NASAHA
Na. 049 Jumatano Mei 24 - 30, 2000
Ukurasa wa mwanzo
Islam Tanzania
Matoleo yaliyopita
Udini wa CCM utaisambaratisha nchi -Tambwe

Na Mwandishi Wetu

Mwenyekiti wa chama cha CUF Wilaya ya Temeke, ambaye pia ni mgombea wa ubunge wa chama hicho katika jimbo hilo amesema, udini wa CCM utaisambaratisha nchi.

Akizungumza kama mgeni rasmi katika mkutano wa kumpongeza Prof. Lipumba kwa hatua yake ya kuchukua fomu za kugombea Urais uliofanyika Kigogo, jijini Mei 21 mwaka huu, Bwana Hiza alisema, CCM imekuwa ikiutumia wingi wa Waislamu kupata kura zao kwa kumtumia Sheikh Mkuu wa Bakwata kuwafanyia kampeni misikitini. Ili kuficha ukweli huo CCM imekuwa ikikituhumu chama cha CUF kuwa kinawatumia Waislamu kukifanyia kampeni misikitini.

Huko nyuma Katibu Mkuu wa CCM Bwana Philip Mangula amewahi kuripotiwa akidai kuwa Waislamu wamekuwa wakihongwa kanzu, kanga na kofia ili kuendesha siasa misikitini.

Kauli ya Katibu huyo wa CCM ililaaniwa vikali na viongozi wa Kiislamu ikiwemo Shura ya Maimamu inayoongozwa na Sheikh Mbukuzi iliyomtaka Bwana Mangula afute kauli yake na kuwaomba radhi Waislamu.

Hata hivyo imefahamika hivi karibuni kuwa Sheikh Mkuu wa BAKWATA Hewmed Bin Jumaa akiongoza ujumbe wa chama hicho cha BAKWATA imeripotiwa akipita mikoani kuipigia kampeni CCM misikitini. 

Wakati ujumbe huo wa BAKWATA ukiwa mjini Iringa ilielezwa kuwa mmoja wa Masheikh katika ujumbe huo, Bwana Bafadhil alihamasisha kwa kusema "Mkapa juu".

Akiendelea kufafanua Mhe. Tambwe Hiza alisema kuwa kitendo hicho si tu kuwa ni udini katika kampeni lakini pia ni kuwadhalilisha Waislamu kwamba si welevu na kwamba wao ni watu wa kutumiwa." Kwanini CCM haiwatumii mapadre na maaskofu kupiga kampeni, badala yake.

Mwenyekiti huyo wa CUF Wilaya ya Temeke ambaye anapewa nafasi kubwa ya kushinda ubunge katika jimbo la Temeke na wananchi amesema kuwa CCM imekuwa ikipiga propaganda kuwa CUF ni chama cha Waislamu ili kuwazuia Wakristo wasijiunge nacho. Akasema hiyo ni hatua mbaya ambayo inaweza kuwagawa wananchi kwa dini zao kama wananchi wasipotumia akili zao vyema kung’amua propaganda hizo za CCM. Akaongeza kusema kuwa Wakristo warevu kama yeye hawababaishwi na propaganda hizo na wanaendelea kujiunga na chama hicho siku hadi siku.

"Sisi katika CUF tunatambua kuwa huwezi kutumia Biblia wala Qur’an katika kujenga barabara, mahospiali wala mashule. Bali kuwa na mipango mizuri na kwa kutumia vyema kodi ya wananchi", alisema Mhe. Tambwe na kuongeza kuwa propaganda hizo za CCM wao haziwasumbui na ni dalili ya kufilisika kisiasa.
 

Juu
 

YALIYOMO
 

TAHARIRI
KERO katika Elimu ziondolewe haraka

Chuo Kikuu Dar wafanya mitihani katika Bwalo la chakula

Udini wa CCM utaisambaratisha nchi -Tambwe

‘Kutoweka’ kanda ya Kakobe: CCM yatuhumiwa

Maalim Seif awaambia Wazanzibari: Wenye mamlaka ya kumuweka mtu Ikulu ni wananchi

Mkapa afurahia maendeleo Pwani

Wapinzani wajiimarisha Moro

‘Zawadi’ ya Uchaguzi yatishia kusambaratisha taasisi ya Kiislam Tanga

Serikali yakemea mwanamke kudhalilishwa

Ushauri Nasaha
Umuhimu wa kushirikiana na majirani katika malezi ya watoto

MAKALA
Afande Mahita, wananchi hatutaki Dola ya kipolisi

Makala
CCM hawawezi kuondoa umasikini, ndio tegemeo lao

Kalamu ya Mwandishi
Makubaliano kwa vitendo Z'bar

MAKALA
CCM na sera za maendeleo (5)

Makala
Wanawake na maendeleo: Je ni wimbo wa kuchaguliwa?

Makala
CCM inatawala badala ya kuongoza

Habari za Kimataifa

RIWAYA
Mapinduzi ya fikra -4

Lishe
Unachotakiwa kufanya kabla ya kuweka chakula kwenye jokofu

BARUA

MASHAIRI

MICHEZO

  • Raza kufungua mashindano ya Wavu Zanzibar
  • Real Madrid yaota Ubingwa  leo
  • Kajumulo asema Yanga timu ya Wananchi

  •  


       Kutoa maoni yako kuhusu ukarasa huu:Bonyeza hapa
    Au
    Andika barua  kwa: nasaha1420@yahoo.com

    Ukurasa wa mwanzo
    Islam Tanzania
    Matoleo yaliyopita