|
|
|
Na. Masoud Mohammed Barua iliyoandikwa na Ndugu Agustine Mwinuka katika gazeti la Msemakweli toleo Namba 018 la tarehe 5-11, Julai 1998 haiwezi kupita bila kuchangiwa. Mwandishi wa barua hiyo iliyokuwa na kichwa cha habari Nabii Issa na Yesu kweli hawahusiani, amejitahidi kufanya uchambuzi japo siyo yakinifu na kuona kuwa kuna tofauti fulani juu ya sifa za Yesu kama zinavyoelezwa katika Biblia na sifa za Issa kama zinavyoelezwa katika Qur’ani tukufu. Ni kutokana na tofauti hizo ndiyo Ndugu Mwinuka anahitimisha kuwa Yesu wa kwenye Biblia siyo Issa wa kwenye Qur’ani." Pamoja na juhudi zote alizofanya, kwa bahati mbaya sana Ndugu Mwinuka alikosa uhuru wa mawazo na hivyo kuishia katika kutoa hitimisho nusu. Kama angelikuwa huru na mwaminifu kwa kuanza kuichunguza historia ya Yesu ndani ya Biblia yenyewe siyo ajabu kwamba kabla hajagundua kuwa Yesu wa kwenye Biblia siyo Issa wa kwenye Qur’ani, angegundua kwanza kwamba Yesu wa kwenye Mathayo siyo Yesu wa kwenye Luka. Ninasema hivyo kwa sababu ukoo wa Yesu wa kwenye Injili ya Mathayo unaanzia kwa Solomon, Roboam, Abia, Asa, Japhat…. Na kizazi cha 25 akiwa ni Jakobo aliyemzaa Yusufu aliyemzaa Yesu (Taz. Mathayo 1:1-18). Kwa upande mwingine ukoo wa Yesu wa Injili ya Luka ni mwingine kabisa ukiwa na majina tofauti na Yesu wa kwenye Mathayo. Ukoo huu unaanzia kwa Mathani, Mattatha, Menan…. Kizazi cha 40 kikiwa ni Heli aliyemzaa Yusufu aliyemzaa Yesu. (Taz. Lk. 3:23-31). Tofauti kubwa iliyopo kwa Mayesu hawa wawili ni kwamba yule wa kwenye Mathayo anatokana na ukoo tofauti kabisa na yule wa Luka. Ni jina moja tu la Yusufu linalopatikana kwa Mayesu hawa wawili na hata Mayusufu hawa wanaonekana kuwa tofauti. Wakati Yusufu wa kwenye Mathayo alizaliwa na Yakobo, Yusufu wa kwenye Luka alizaliwa na Heli. Hii ilikua ni hoja ya msingi kabisa kumfanya Bwana Mwinuka aamini kuwa Yesu wa kwenye Luka siyo wa kwenye Mathayo, lakinihilo hakuliona. Tofauti nyingine inahusiana na namna hawa Mayesu wawili walivyokufa. Yesu wa kwenye Mathayo neno lake la mwisho kutamka kabla hajakata roho ni Mungu wangu Mungu wangu mbonaumeniacha?" (Taz. Mathayo 27:45) wakatiYesu wa kwenye Luka neno lake la mwisho kutamka kabla ya kufa ni "Roho yangu naiweka mikononi mwako". Taz. (Lk.23:46). Hali kadhalika tukiangalia historia ya kufufuka na Mayesu hawa wawili ni rahisi kugundua kuwa walikuwa watu wawili tofauti. Kaburi la Yesu wa kwenye Mathayo lilitembelewa na wanawake,Mariamu Magdalena na Mariam wa pili siku ya kufufuka na kwamba wanawake hawa wawili walitokewa na malaika mmoja (Taz. Mathayo 28:1-8), kwa upande wa Yesu wa kwenye Luka yeye kaburi lake lilitembelewa na wanawake watatu ambao walitokewa na malaika wawili na siyo mmoja siku ya kufufuka (Tz.LK. 24:1-12) Ni kutokana na maelezo hayo juu ndiyo nimesita kumjibu Ndugu Mwinuka neno kwa neno ili kumpa nafasi aweke wazi zaidi misingi ya hoja yake. Haieleweki kama anataka kuonyesha kuwa kuna tofauti katika maelezo ya historia ya Yesu katika Biblia na katika Quraani na hivyo tuangalie ni ipi historia sahihi ya Yesu? Au anataka kumaanisha kuwa Jesus wa kwenye King James Version ni tofauti na Yesu wa Biblia ya Kiswahili? Na kama hivyo ndivyo la kwanza kufanya ilikuwa ni kutuonyesha ukoo wa Yesu na Issa na mengine yangefatia baadaye. Yote katika yote ningemuomba sana ndugu yangu Mwinuka afafanue juu ya
hayo, na kama atakubaliana\ na maelezo hapo juu kuwa Yesu wa kwenye Mathayo
si yule wa kwenye Luka, kwa mtizamo huo sitakuwa na sababu ya kung’ang’ania
kwamba Yesu wa kwenye Luka ndiyo Isa wa kwenye Quraani. Kwani hata Qur-an
haisemi kuwa Yesu ni Yesu kwa sababu yumo katika Biblia. Zaidi ya hapo
ningependa ndugu huyu afafanue zaidi na hatimaye nipate nafasi ya kumpatia
ushahidi wa kimaadiko (Qurani na Biblia), ushahidi wa kihistoria na ushahidi
kutoka katika matamshi ya mapadri na wachungaji wake toka katika madhehebu
mbalimbali wakishuhudia kuwa Yesu wa kwenye Quraani ndiye Yesu wa kwenye
Biblia.
|
TAHARIRI Maoni yetu: Wananchi kataeni kupotoshwa SUALA LA MWEMBECHAI: Wabunge
wataka kujua nani aliamrisha kuua
Katiba ya nchi yapuuzwa: Waislamu wapigwa marufuku kuhubiri Mtihani darasa la saba 1998: Manispaa
Moro yaagiza ipewe majina ya wanafunzi Wakatoliki
“Wushu”ya Waislamu wa China
na jinsi ilivyowasaidia kupambana na dhulma dhidi yao
Yesu wa kwenye Mathayo siyo Yesu wa
kwenye Luka
Ni nani hawa Waislamu wa Siasa Kali
?
Waislamu tuondokane na unyonge
Waislamu wana mwelekeo wao
Ni mwaka gani Yesu alianza kuitwa
Mungu
Wanawake wameamua kuwa wazi
kweli kweli
Kimya kingi kina mshindo mkuu:
Vipi Mhe. Rais wale walioua?
Mtazamo wa madhalimu wa Tanzania
kwa Waislamu
Waislamu mkoa wa Morogoro
wampinga Yahya
Polisi wachafua mazingira
ya msikiti wa Mwembechai
Wanawake wa Kiislamu Ubungo
darajani wamuunga mkono Sheikh Bafadhil
Mafundisho ya Qur'an: Kanuni za kumkumbuka Allah na kutumia katika njia yake Chakula na lishe: Lishe ya
mtoto aliyekuwa mgonjwa
|