|
|
Maiti
ya Muislamu yasusiwa
Habari zilizopatikana kutoka kijiji hicho zimeeleza kuwa kususiwa kwa maiti hiyo kunatokana na marehemu kutojishughulisha na ibada yoyote katika uhai wake zaidi ya vitendo vya maasi. Imeelezwa kuwa marehemu huyo aliyetajwa kwa jina moja tu la Saidi alikuwa Muislamu aliyeachana na sala. Alifia katika hospitali teule iliyopo wilayani Muheza baada ya kuugua kwa muda mfupi na baada ya taarifa za kifo chake kusambazwa, Sheikh wa kijiji hicho ambaye pia ni Sheikh wa tarafa alidai kuwa hatamzika wala kumsalia kwa sababu marehemu alikuwa tarkuswalat (haswali). Kutokana na Waislamu wengi wa kijiji hicho kuweka msimamo wa kutomswalia wala kumzika mtu aliyekuwa haswali, maiti ya marehemu ilitekelekezwa hospitali kwa siku mbili na siku ya tatu yake inadaiwa ni vijana wa maskani waliokwenda kuichukua hospitali kwa kutumia baiskeli ambapo ilifungwa kwenye kiti cha nyuma na kusafirishwa hadi kijijini hapo. Walioshuhudia tukio hilo walieleza kuwa vijana hao ndio waliomuosha kijana mwenzao wakamvisha sanda na kwenda kumzika wanavyoweza bila kumsalia wala kumuombea dua yoyote ile. Mkazi mmoja wa kijiji hicho aliyejitambulisha kwa jina la Bakari Ramadhani alipohojiwa na mwandishi wa habari hizi kuhusiana na tukio hilo alisema Waislamu wa kijiji hicho wameweka msimamo wa kutomsalia wala kumzika Muislamu yeyote anayejishughulisha na vitendo vya shirk au kukataa kuswali. Alisema marehemu Saidi alikuwa tarkuswalaat na aliingia siku moja tu
kwenye Msikiti baada ya kuchukuliwa na vijana wa Answar Sunna ambao walikuwa
wakiendesha Da’awa kijijini hapo.
Mwinyi apongeza juhudi za kulea yatima Mwanza RAIS mstaafu Ali Hassan Mwinyi amewakumbusha Waislamu kwamba kutunza mayatima sio hiari bali ni amri kama zilivyo amri nyingine ndani ya maagizo ya Allah (s.w.). Akiongea na Waislamu waliohudhuria katika kituo cha mayatima cha Ilemela, Mwanza kinachoendeshwa na taasisi ya Ilemela Yatima Foundation alisema kuwa Mwenyezi Mungu ameahidi ujira na faida mbalimbali kwa anayejishughulisha na ulezi wa mayatima. Kabla ya kuzungumza hayo ndani ya jengo linalokusudiwa litakapokamilika kuwa mahali pa kulia chakula, mikutano, semina na shughuli mbalimbali zinazojumuisha watu wengi, alipata fursa ya kusali sala ya alasiri ndani ya Msikiti uliojengwa na Africa Muslims Agency na alitembezwa maeneo mbalimbali ili kujionea mazingira ya kituo hicho. Kabla ya kumkaribisha kuongea na Waislamu pamoja na yamatima wenyewe, watoto hao chini ya mwalimu wao ambaye ndiye mkuu wa kituo hicho Ustadh Nasib Issa, walionyesha mambo mbalimbali wafundishwayo hapo kituoni. Waliimba nyimbo zilizokuwa na ujumbe kwa kuwahimiza watu kuwajali watoto wenye matatizo mbalimbali, hasa mafunzo ya tabia njema kwa ujumla, waliigiza kwa lugha ya Kiarabu, Kiswahili na Kiingereza. Baadaye Mwenyekiti wa Bodi wa kituo hicho Sheikh Jabir Yusufu Katura alisoma historia ya kituo na kutoa shukrani za pekee kwa wafadhili mbalimbali waliojitokeza mara moja baada ya mfadhili mwanzilishi marehemu Bashiri Hussein Sherally kufariki kwa ajali ya ndege huko Kenya mwishoni mwa mwaka juzi. Mwenyekiti huyo alisema kuwa kituo kilianza Desemba 26, 1997 kikiwa na watoto 16, hivi sasa wako 26, alisema kituo kinatoa huduma za kulea, chakula, malazi, mavazi, matitabu ambapo kwa sasa hivi mtoto mmoja anagharimu shilingi 25,000 kwa mwezi. Sheikh Jabir aliomba wafadhili mbalimbali wajitokeze kwani kituo kinahitaji zaidi ya shilingi laki tisa kwa mwezi. Akiongea, Alhaj Mwinyi alisema kuwa mwanzo tayari umepatikana, sasa ni juu ya Waislamu wote kwa ujumla kuuendeleza mwanzo. Aliahidi yeye kupitia kwa marafiki zake kuchangia chochote watakachopata ili nao wapate fadhila za sadakat-jaria (sadaka yenye kudumu). Awali aliombwa kuwa mlezi wa kituo na alikubali bila ya pingamizi kwa kusema kuwa hilo ni jambo la kheri na hakuna awezaye kupinga. Wakati huo huo, Rais Mstaafu Ali Hassan Mwinyi amewataka Waislamu kuchukua hadhari kubwa kutokana na uharibifu mkubwa wa kimaadili unaofanywa na nchi za Ulaya. Amesema nchi hizo kupitia mtandao wa vyombo vya habari; wamekuwa wachafuzi wa maadili na mila za Kiislamu hivyo hapana budi kwa Waislamu kuwa na taratibu madhubuti za kukabiliana na uharibifu huo. Nasaha hizi Alhaj Mwinyi alizotoa wakati akiwa mgeni rasmi katika mahafali
ya pili ya shule ya Thaqafa kitengo cha Dini.
|
YALIYOMO
Tahariri Hakuna Idd kwa wanafunzi Waislamu mwaka huu Baada ya wanafunzi Wakristo kusherehekea Krismasi: Wanafunzi Waislamu kuikosa Id el Fitr Hoi hoi zatawala ziara ya Mwinyi Mwanza Waislamu Tunduma waswali ndani ya kilabu cha ulanzi MARADHI YA KISAIKOLOJIA: FROTTEURISM Barabara za Tabora zimepitwa na wakati Jicho la
Uzalendo: Nihiari yetu kuendelea kujidanganya!
Kuanza na kwisha mwezi wa Ramadhani Taarifa ya Kamati juu ya yaliyotokea Mwembechai Maazimio ya kongamano la wanawake wa Kiislamu Waislamu kijijini Kidunda Moro wahitaji mwalimu Waislamu Mtwara wadai jengo la Wakfu kwa CCM Wakati Makanisa yakimeremeta: Msikiti wageuka gofu Sanya Juu Sheikh Khalifa Suleiman afariki dunia Sheikh wa wilaya ya Lushoto afariki Ijue Madrasat Riyaadhwa ya mjini Dodoma Mwinyi apongeza juhudi za kulea yatima Mwanza Tuhuma za kupindua uongozi wa Bakwata: Sheikh Hamim Boza akanusha kuhusika Kuongezeka kwa ajali za barabarani Njia ya
uzimani ni nyembamba, waionao ni wachache - 4
Saggaf awataka watoto wahifadhi Qur'an Waislamu watakiwa kujitolea kupigania dini yao Kesi nyingine Mwembechai yaahirishwa Sayansi
na Teknolojia
Chakula
na lishe
|