|
|
|
Kuna kanuni za jumla na kanuni maalum katika suala zito la kumkumbuka Mwenyezi Mungu. Kanuni hizo zinatajwa na Aya zifuatazo. Mkumbukeni Mwenyezi Mungu msimamapo, mkaapo na (mlalapo) ubavu. Na mkumbukeni Mwenyezi Mungu kwa wingi ili mpate kufaulu. (4:103) Katika kuumbwa mbingu na ardhi na mfuatano wa usiku na mchana zipo hoja (Ayat) kwa wenye akili. Ambao humkumbuka Mwenyezi Mungu wakiwa wima na wakikaa na wakilala. Na hufikiria umbo la mbingu na ardhi (kwa makini) husema: "Mola wetu hukuviumba hivi bure." Kuna Aya nyingi zaidi ya hizi ambazo zimeamriwa kuendelea kumkumbuka Mungu siku zote katika kila hali kwa sababu kumkumbuka Mungu ndiko kunakoyaweka matendo ya mtu katika njia iliyosahihi. Wakati wowote mtu awapo hamjali au hamkumbuki Mungu, haja za kimwili na matamanio yake humtawala, matokeo yake ni kwenda kinyume na kukiuka mipaka ya Njia iliyonyooka katika maisha yake. Kanuni Maalumu ya kumkumbuka Allah huonekana katika Swala ambayo ni mara tano kwa siku. Hii haina maana kuwa baada ya swala mtu yuko huru. La hasha wakati wote wa saa ishirini na nne unatakiwa umkumbuke Mwenyezi Mungu. Na hivi ndivyo ilivyo kwenye kutoa katika Njia ya Allah; kuna hukumu ya jumla na hukumu Maalumu. Kanuni za jumla kuhusu kutumia katika Njia ya Allah Upande mmoja inaamriwa: Jizuie na ubakhili na uchoyo kwa kuwa ni chanzo na ni mambo mabaya katika jamii. Katika vile ambavyo Mwenyezi Mungu ambae nyakati zote anawashushia viumbe wake ameamuru kutumia chochote awezacho mja katika njia yake. Weka akiba kiasi utachoweza kutokana na mahitaji yako na kutokana na akiba yako tosheleza mahitaji ya watumishi wengine wa Mungu ambao ni wahitaji. Kamwe usiache kujitolea maisha yako na mali yako katika kulitukuza neno la Mwenyezi Mungu na kuitumikia Dini Yake tu. Kama unampenda Mwenyezi Mungu basi toa pendo la mali kwa Mwenyezi Mungu. Hii ndio hukumu ya jumla ya kutoa katika njia ya Allah kama Aya zisemavyo: "Hamtaweza kuufikia wema khasa mpaka mtoe katika vile mnavyovipenda; na chochote mnachokitoa, basi hakika Mwenyezi Mungu anakijua." (3:92). "Na toeni katika njia ya Mwenyezi Mungu, wala msijitie kwa mikono yenu katika maangamizo. Na fanyeni wema, hakika Mwenyezi Mungu huwapenda wafanyao wema". (2:195). "Shetani anakuogopesheni ufukara na anakuamrisheni ubakhili; na Mwenyezi
Mungu anakuahidini msamaha, utokao kwake na ihsani (kubwa pindi mkitoa);
na Mwenyezi Mungu ni Mwenye wasaa mkubwa na Mwenye kujua." (2:268).
|
Maoni yetu: Wananchi kataeni kupotoshwa SUALA LA MWEMBECHAI: Wabunge
wataka kujua nani aliamrisha kuua
Katiba ya nchi yapuuzwa: Waislamu wapigwa marufuku kuhubiri Mtihani darasa la saba 1998: Manispaa
Moro yaagiza ipewe majina ya wanafunzi Wakatoliki
“Wushu”ya Waislamu wa China
na jinsi ilivyowasaidia kupambana na dhulma dhidi yao
Yesu wa kwenye Mathayo siyo Yesu wa
kwenye Luka
Ni nani hawa Waislamu wa Siasa Kali
?
Waislamu tuondokane na unyonge
Waislamu wana mwelekeo wao
Ni mwaka gani Yesu alianza kuitwa
Mungu
Wanawake wameamua kuwa wazi
kweli kweli
Kimya kingi kina mshindo mkuu:
Vipi Mhe. Rais wale walioua?
Mtazamo wa madhalimu wa Tanzania
kwa Waislamu
Waislamu mkoa wa Morogoro
wampinga Yahya
Polisi wachafua mazingira
ya msikiti wa Mwembechai
Wanawake wa Kiislamu Ubungo
darajani wamuunga mkono Sheikh Bafadhil
Mafundisho ya Qur'an: Kanuni za kumkumbuka Allah na kutumia katika njia yake Chakula na lishe: Lishe ya
mtoto aliyekuwa mgonjwa
|