AN-NUUR
Na.158 Rabi' Awal 1419, Julai 17 - 23, 1998
 
Home Links Islam Tanzania Matoleo yaliyopita
 
.Katiba ya nchi yapuuzwa: 
 
  • Waislamu wapigwa marufuku kuhubiri 
  • Mahubiri ya Wakristo yashamiri Mwanza
  • Walokole Mtwara wasema Yesu ni Mungu Mkuu
  • Songea Waislamu wanne watupwa rumande
Na Muhidini Mustafa 

HUKU serikali ikiendelea na madai yake kwamba haina chuki na Waislamu na kwamba haijazuia mahubiri ya dini, mjini Mwanza Kamanda wa Polisi Wilaya amepiga marufuku mahubiri hayo kinyume na katiba ya nchi. 

Kwa mujibu wa barua ya kamanda huyo kwa tawi la Almallid mjini Mwanza yenye kumbukumbu Na. MZA/B.3/24/Vol.1/235 ya Juni 3, 1998, mahubiri ya dini yamezuiliwa mjini humo kwa muda usiojulikana. 

Haikuelezwa sababu hasa za kuzuia mahubiri hayo, lakini taarifa zinafahamisha kwamba huenda huo ukawa ni mkakati wa jeshi hilo kufuta mihadhara inayodaiwa kuwa ni ya kashfa. Mihadhara hiyo ni pamoja na ile ya Waislamu ambayo hueleza kuwa Yesu si Mungu wala si Mtoto wa Mungu. 

Hata hivyo wakati mihadhara ya Waislamu ikipigwa marufuku mkoani humo, kuna taarifa kwamba Wakristo wameendelea kuhubiri kwa vishindo kwamba Yesu ni Mungu Mkuu na kwamba asiyekubali imani hiyo amepotea. 

Mahubiri hayo ya Wakristo yamekuwa yakifanyika katika viwanja vya furahisha chini ya Mchungaji aliyefahamika kwa jina la moja la Mkova. 

Mahubiri mengine yamekuwa yakiendelea katika viwanja vya Kitangiri, Kilimahewa, Igogo na sehemu nyingine. 

Wakati huo huo, Mwandishi Idi Katimba anaripoti kutoka mjini Mtwara kwamba Wakristo wa dhehebu la Walokole wamekuwa wakiendesha mahubiri yanayodai Yesu sio Mwislamu bali ni Mungu Mkuu na kwamba wasioikubali imani hiyo wamepotea na watakwenda Jahannam. 

Miongoni mwa waliotajwa kwenda Jahanam ni pamoja na Waislamu na Wakatoliki. 

Taarifa kutoka mjini humo zinaeleza kuwa wakazi wa mji huo ambao sehemu kubwa ni Waislamu, wamepigwa na butwaa kufuatia mahubiri hayo ambayo yamekuwa yakiendelea kwa masiku kadhaa. 

Halikadhalika mjini Songea nako hali si shwari kwa upande wa Waislamu, huko imeripotiwa kwamba mwishoni mwa wiki iliyopita Waislamu wanne walipata mkong’oto kutoka kwa polisi wa mjini humo kwa madai ya kuuza kanda zinazodaiwa kukashifu dini nyingine. 

Waislamu hao wametajwa kuwa ni Bwana Mohamed Kawanga, Abdallah Hussein, Ali Kipande na Mzee Kalungo. 

Gazeti hili liliwasiliana na kamanda wa polisi mkoani humo siku ya Jumatano kuthibitisha taarifa hizo, hata hivyo kamanda huyo alisema hana taarifa kamili na aliahidi kutoa maelezo siku iliyofuata. 

Hadi gazeti hili linakwenda mtamboni jitihada za kuwasiliana tena kamanda huyo hazikufanikiwa. 

 
Juu 
 

YALIYOMO
 
TAHARIRI  

Maoni yetu: Wananchi kataeni kupotoshwa 

SUALA LA MWEMBECHAI: Wabunge wataka kujua nani aliamrisha kuua 
Na Mwandishi wetu  

Katiba ya nchi yapuuzwa: Waislamu wapigwa marufuku kuhubiri  

Mtihani darasa la saba 1998: Manispaa Moro yaagiza ipewe majina ya wanafunzi Wakatoliki 
Na Rajab Rajab, Morogoro 

 “Wushu”ya Waislamu wa China na jinsi ilivyowasaidia kupambana na dhulma dhidi yao 
Na MUSSA ALLY  

Yesu wa kwenye Mathayo siyo Yesu wa kwenye Luka 
Na. Masoud Mohammed 

Ni nani hawa Waislamu wa Siasa Kali ? 
Na USTADH  A.S. FUNDI  

Waislamu tuondokane na unyonge 
Na Abubakar Marwilo 

Maisha ya ndoa kwa Mwislamu 

Waislamu wana mwelekeo wao 
Na Sheikh Pandukizi Dilunga 

Ni mwaka gani Yesu alianza kuitwa Mungu 
Na MCHUNGAJI A.T. MANONI  

Wanawake wameamua kuwa wazi kweli kweli 
Na Bi. Fatma Musa 

Kimya kingi kina mshindo mkuu: Vipi Mhe. Rais wale walioua? 
Na Mussa Ally 

Mtazamo wa madhalimu wa Tanzania kwa Waislamu 
Na Rajab Isa 

Aliyoyasema KK bungeni 

Waislamu mkoa wa Morogoro wampinga Yahya 
Na. Abu Adli  

Polisi wachafua mazingira ya msikiti wa Mwembechai 
Na Badru Kimwaga 

Wanawake wa Kiislamu Ubungo darajani wamuunga mkono Sheikh Bafadhil 
Na Kassim Juma 

Barua za wasomaji  

Mashairi  

Mafundisho ya Qur'an: Kanuni za kumkumbuka Allah na kutumia katika njia yake 

Masomo  

Chakula na lishe: Lishe ya mtoto aliyekuwa mgonjwa 
Na Mujahiid Mwinyimvua 
 

 

 

 
 Kutoa maoni yako kuhusu ukarasa huu:
Bonyeza hapa
Au
Andika barua  kwa: webmaster@islamtanzania.org
 
Home Links Islam Tanzania Matoleo yaliyopita