|
Na. 049 Jumatano Mei 24 - 30, 2000 |
|
|
|
|
|
CCM yatuhumiwa Na Mwandishi Wetu Wasiwasi na hofu vimeendelea kujengeka miongoni mwa wananchi juu ya iwapo chama tawala cha CCM kinajenga mazingira ya kuwepo kwa uchaguzi wa haki na huru kwa kutoingilia uhuru wa vyombo vya habari na uhuru wa watu kutoa maoni yao, imefahamika. Hali hii imetokana na kushindikana kurushwa hewani kipindi maarufu cha televisheni cha Kiti Moto ambapo mgeni mwalikwa katika kipindi hicho alikuwa Askofu Mkuu Zakaria Kakobe wa Kanisa la Full Gospel Bible Fellowship ambaye katika siku za hivi karibuni aliwahi kukikosoa hadharani Chama cha Mapinduzi(CCM) kwa madai kuwa viongozi wake ni waoga na wanafiki.Gazeti moja la kila siku la Mei 21 liliripoti kuwa viongozi wa CCM ndio walioshinikiza kanda hiyo isitangazwe. Shutuma hizo za Askofu Kakobe zilijibiwa na viongozi wa chama hicho akiwemo Katibu Mkuu wa CCM, Bw. Philip Mangula na Mwenyekiti wa Taifa wa Umoja wa Vijana wa CCM, Bw. Emmanuel Nchimbi, ambapo wote wawili walimponda Askofu huyo. Katika maelezo yake, Bw. Mangula alimwelezea Askofu Kakobe kuwa ni mtu anayestahiki "kusamehewa tu na CCM", wakati Bw. Nchimbi alimtaka Askofu Kakobe achague kati ya siasa au dini. Mpambano huo kati ya Askofu na viongozi wa chama tawala ambao ulitoa mvuto wa aina yake kwa wananchi inaaminika ndio uliopelekea kuandaliwa kwa kipndi hicho na kumshirikisha Askofu kakobe ambaye alihudhuria na kipindi kurekodiwa kama kawaida. Kipindi cha Kiti Moto kwa kawaida hurushwa hewani siku ya Alhamisi na Kituo cha Televisheni cha DTV; na kipindi hicho kilichomrekodi Askofu Kakobe kilitarajiwa kutoka wiki iliyopita lakini mpaka sasa hakijatolewa hadharani na wala hazijaelezwa sababu zozote kuhusiana na hali hiyo isiyo ya kawaida. Nasaha jana iliwasiliana kwa simu na ofisi ya Askofu Kakobe kutaka kujua iwapo kuna habari zozote za kuhusu sababu za kipindi hicho kutorushwa hewani na ni nini maoni na nasaha zake kwa watanzania. Hata hivyo Katibu Muhstasi wa Askofu huyo alijibu kwamba Akofu Kakobe hakuwepo ofisini kuweza kuzungumzia suala hilo na kwamba hapakuwa na kiongozi mwingine yeyote wa Kanisa ambaye angeweza kuzungumza kwa niaba ya Askofu Mkuu huyo wa Kanisa la Full Gospel Bible Fellowship. Aidha Katibu huyo muhtasi alifafanua kuwa Askofu Kakobe alikuwa nje ya ofisi akishughulika na wanafumnzi wake. Hivi karibuni Kanisa hilo lilipata wachungaji wa kwanza ambao walibarikiwa na Askofu Kakobe mwenyewe. Nasaha pia iliwasiliana kwa simu na Ofisi za DTV kutaka kujua kilichokwamisha kipindi hicho ambacho uchunguzi wa gazeti hili umebaini kilikuwa kikingojewa kwa hamu na wananchi ambapo msemaji wa ofisi hiyo ‘aliutupa mpira’ kwa waandaji wa kipindi hicho, Maasai studio. "...tafadhali wasiliana na Maasai Studio, wao ndio walioandaa..." Juhudi za kuwasiliana na Maasai Studio hazikufanikiwa. Wachunguzi wa masuala ya kisiasa na kijamii nchini wanadai kuwa kanda hiyo imezuiliwa isitoke kwa shinikizo la CCM kwa vile "yaliyomo katika kanda hiyo ni mapigo dhidi yake". Hofu ya CCM kuporomoshwa kutokana na shutuma za viongozi wa dini zimeongezeka kwa vile shutuma hizo za Askofu Kakobe zimekuja sambamba na shutuma dhidi ya viongozi wa siasa nchini zilizomo katika kitabu kilichotolewa na Tume ya Haki na Amani ya Baraza la maaskofu nchini ambapo watu wengi wameeleza kuwa viongozi wa kisiasa waliokusudiwa katika kitabu hicho ni wa CCM kwa vile wao ndio wenye serikali. Kadhalika viongozi wa kiislamu nchini wamekuwa wakiishutumu serikali kwa kutowatendea haki waislamu hususani suala la mauaji ya Mwembechai. |
YALIYOMO
TAHARIRI
Chuo Kikuu Dar wafanya mitihani katika Bwalo la chakula Udini wa CCM utaisambaratisha nchi -Tambwe ‘Kutoweka’ kanda ya Kakobe: CCM yatuhumiwa Maalim Seif awaambia Wazanzibari: Wenye mamlaka ya kumuweka mtu Ikulu ni wananchi Mkapa afurahia maendeleo Pwani ‘Zawadi’ ya Uchaguzi yatishia kusambaratisha taasisi ya Kiislam Tanga Serikali yakemea mwanamke kudhalilishwa Ushauri Nasaha
MAKALA
Makala
Kalamu ya Mwandishi
MAKALA
Makala
Makala
RIWAYA
Lishe
|
|
|
|
|