|
Na. 050 Jumatano Mei 31 - Juni 5, 2000 |
|
|
|
|
|
Na Mwandishi Wetu SERIKALI imetoa muelekeo wa budget ya mwaka wa fedhaujao 2000/2001, na hapo hapo kutoa tahadhari ya njaa inayokabili nchi mwaka huu. Taarifa hiyo ya muelekeo wa bajeti imetolewa na Waziri Daniel Yona mbele ya kamati ya Bunge ya Fedha, uchumi na Huduma za Jamii, tarehe Mei 29, 2000 kwenye ofisi za Bunge jijini. Taarifa hiyo imeonesha kwamba serikali itatumia jumla ya shilingi bilioni 1,389.5 kwa ajili ya maendeleo na matumizi ya kawaida. Pamoja nataarifa hiyo, Serikali pia imetangaza kuwa hali ya chakula nchini ni mbaya kuashiria kuwepo kwa njaa mwaka huu kuanzia mweziJulai. Taarifa hiyo ya kuwepo kwa njaa ilitolewa naWaziri wa TawalazaMikoa na Serikali za Mitaa, Mhe. Kingunge Ngombale Mwiru juzi Mei 29, mwaka huu wakati akiwasilishamuelekeo wa bajeti ya Wizara yake kwa kamati za Bunge za Fedha na Huduma za Jamii katika ofisi za Bunge jijini Dar es Salaam. Mhe.Kingunge alieleza kuwa sababu ya hali hiyo ya njaa inatokana na upungufu wa mvua za msimu wa vuli ambao umeathiri umefifisha tegemeolakupata mavunano katikamaeneo ya Kilimanjaro, Arusha, Tanga, Pwani,Lindi, Mtwara, Singida, Dodomana Tabora. Mhe. Kingunge alieleza kuwa kwa kuwa asilimia 80 ya wananchi wanaishi vijijini, ni vyema wananchi hao na wananchi wote kwa ujumla wao kuiwekea akiba ya chakula kitakachopatikana baada ya mavuno. Alishauri piawalewatakaopata mavuno machachewanunue na kujiwekea akiba. Taarifa ya Mhe. Kingunge ingawa ni ya kuhuzunisha, imepongezwa nabaadhi ya wananchi kwa kuwa imeweka wazi mambo ambayo huko nyumayalikuwa hayatolewi njemapema. Maka 1998 maeneomengi ya nchi yalikumbwa nanjaa kiasi cha baadhi yaokufa kwa njaa hiyo Wilayani Ulanga. Taarif aza njaa ya mwaka huo hazikuwekwa wazi mapema na hata taarifa za vifo hivyo awali zilianza kukanushwa. |
YALIYOMO
TAHARIRI
Zanzibar wadai kuyumbishwa na Bara Serikali yatoa muelekeo wa Bajeti na kutangaza njaa Habari za ndani
SMZ haishughulikii mikarafuu -Maalim Seif Mwalimu Mkuu Msimbazi Mseto atishia kujiuzulu Hizi ni 'arobaini' za mapandikizi Waislamu Mbeya wamsusa Sheikh Mkuu wa BAKWATA Masheikh wa BAKWATA waongoza sherehe za kuwasimika makamanda wa vijana wa CCM MAKALA
Makala
MPASHO NASAHA
Kalamu ya Mwandishi
MAKALA
Habari za Kimataifaza Kimataifa Lishe
RIWAYA
Ambari, Mwakipesile wajitosa kugombea DRFA |
|
|
|
|