|
|
|
Wananchi kataeni kupotoshwa Waziri wa Mambo ya Ndani, Mhe. Ali Ameir katika hotuba yake Bungeni amesema kwamba vurugu za Mwembechai zilisababishwa na vikundi vya dini ambavyo vingine vimesajiliwa na vingine havina uhalali wowote kisheria ila vipo tu na vinatumiwa kuendeleza ghasia na maovu. Aidha akasema vikundi hivyo vinahubiri kashfa na chuki baina ya dini na dini. Kutokea hapo Mhe. Waziri akasema kwamba wapo viongozi wamejitumbukiza katika kuvitetea vikundi kama hivyo na kuanzisha malumbano dhidi ya serikali. Na akadai kwamba viongozi wa aina hii hawalitakii mema taifa letu huku akiwashawishi wananchi wote wawakatae viongozi hao na wakatae kupotoshwa na viongozi aliodai "wachache wenye uchu wa umaarufu na madaraka." Kwanza tungependa Mhe. Ali Ameir atueleze zile Balozi za nje zilizohusika awali ni zipi na amezichukulia hatua gani. Pamoja na Balozi hizo, wananchi wangependa kujua vyama gani vya siasa vilihusika kwa ushahidi na vimechukuliwa hatua gani. Pili, Mhe. Waziri angetueleza ni vyama gani hivyo vya kidini vinavyotumia kivuli cha dini kuendeleza ghasia na maovu. Kisha aueleze umma wa Watanzania ni lini na wapi vyama hivyo vilileta ghasia vikaua au kuharibu mali za raia au serikali kabla ya polisi kuvamia msikiti wa Mwembechai na kuua au pale walipowavamia kule Mwananyamala Februari 12, ni ghasia na maovu gani yaliyokuwa yanafanyika pale msikitini. Mhe.Waziri amesema vikundi hivyo vimehubiri chuki na kashfa dhidi ya dini nyingine.Chuki gani na kashfa gani. Dini gani zimeparurana kuonyesha kwamba zinachukiana. Dini gani iliyoshitaki mahakamani kwamba inakashifiwa na ikaiainisha hiyo kashfa yenyewe. Kama ipo kashfa sheria inasema wauliwe au wafikishwe mahakamani. Hatuna kumbukizi ya kiongozi yeyote wa dini yoyote kufungua kesi ya kashfa dhidi ya dini nyingine. Labda Mhe. Waziri atueleze dini hiyo inayokashifiwa dini gani, je; ni dini ya serikali ndio maana inakuja juu na kuua bila hata kwenda mahakamani? Kiongozi yeyote mwenye busara na mwenye kujali maslahi ya nchi ya muda mrefu hawezi kuifumbia macho dhulma. Hawezi kuridhika kuona jamii moja katika nchi inaonewa, kudhalilishwa na kunyimwa haki zao. Ataikemea dhulma ili kuepusha yale ya Rwanda, Burundi, Ireland, Lebanon n.k. Hawa ndio wenye kuitakia mema nchi. Hawa ndio wazalendo wenye kujali amani na usalama wa nchi wa kudumu. Hawa ndio wenye kujali maslahi ya wananchi wanyonge wote. Hawa wapo pamoja na wananchi.Na wananchi hawatokubali kupotoshwa na wachache wanaotumiwa kutetea maslahi binafsi ya wachache na ya muda mfupi pamoja na ‘better chance’ za dini zao. Waislamu na watu kote duniani wameweka historia ya kusimama pamoja na wale wanaopambana na dhulma. Hapa Tanzania haitokuwa kinyume. Wananchi hawatosimama na wale waliowatesa wazee wa mika 83 mpaka wamechanganyikiwa wala hawatosimama pamoja na wale walioua. |
TAHARIRI Maoni yetu: Wananchi kataeni kupotoshwa SUALA LA MWEMBECHAI: Wabunge
wataka kujua nani aliamrisha kuua
Katiba ya nchi yapuuzwa: Waislamu wapigwa marufuku kuhubiri Mtihani darasa la saba 1998: Manispaa
Moro yaagiza ipewe majina ya wanafunzi Wakatoliki
“Wushu”ya Waislamu wa China
na jinsi ilivyowasaidia kupambana na dhulma dhidi yao
Yesu wa kwenye Mathayo siyo Yesu wa
kwenye Luka
Ni nani hawa Waislamu wa Siasa Kali
?
Waislamu tuondokane na unyonge
Waislamu wana mwelekeo wao
Ni mwaka gani Yesu alianza kuitwa
Mungu
Wanawake wameamua kuwa wazi
kweli kweli
Kimya kingi kina mshindo mkuu:
Vipi Mhe. Rais wale walioua?
Mtazamo wa madhalimu wa Tanzania
kwa Waislamu
Waislamu mkoa wa Morogoro
wampinga Yahya
Polisi wachafua mazingira
ya msikiti wa Mwembechai
Wanawake wa Kiislamu Ubungo
darajani wamuunga mkono Sheikh Bafadhil
Mafundisho ya Qur'an: Kanuni za kumkumbuka Allah na kutumia katika njia yake Chakula na lishe: Lishe ya
mtoto aliyekuwa mgonjwa
|