AN-NUUR 
Na.181 Ramadhan 1419, Desemba 25 - 31, 1998 
 
Home Links Islam Tanzania Matoleo yaliyopita
 
Baada ya wanafunzi Wakristo kusherehekea Krismasi:
Wanafunzi Waislamu
kuikosa Id el Fitr
 
  • Mitihani ya kidato cha nne kuanza Jan. 13 
  • Jiji nalo laandaa tamasha ndani ya Ramadhani
WAKATI wanafunzi Wakristo wakisherehekea sikukuu ya Noeli na Mwaka Mpya pamja na familia zao, ratiba ya mitihani ya kidato cha nne iliyotangazwa na baraza la mitihani imezua hisia na wasiwasi mkubwa miongoni mwa wanafunzi Waislamu ambapo inaonyesha itaanza ndani ya mfungo wa Ramadhani na huenda ikahusisha na sikukuu ya Id el Fitri. 

Wasiwasi huo umetokana na ukweli kwamba kwa mujibu wa kanuni za Baraza hilo ratiba ya mitihani ikishapangwa haiwezi kubadilishwa kwa sababu yoyote ile. 

Baadhi ya wananchi mbalimbali walioongea na gazeti hili wameelezea masikitiko yao kuhusu uamuzi wa Baraza kupanga mitihani hiyo ndani ya mwezi mtukufu wa Ramadhani na katika sikukuu za Idd el Fitri. 

Wamesema kuwa ratiba hiyo inathibitisha kutokutambuliwa kwa imani ya Kiislamu katika upangaji na uendeshaji wa masuala mbalimbali ya kinchi. 

Bwana Maulid Hassan wa Manzese akizungumzia suala hili alisema upangaji huo wa ratiba umezingatia Krismasi na Boxing Day yake, umezingatia Mwaka Mpya na pia umezingatia sikukuu ya Mapinduzi lakini haukuweza kukumbuka mfungo wa Ramadhan na sikukuu ya Eid. 

Naye Bwana Masoud wa Ilala Boma yeye alitilia mashaka ratiba hiyo kuwa huenda imepangwa hivyo ili kuwakomoa Waislamu kwani shughuli nyingi zote za kitaifa zimezingatiwa. 

"Ratiba imeanza siku ya Jumatano badala ya Jumatatu ili wanafunzi wasifanye mitihani wakati wa sikukuu ya Mapinduzi ya Zanzibar", alisema kwa hisia Bwana huyo. 

Wengi wametuhumu ratiba ya mtihani kuwa ni ya "kibaguzi" isiyozingatia walipa kodi Waislamu wa nchi hii. 

Mitihani ya kidato cha nne iliyofutwa Novemba 1998 sasa itafanyika kuanzia Janauri 13 hadi Janauri 27 mwakani kwa mujibu wa ratiba iliyotolewa na baraza la mitihani hivi karibuni. 

Jumatatu imetangazwa kuwa ni siku ya mapumziko ili kufidia siku ya Boxing Day iliyoangukia Jumamosi. 

Kutangazwa kwa siku ya hiyo ya Jumatatu kuwa ni ya mapumziko kumekuja wakati vyombo vya habari huko nyuma viliwahi kuripoti kuwa utaratibu wa kufidia sikukuu zinazoangukia Jumamosi na Jumapili ulifutwa na Bunge. 

Wakati huo huo, imefahamika kwamba linaandaliwa Tamasha kubwa la Jiji kuanzia Januari 16 ambalo litadumu kwa wiki moja. 

Tamasha hilo ambalo litafanyika katika viwanja vya Mnazi Mmoja limekuwa likilalamikiwa na baadhi ya wakereketwa wa CCM kwa kutozingatia hisia za waliofunga. 

Japo ratiba maalum ya Tamasha hilo haijajulikana lakini wengi wanaojua kuwepo kwa tamasha hilo wamesema kwamba ngoma na unywaji ni vitu ambavyo havitakosekana. 

Kupangwa kwa Tamasha hilo ndani ya Ramadhani bila ya kujali kwamba miongoni mwa washiriki watakuwa ni Waislamu ambao watakuwa wamefunga kumeelezwa kwamba kumetokana na Tume ya Jiji kujaa Wakurugenzi wa dini moja. 

Hali hiyo imeelezwa kwamba inawafanya wasiwe makini wala kuzingatia uwepo wa Waislamu na hisia zao kutokana na imani yao. 

Gazeti hili liliwasiliana na Katibu wa Tume ya Jiji ambaye alithibitisha kuwepo kwa tamasha hilo. 
 

Juu 
 

YALIYOMO 
 
 
Tahariri 
Hakuna Idd kwa wanafunzi Waislamu mwaka huu 

Baada ya wanafunzi Wakristo kusherehekea Krismasi: Wanafunzi Waislamu kuikosa  Id el Fitr 

Hoi hoi zatawala ziara ya Mwinyi Mwanza 

Waislamu Tunduma waswali ndani ya kilabu cha ulanzi  

MARADHI YA KISAIKOLOJIA: FROTTEURISM 

Barabara za Tabora zimepitwa na wakati 

Jicho la Uzalendo: Nihiari yetu kuendelea kujidanganya! 
Na Sompo wa Kahambwe 

Kuanza na kwisha mwezi wa Ramadhani 

Taarifa ya Kamati  juu ya yaliyotokea Mwembechai 

Hotuba ya Mwenyekiti wa Wanawake wa Kiislamu katika Kongamano lililofanyika Masjid Nnuur Sinza  19/12/1998 

Maazimio ya kongamano la wanawake wa Kiislamu 

Waislamu kijijini Kidunda Moro wahitaji mwalimu 

Waislamu Mtwara wadai jengo la Wakfu kwa CCM 

Wakati Makanisa yakimeremeta: Msikiti wageuka gofu Sanya Juu 

Sheikh Khalifa Suleiman afariki dunia 

Sheikh wa wilaya ya Lushoto afariki 

Ijue Madrasat Riyaadhwa ya mjini Dodoma 

Somo la Zaka 

Maiti ya Muislamu yasusiwa 

Mwinyi apongeza juhudi za kulea yatima Mwanza 

Tuhuma za kupindua uongozi wa Bakwata: Sheikh Hamim Boza akanusha kuhusika 

Kuongezeka kwa ajali za barabarani 

Njia ya uzimani ni nyembamba,  waionao ni wachache - 4 
Na Yasin Valerian Massawe 

Matajiri wahimizwa kutoa zaka 

Saggaf awataka watoto wahifadhi Qur'an 

Waislamu watakiwa kujitolea kupigania dini yao 

Kesi  nyingine Mwembechai yaahirishwa  

Sayansi na Teknolojia  
[Kuirekebisha Modem Yako]  

Masomo ya Dini ya Kiislamu  

Barua za Wasomaji  

Mashairi  

Chakula na lishe  
[Saumu na lishe ya mama mjamzito] 
 

   Kutoa maoni yako kuhusu ukarasa huu: Bonyeza hapa
Au
Andika barua  kwa: webmaster@islamtanzania.org
 
Home Links Islam Tanzania Matoleo yaliyopita