AN-NUUR
Na.164 Jamada Awal 1419, Agosti 28 - Septemba 3, 1998
Home Links Islam Tanzania Matoleo yaliyopita
 S.L.P. 55105, SIMU 181365, DSM

TAHARIRI

Dawa ya ugaidi si kufanya ugaidi ndani ya ugaidi


 




Akiongea baada ya shambulio la Agosti 21, dhidi ya Sudan na Afghanistan Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje wa Marekani Bibi Albright alisema kwamba magaidi waweza kujificha lakini hawawezi kuukwepa mkono wa sheria. Naye Waziri wa Ulinzi Bw. William Cohen akasema kwamba hapatakuwa na vikwazo vyovyote katika azma ya Marekani kulinda raia wa Marekani na maslahi yao, pamoja na maadili ya demokrasia na sheria.

Maneno ya wakubwa hawa hayana tatizo; swali ni je; Marekani yenyewe inafuata sheria; na je; inajali demokrasia.

Je, kuipiga Sudan na Afghanistan bila ya ushahidi wowote wa kisheria unaotambulika na jumuiya ya kimataifa ndio sheria?

Kujichukulia mamlaka mkononi bila kujali kanuni za Baraza la Umoja wa Mataifa na Baraza lake la Usalama; ndio demokrasia na sheria!

Marekani imekuwa ikishinikiza kuadhibiwa kwa Iraq na Libya kwa kile ilichodai nchi hizo kupuuza maamuzi ya Baraza la Usalama. Je, kwakujichukulia mamlaka kinyume na taratibu za Baraza la Usalama ndio Marekani imeliheshimu Baraza hilo!

Je; kwa Marekani kulishinikiza Baraza la Usalama lisipeleke tume ya uchunguzi Sudan kuchunguza madai yake kwamba kiwanda ilichoshambulia kinatengeneza silaha za sumu, ndio demokrasia na sheria!

Sheria gani inategemea ushahidi wa upande mmoja! Sheria gani ambapo mtuhumu anakuwa ndiye shahidi, hakimu na mnyongaji! Marekani inaituhumu Sudan, Marekani hiyo hiyo imesema inaushahidi kisha yenyewe inatoa hukumu na kutoa adhabu!

Akitetea tendo hilo la kuipiga mabomu Sudan na Afghanistan msemaji wa upande wa sheria wa Marekani amesema kwamba hata mwaka 1986 Reagan aliipiga Libya baada ya bomu kulipuka katika disco huko Ujerumani ambapo wanajeshi kadhaa wa Marekani waliuliwa.

Hata hivyo msemaji huyo hakueleza kwamba Reagan alipiga Libya kwa kuituhumu na kusema kwamba ina ushahidi (kama inavyosema kwa Sudan leo) kwamba Libya ndiyo iliyolipua bomu katika ukumbi huo wa Disco. Ambapo baadae iligundulika kwamba Libya haikuhusika.Ubalakala na ubabe wa aina hii hauwezi kutatua matatizo ya ugaidi, na ukosefu wa amani duniani.

Kwa upande mwingine kama jambo ni ovu basi litakuwa ni ovu kama litafanywa na mkubwa au mdogo, masikini au tajiri, mtu binafsi au nchi. Na ni muhimu na ndio uadilifu wenyewe kwamba wahalifu wote wakemewe; vinginevyo utakuwa ni unafiki kukemea kosa linapofanywa na mnyonge na kufumba macho kosa hilo hilo linapofanywa na mwenye nguvu.

Dawa ya ugaidi si kufanya ugaidi ndani ya ugaidi.

Juu

YALIYOMO

TAHARIRI: Dawa ya ugaidi si kufanya ugaidi ndani ya ugaidi

Bakwata yalaani ubabe wa Marekani
Na Mwandishi Wetu

Wanakijiji wawapiga Polisi Olesiva
Na Mwandishi wetu, Arusha

Waislamu washinda kesi Same
Na Mwandishi Wetu, Same

Wasafiri ATC wadai ndege ya Jeddah inahujumiwa 
Na Mwandishi Wetu

KOSOVA: Bosnia nyingine

Mahojiano kati ya CNN na Bwana Usama bin Ladin

Historia ya damu za mashujaa Afghanistan

Msikiti wa Wagoma Kigoma wapata viongozi wapya
Na Suleiman Simba, Kigoma

Muhadhara wanguruma Masjid Hijaz
Na Said Shariff

Waislamu waitumie Misikiti ipasavyo
Na Ashraf Yusuph, Moshi

Mpango wa kudhibiti uzazi utawaangamiza wengi
Na Mwandishi Wetu

Hoja za kutofautisha Yesu na Issa ni udhaifu,  ni uzushi mtupu! - 3
Na Muhibu Said

Wanawake wa Kiislamu washiriki maonyesho ya kilimo
Na Habiba Swedi

Wanawake wa Kiislamu washauriwa kupigania haki zao
Na Habiba Swedi, Arusha

Africa Muslims Agency: Inavyohudumia jamii
Na Mwandishi Wetu

Kitengo cha Zakkah chasafirisha wanafunzi
Na Mwandishi Wetu

Kupinga kifo cha Yesu ni kumpinga Mungu?
Mahfudhi M. Mahfudhi

MAONI: Porojo za Ngatara -2

Zanzibar na  biashara ya utumwa
Na J. Hussein

Marekani ishitakiwe
Na Abubakar Msham

MAPENDEKEZO YA KATIBA YA SHIRIKISHO LA TANZANIA - 3

Mafundisho ya Quran

Barua za wasomaji

Mashairi

Masomo ya dini ya Kiislam

Chakula na Lishe
 
 
 
 

 

 Kutoa maoni yako kuhusu ukarasa huu:
Bonyeza hapa
Au
Andika barua  kwa: webmaster@islamtanzania.org

Home Links Islam Tanzania Matoleo yaliyopita