|
|
| Fuateni
Sharia ya Allah - Sheikh
Na Badru Kimwaga Imeelezwa kuwa vitendo viovu na kuharibika kwa maadili ya jamii huchangiwa kutokana na kupuuzwa kwa sheria za Mweneyezi Mungu, ambayo inaelekezwa na Kitabu kitakatifu cha Qur-an na pia kudhaniwa kuwa sheria za Mwenyezi Mungu ndani ya Kitabu hicho kinawahusu Waislamu peke yao. Hayo yameelezwa na Sheikh Idd Mohamed alipokuwa akiongea na waumini wa Msikiti wa Bonde la Mpunga Msasani, mara baada ya swala ya Alasir, Msikitini hapo, jijini wiki iliyopita. Sheikh Mohamed alisema kuwa watu wengi hudhani kuwa Qur-an ni Kitabu cha Waislamu tu na sheria zake zinawahusu wao, wakati ukweli ni kwamba sheria za Mwenyezi Mungu zinawahusu binadamu yeyote aliye ndani ya zama za Umma wa Mtume Muhammad (s.a.w.). "Maovu yamezidi kutokana na sheria za Mwenyezi Mungu kutofuatwa, huku Waislamu wanapoitangaza na kueleza bayana wako watu wenye kupinga ilihali zina malengo ya kuendesha maisha ya binadamu zama hizi katika ulinganifu bila kuzingatia yupi dini ipi na yupi Muislamu "Alisisitiza Sheikh Mohamed. Aliongeza kuwa, sheria kama za kukataza watu kuzini kulingana na Qur-an inakataza, lakini watu wenye kumuhalifu Mungu, ndio kwanza husisitiza matumizi ya kondomu, ikiwa unataka kujiepusha na ukimwi, wakati kama ingetekelezwa sheria hiyo, hakungekuwa na magonjwa ya zinaa kama ukimwi. Pia aligusia mambo ya wizi, ubakaji na kunajisi na kusema kuwa hii ni kazi na laana ya kuacha sheria za dini ya Kiislamu, iliyo ndani ya kitabu cha Qur-an na kuwaomba Waislamu kuwa watendaji wakuu katika kuitekeleza iili kuwavutia watu wasio Waislamu kuona umuhimu wa kuzingatia sheria hizo. "Lau watu wangelishikama na sheria zangu ningeliwaneemesha neema mbalimbali (alinukuu Aya) lakini je tunashikama na kamba hiyo au ndiyo wenye kupinga na kujifanya binadamu tuna akili nyingi kuliko aliyetuumba, Astaqafirullah... "Alisema Sheikh Mohamed na kumalizia. Alitoa mfano kwa kusema nchi zinazozingatia Qur-an ugonjwa kama ukimwi
na uhalifu hutendwa kwa asilimia kidogo kulinganisha na nchi nyingine zinazodai
kustaarabika ingawa sio kweli.
Wanawake wa Kiislamu Mburahati wahimizwa kutafuta elimu Wanawake wa Kiislamu Mburahati Jijini Dar es Salaam wamehimizwa kujipinda kuijua dini yao ili waweze kuishi kwa mujibu wa mafundisho yake. Wanawake hao wametakiwa pia kuwa na mapenzi miongoni mwao kwa kupeana sadaqa na kutembeleana. Hayo ni baadhi ya mambo yaliyoelezwa katika mada mbali mbali zilizowasilishwa katika kongamano la wanawake wa Kiislamu lililofanyika Oktoba 10, 1998 Masjid Aqswa Mburahati Jijini Dar es Salaam. Akizungumza katika kongamano hilo Bi. Tunda alisema kwamba kutafuta elimu, upendo na utoaji wa sadaqa ni vitu vinavyoweza kumsaidia Mwanaadamu dunia na akhera, hivyo aliwataka wanawake hao kushikamana na vitu hivyo. Mzungumzaji mwingine Bi. Fatma alitolea mfano wa utekelezaji wa nguzo ya zaka kama ni moja ya mambo yanayoweza kustawisha udugu miongoni mwa jamii. Mzungumzaji aliyeonekana kuvuta hisia za wengi alikuwa Bi. Amina ambaye alizungumzia madhila mbalimbali yanayowafika Waislamu wa hapa nchini. Alisema kadhia ya Mwembechai imethibitisha malalamiko ya Waislamu kwamba hawatendewi haki sawa na raia wengine. Alitoa mfano wa mambo waliyotendewa wanawake wa Kiislamu Mwembechai na kuhoji ni hatua gani ilizochukuwa Serikali dhidi ya wahusika. Aidha, mzungumzaji huyo aligusia suala la Nzasa na kusema kwamba anasikitishwa na jinsi Serikali ilivyowatendea wananchi wa eneo hilo. |
YALIYOMO
TAHARIRI
Wasomi watetea haki ya wananchi kumiliki ardhi Serikali izungumze na wananchi–Mzee Gonga Akina mama watakiwa kushikamana na dini yao Maoni
Dondoo
za Saikolojia: Hoja kengeza
Makala ya mtangazaji
Makala
Tanzania
tuna sera gani kuhusu kanda
Mdahalo
kati ya Waislamu na Wakristo- 2
Teknologia
Makala na habari
Mwinyimkuu
kufanya sensa ya waumini Magomeni
Wazazi
Mwanza wahimizwa kuwashonea watoto wao Hijab
Tuwaige
Wangazija, 'tutafanikiwa'
Serikali
imeweka rekodi ya kutisha – Sheikh Salim
Muhadhara
waunguruma Geita
Fuateni
Sharia ya Allah - Sheikh
Wanawake wa Kiislamu Mburahati wahimizwa kutafuta elimu Mafunzo
ya Qur'an
Chakula na lishe
|