AN-NUUR
Na.156 Rabi' Awal 1419, Julai 4 - 9, 1998
 
Home Links Islam Tanzania Matoleo yaliyopita
 
Maoni yetu

Tusianze kuulizana tena shida yenu nini

TUNASHUKURU kwamba kila ambalo Waislamu wamekuwa wakilalamikia au kudai kama haki yao, wameliwekea kumbukumbu ambazo zaweza kuwasilishwa katika Mamlaka, Majlis na Mahakama yoyote duniani kama ushahidi.

Makala, waraka, vitabu na barua rasmi zimekuwa zikiandikwa na watu binafsi, Jumuiya na Taasisi za Kiislamu , kuweka ushahidi wa malakamiko na madai ya Waislamu.

Huko Serikalini nako, kumbukumbu zipo.

Waziri wa Elimu wakati fulani alishaandaa dokezo rasmi kutaka mfumo wa elimu uangaliwe ni vipi unakwaza sehemu ya jamii kupiga hatua. Dokezo hilo lilijadiliwa hadi katika vikao rasmi vya chama CCM.

Na haya aliyozungumza Mbunge wa Kigamboni, Mh. Kitwana Kondo bungeni ni ushahidi na kumbukumbu nyingine.

Alhamdulillah kumbukumbu za vikao vya Bunge la Tanzania litakuwa limerekodi hoja za Waislamu juu ya dhulma zinazofanywa dhidi ya Waislamu.

Wakati wa Uchaguzi Mkuu mwaka 1995, Waislamu waliulizwa shida yenu nini, matatizo yenu nini. Sasa baada ya yote haya pamoja na yale aliyosema Mh. Kitwana Kondo, Waislamu hawategemei kuulizwa tena "shida yenu nini".

Mwananchi ni haki yake kupiga kura na yeyote ana haki kushawishi wapiga kura wamchague. Lakini sio katika vikao vya chakula vya kibarazani.

Itakuwa ni jambo la kushangaza sana na kwa kweli kejeli kubwa kama baada ya "piga yule", baada ya "Mohamed Omar", baada ya "Chuki Athumani" na haya aliyosema Mh. Kondo, atatokea Mheshimiwa mwingine kuuliza "shida yenu nini".

Shida yetu dhulma iondoke. Shida yetu walioua wakamatwe, wafikishwe mahakamani,. Shida yetu "Inquest".

Mheshimiwa Kitwana Kondo kahitimisha, kaweka kumbukumbu. Msemo wa AN-NUUR isije semwa hatukusema.

Tunayasema haya kwa sababu kesho na keshokutwa wasijeitwa watu katika vikao vya pembeni vya kahawa na visheti na kuulizwa shida yenu nini! Mkaanza kuongopeana hamjui na hamna watu wa kuwaambia.

K.K. hamkumsikia? Waraka wa Ponda hamkuusoma? Abu Azizi naye vipi? Sivalon je!

Yaliyomsibu Chuki Athumani hayawatoshi kuwa somo! Shida yetu dhulma iondoke lakini pamoja na haya, Mtume (s.a.w.) anasema: Muislamu ni yule ambaye Waislamu wenzake wamesalimika na ulimi wake. Sio kuwakera kila siku hata katika masiku yao ya furaha na sherehe. Na hivi karibuni tutawasikia katika Baraza la Maulid.

Wamepigwa risasi watu na kuuliwa, wengine sasa vilema na wengine bado wanateseka magerezani. Chimbuko la yote ni kukiri kwao upweke wa Mungu Muumba na kuukataa Utatu. Wengi yamewakuta yaliyo wakuta kwa kukataa kwao kuimba wimbo wa "pambio". Heri yao walioimba kwa hiari yao waliimba kwa furaha na kunyanyua mikono juu.

Juu 
 

YALIYOMO
 
TAHARIRI 

Maoni yetu:Tusianze kuulizana tena shida yenu nini 

Agizo la Rais Mkapa lapuuzwa:Wazee wa miaka 80 wateseka Gerezani

Wanawake wasema hawatarudi nyuma mpaka dhulma iondoke

Serikali kuzuia mahubiri ya Waislamu, kuvamia Msikiti, kukamata, kudhalilisha na kuua Wananchi ni kuvunja Katiba na Sheria za Nchi

Kujua lugha ya Kiarabu sio kuujua Mwongozo wa Allah
Na Sadick M. Sadick"

Serikali isidhani kuwa Waislamu wa Tanzania wamelala usingizi

Intifada ndio jibu (2)
Na Sheikh Pandukizi Dilunga

Kusema ukweli ni sehemu ya uadilifu
A.S. Chachika

Mafumbo ya imani yabakie ndani ya Makanisa
Na J. Hussein

Majibu kwa Kamara Kusupa

Tamko la Wanawake wa Kiislamu mkoa wa Morogoro kuhusu kadhia ya Mwembechai

Asiye na elimu kwa mujibu wa Biblia
Na Sheikh Bernard P. Nyangasa

TAMTA yaadhimisha miaka 36
Na Masoud Mohamed Said, Tanga

Muumini aliyeachiwa aeleza jinsi Waislamu wanavyoteswa Segerea
Na Muhibu Said

Wakwama kujenga msikiti kwa miaka 30

Habari za Madrasa

Barua 

Mashairi 

Lishe : Mtoto anyonye maziwa ya mama miaka miwili 
Na Dk. Ali. A. Mzige
  

 

 

 
 Kutoa maoni yako kuhusu ukarasa huu:
Bonyeza hapa
Au
Andika barua  kwa: webmaster@islamtanzania.org
 
Home Links Islam Tanzania Matoleo yaliyopita