AN-NUUR
Na.156 Rabi' Awal 1419, Julai 4 - 9, 1998
 
Home Links Islam Tanzania Matoleo yaliyopita
 
Wanawake Waislamu Morogoro wakutana na kusema Hawatarudi nyuma mpaka dhulma iondoke 

Wadai wauaji wafikishwe mahakamani

Waliowadhalilisha wanawake waadhibiwe

Wamuunga mkono Sheikh Bafadhil

Na Mwandishi Wetu, Morogoro
 

WANAWAKE wa Kiislamu mjini Morogoro wamesema kwamba wanaungana na Waislamu kote nchini katika juhudi za kuondoa dhulma dhidi ya Waislamu na kwamba hawatarudi nyuma wala hawatahofu mpaka haki ipatikane.

Aidha, wanawake hao wamesema kwamba wanalaani mauaji ya Waislamu yaliyofanywa na polisi Mwembechai na kile kitendo cha wanawake kudhalilishwa na kunyanyaswa mikononi mwa polisi na askari Magereza.

Katika tamko lao baada ya mkutano wao wa Juni 28, 1998 nje ya Msikiti Mkuu wa Ijumaa Mjini Morogoro, wanawake hao wamelaani matumizi ya mabavu katika uendeshaji wa shughuli za serikali na hususani kitendo cha askari polisi kuua wananchi, kuvamia na kunajisi Misikiti, kuwapiga na kuwatesa wananchi kinyume na taratibu za kisheria.

Aidha, wamesema wanaungana na Masheikh na Maimamu wao wanaosimama kueleza na kupinga dhulma dhidi ya Waislamu. Katika nukta hii, wamesema wanamuunga mkono Sheikh Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Sheikh Omar Bafadhil kwa jitihada anayoifanya kutetea haki za Waislamu.

Awali, katika kuwasilisha mada ya mjadala, akina mama hao walisisitiza kwamba, muda wote Waislamu ni wagumu kwa makafiri na madhalimu wote, ila huwa wapole na wenye kuhurumiana wao kwa wao (48:29). Ni kwa ajili hiyo wamesema, wamelazimika kukutana kuzungumzia madhila waliyofanyiwa Waislamu wa Mwembechai.

Wakitoa mada katika kongamano hilo, wanawake toka Msikiti wa Mafiga waliwakumbusha wanawake wa Kiislamu warejee historia ya Uislamu, waone jinsi wanawake walivyotoa mchango mkubwa katika kuuhami Uislamu.

Pamoja na matamko yaliyotolewa katika kongamano, lakini kubwa zaidi, wanawake wamehimizwa wawe tayari kujitoa mhanga kwa ajili ya dini yao.

Juu
 
 

 

YALIYOMO
 
TAHARIRI 

Maoni yetu:Tusianze kuulizana tena shida yenu nini 

Agizo la Rais Mkapa lapuuzwa:Wazee wa miaka 80 wateseka Gerezani

Wanawake wasema hawatarudi nyuma mpaka dhulma iondoke

Serikali kuzuia mahubiri ya Waislamu, kuvamia Msikiti, kukamata, kudhalilisha na kuua Wananchi ni kuvunja Katiba na Sheria za Nchi

Kujua lugha ya Kiarabu sio kuujua Mwongozo wa Allah
Na Sadick M. Sadick"

Serikali isidhani kuwa Waislamu wa Tanzania wamelala usingizi

Intifada ndio jibu (2)
Na Sheikh Pandukizi Dilunga

Kusema ukweli ni sehemu ya uadilifu
A.S. Chachika

Mafumbo ya imani yabakie ndani ya Makanisa
Na J. Hussein

Majibu kwa Kamara Kusupa

Tamko la Wanawake wa Kiislamu mkoa wa Morogoro kuhusu kadhia ya Mwembechai

Asiye na elimu kwa mujibu wa Biblia
Na Sheikh Bernard P. Nyangasa

TAMTA yaadhimisha miaka 36
Na Masoud Mohamed Said, Tanga

Muumini aliyeachiwa aeleza jinsi Waislamu wanavyoteswa Segerea
Na Muhibu Said

Wakwama kujenga msikiti kwa miaka 30

Habari za Madrasa

Barua 

Mashairi 

Lishe : Mtoto anyonye maziwa ya mama miaka miwili 
Na Dk. Ali. A. Mzige
  

 

 

 
 Kutoa maoni yako kuhusu ukarasa huu:
Bonyeza hapa
Au
Andika barua  kwa: webmaster@islamtanzania.org
 
Home Links Islam Tanzania Matoleo yaliyopita