|
|
WASI WASI mkubwa umeanza kuwaingia wazazi Waislamu wa mjini hapa kufuatia kupatikana kwa barua kutoka ofisi ya Elimu Manispaa inayowaagiza walimu wakuu wote wa shule za msingi kupeleka majina ya wanafunzi Wakatoliki wa darasa la saba wa mwaka huu. Mapema juzi baadhi ya Waislamu walionekana kupigwa na bumbuwazi baada ya kupata taarifa hizo na baadhi yao wakiwa wameiona nakala ya barua hiyo. Gazeti hili lilifanikiwa kuipata nakala ya barua hiyo ambayo imetiwa saini na mtu aitwaye E.P. Mpessa kwa niaba ya Afisa Eimu wa Manispaa ya Morogoro. Katika barua hiyo yenye kumbukumbu namba E.10/MMC-1/183 iliyoandikwa Juni 9 mwaka huu, inawataka walimu wakuu wote wa shule za msingi Manispaa ya Morogoro kutuma majina ya wanafunzi Wakatoliki darasa la saba hadi kufikia Juni 12, 1998. Barua hiyo fupi haikufafanua kiundani majina hayo ni ya nini jambo ambalo limewafanya Waislamu wa hapa kuanza kuwatilia mashaka walimu wakuu wa shule hizo kuwa wanafahamu suala hilo kiundani zaidi ndio maana Mwandishi hakulazimika kufafanua. Wakizungumza na gazeti hili baadhi ya Waislamu wamedai kuwa vitu vya namna hiyo ndivyo vinavyowafanya waumini wa dini ya Kiislamu kuituhumu serikali kuwa inawapendelea Wakristo katika nyanja zote na hususan katika elimu. "Hali hii na mikakati kama hii viongozi wetu wa Kiislamu walio serikalini hawajui na wakipewa taarifa kama hii huwa hawaifanyii kazi badala yake wanawarushia Waislamu kashfa kwa kuwaambia hawana dira", alisema kwa uchungu muumini mmoja wa eneo la Kingo Bwana Ally Seifu. Naye Bw. Athman Salim wa Mafiga amesema "hata watoto wetu wasipochaguliwa kujiunga na shule za sekondari za serikali mwakani tutaamini kuwa imetokana na njama hizi." Kufuatia kupatikana waraka huo baadhi ya waumini wametishia kulipeleka suala hili mbele ya sheria (mahakamani) kwa madai kuwa linahatarisha hali ya baadaye ya vijana wao kimasomo. Aidha baadhi ya waumini hao wa Kiislamu wameiomba serikali kutopuuzia hali hii na kwamba ufanyike uchunguzi wa kina kwa kuunda tume huru vinginevyo huenda kukatokea mgawanyiko miongoni mwa raia wake. Mitihani ya Darasa la Saba inatarajiwa kufanyika nchi nzima mwezi Septemba
mwaka huu.
|
TAHARIRI Maoni yetu: Wananchi kataeni kupotoshwa SUALA LA MWEMBECHAI: Wabunge
wataka kujua nani aliamrisha kuua
Katiba ya nchi yapuuzwa: Waislamu wapigwa marufuku kuhubiri Mtihani darasa la saba 1998: Manispaa
Moro yaagiza ipewe majina ya wanafunzi Wakatoliki
“Wushu”ya Waislamu wa China
na jinsi ilivyowasaidia kupambana na dhulma dhidi yao
Yesu wa kwenye Mathayo siyo Yesu wa
kwenye Luka
Ni nani hawa Waislamu wa Siasa Kali
?
Waislamu tuondokane na unyonge
Waislamu wana mwelekeo wao
Ni mwaka gani Yesu alianza kuitwa
Mungu
Wanawake wameamua kuwa wazi
kweli kweli
Kimya kingi kina mshindo mkuu:
Vipi Mhe. Rais wale walioua?
Mtazamo wa madhalimu wa Tanzania
kwa Waislamu
Waislamu mkoa wa Morogoro
wampinga Yahya
Polisi wachafua mazingira
ya msikiti wa Mwembechai
Wanawake wa Kiislamu Ubungo
darajani wamuunga mkono Sheikh Bafadhil
Mafundisho ya Qur'an: Kanuni za kumkumbuka Allah na kutumia katika njia yake Chakula na lishe: Lishe ya
mtoto aliyekuwa mgonjwa
|