Ukristo ama dhidi ya Uislamu penginehata dhidi ya imani binafsi ya mtendaji au hakimu ni kinyume kabisa nauadilifu au maadili ya uongozi kwa sababu zinalenga kuwafurahisha wakuu wachache ama tabaka fulani katika jamii. 

Hivyo waliopewa dhamana wasisahau kiapo walichokula kwa kuwa wataulizwa na Mwenyezi Mungu kama walitekeleza waliyowaahidi wananchi". Alikumbusha Musatafa. "Ni vema Rais wetu akawa makini na wale viongozi wanaonekana kuhatarisha amani na usalama wa nchi yetu katika utendaji wao", alimalizia Mustafa. 

Naye Muhidin Mwalimu alisema, "Ni wengi wanaohitaji sana madaraka kwa kuwa mamlaka yake ni matamu. Lakini wanapopata wanasahau kaisa sharti lake kuu ambalo ni "Uadilifu’. Hivyo, viongozi wetu wasisahau kuwa huo ni mtihani waliopewa na Mwenyezi Mungu. Na alipowateua amewaacha wengine wenye uwezo pengine zaidi yao." 

Akizungumzia suala hili Mzee Abasi Haji wa Ngara Mtoni alihoji, "Ni vipi katika zama hizi za uwazi na ukweli vyombo vingi vya habari havikutoa kipaumbele katika hoja hii ya Mhe. Kondo kwa kuwa inalenga kulitengeneza taifa letu? "Hii inamaana moja tu, kuwa vyombo vyetu vingi vya habari vinatilia umuhimu mkubwa zaidi matakwa ya watu binafsi wachache na umuhimu kidogo kwa baadhi ya wananchi au maslahi ya aifa letu", alimaliza Mzee Abas. 
 

Juu 
 

YALIYOMO
 
TAHARIRI 

Maoni yetu: Prof. Juma Kapuya, vipi Muislamu usijue agenda za Waislamu? 

Hatimaye Mzee Katambo, Chata waachiwa
Na Mwandishi wetu

Polisi Newala wajenga Msikiti 

Sheikh Bafadhil aitaka Bakwata iwe mtetezi wa Waislamu
Na mwandishi wetu

Makala: Uinjilisti wa Mbuni haufai
Na Rajabu Mbambwa, Kigoma

Mussa Katambo: Mzee aliyewekwa rumande kwa kuandaa mihadhara

Ukweli usiachwe 

Makala: Elimu ya ngono yapenyezwa tena Zanzibar 
Na Saidi Mzee 

Arusha wasema: Hongera Mhe. KK kwa kuwa mfano mwema 
Na Hussein M.,  Arusha 

Wanawake Songea kuandaa maonesho 
Na. Jumah Mbwana, Songea 

Kesi ya mgogoro wa Ardhi
Na. Mustafa Adam 

AN-NUUR marufuku gerezani? 
Na Mwandishi Wetu 

Waislamu Karagwe wadai kusalishwa na imamu asiyejua kutawadha 
Na. Abu Abdallah 

Ofisi mpya za Rabita 
Na Mwandishi Wetu

Barua za wasomaji

Habari za Madrasa

Masomo

 
 Kutoa maoni yako kuhusu ukarasa huu:
Bonyeza hapa
Au
Andika barua  kwa: webmaster@islamtanzania.org
 
Home Links Islam Tanzania Matoleo yaliyopita