|
|
| Waislamu
Tunduma waswali ndani ya kilabu cha ulanzi
BAADHI ya waumini wa Msikiti wa Ijumaa Tunduma wameamua kuhamishia darsa lao amoja na kuswali ndani ya jengo lililokuwa baa maarufu mjini hapa. Hatua hiyo imekuja baada ya kutokea kutokuelewana baina ya makundi mawili pinzani. Waliohama na kukodi jengo lililokuwa baa mashuhuri kwa jina la ‘Kilimanjaro Bar’ ni waumini wote waliokuwa wanahudhuria darsa iliyokuwa ikiendeshwa Msikitini hapo na Ustadh Nassoro Abdallah. Imedaiwa kwamba Sheikh huyo wa Wilaya wa Bakwata Sheikh Abdallah Mwapyate hakubaliani na utaratibu wa kutumia fedha za Msikti kuendeshea madrasa ikiwa ni pamoja na kulipa mishahara ya waalimu. Kutokana na mgongano uliopo kati ya Kamati ya Msikiti na Sheikh wa Wilaya, Kamati iliamua kujiuzulu na wakati huo huo Sheikh akateua Imam mwingine kinyume na yule aliyewekwa na waumini. Hali hiyo ilizaa jamaa mbili ndani ya Msikiti ambapo Sheikh alichukua hatua ya kulisimamisha darsa hadi baada ya Ramadhani. Waumini waliohama Msikiti wamedai kwamba wamekuwa wakipachikwa majina kama "wenye itikadi kali" kwa lengo la kuwafitini kwa serikali na jamii inayowazunguka. Wamesema kwamba ili kuepusha shari wataswalia kwenye jengo hilo la baa kwa muda huku wakifanya juhudi za kujenga Msikiti wao. Kwa upande wa Sheikh wa Wilaya imeelezwa kwamba yeye hakutaka fedha za Msikiti zitumike kuendesha madrasa bali wazazi wachange. Aidha, imeelezwa kwamba Sheikh ana mpango wa kuleta waalimu wengine kutoka Tanga kwa madai kwamba aliyeko ambaye ni Ustadh Nassoro hajulikani ametokea wapi na amesomeshwa na nani. Madrasa hiyo yenye wanafunzi 35 watu wazima wanaume, 42 wanawake na watoto 100 ilifungwa hivi karibuni na Sheikh wa Bakwata wa Wilaya kwa visingizio mbalimbali. |
YALIYOMO
Tahariri Hakuna Idd kwa wanafunzi Waislamu mwaka huu Baada ya wanafunzi Wakristo kusherehekea Krismasi: Wanafunzi Waislamu kuikosa Id el Fitr Hoi hoi zatawala ziara ya Mwinyi Mwanza Waislamu Tunduma waswali ndani ya kilabu cha ulanzi MARADHI YA KISAIKOLOJIA: FROTTEURISM Barabara za Tabora zimepitwa na wakati Jicho la
Uzalendo: Nihiari yetu kuendelea kujidanganya!
Kuanza na kwisha mwezi wa Ramadhani Taarifa ya Kamati juu ya yaliyotokea Mwembechai Maazimio ya kongamano la wanawake wa Kiislamu Waislamu kijijini Kidunda Moro wahitaji mwalimu Waislamu Mtwara wadai jengo la Wakfu kwa CCM Wakati Makanisa yakimeremeta: Msikiti wageuka gofu Sanya Juu Sheikh Khalifa Suleiman afariki dunia Sheikh wa wilaya ya Lushoto afariki Ijue Madrasat Riyaadhwa ya mjini Dodoma Mwinyi apongeza juhudi za kulea yatima Mwanza Tuhuma za kupindua uongozi wa Bakwata: Sheikh Hamim Boza akanusha kuhusika Kuongezeka kwa ajali za barabarani Njia ya
uzimani ni nyembamba, waionao ni wachache - 4
Saggaf awataka watoto wahifadhi Qur'an Waislamu watakiwa kujitolea kupigania dini yao Kesi nyingine Mwembechai yaahirishwa Sayansi
na Teknolojia
Chakula
na lishe
|