|
|
| Vigogo
wahusishwa na madawa ya kulevya Z'bar
Na Mwandishi Wetu Wabunge kutoka Zanzibar wameitaka Wizara ya Mambo ya Ndani kuwafichua vigogo na watu wazito katika jamii wanashiriki katika biashara ya madawa ya kulevya kuliko kuhangaika na vijana wa mtaani, huku wanaowapa madawa hayo wakiachwa. Aidha, Wabunge hao wametahadharisha juu ya uwezekano wa kuwepo kile walichokiita ‘Italian Mafia’ ambacho ni chanzo cha uhalifu wa kupangwa. Akiongea Bungeni hivi karibuni, Mbunge wa Jimbo la Mlandege Mhe. Fatma Said Ali alisema kwamba, hivi sasa biashara ya madawa ya kulevya imeshamiri sana Zanzibar na vijana wameharibika. Akaongeza kusema kwamba shughuli hii ya kuuza na kutumia madawa hayo hufanyika wazi katika maeneo ambayo yamebatizwa na kuitwa Argentina, Uruguay, Peru n.k. Aidha Mbunge huyo akasema katika maeneo ya Vikokotoni shughuli hizo ni maarufu. Katika hali hiyo ya kushamiri biashara hiyo na kufanyika kwa wazi kiasi hicho Mhe. Fatma Saidi Ali aliitaka Serikali iwabane vijana hao waeleze nani anawapa madawa hayo. Hoja ya Mhe. Mbunge Fatma ni kwamba vijana hao kwa hali zao hawana uwezo wa kupata fedha za kusafiri nje na kuyaleta madawa hayo ambayo huuzwa kwa fedha nyingi. Baadhi ya Wabunge wakiitahadharisha serikali kwamba pamoja na kuwa Utalii umekuwa ukiingizia serikali ya Zanzibar mapato lakini ipo haja ya kuangalia aina ya watalii wanaoingia Zanzibar. Mheshimiwa Hashul Nassor Ali alionya kwamba ipo hatari kuharibikiwa kama tahadhari haitachukuliwa. Akisherehesha nukta yake akinukuu maneno ya tahadhari ya Cris Maris kama yalivyoandikwa katika jarida la "Living Africa" la Shirika la Ndege la Aliance. Sehemu ya tahadhari hiyo, inazungumzia, "Rumours about the Presence of the Italian Mafia activities on the Island and some coastal parts are refugees of Western hippies and travellers escaping from the World." Kwa nukuu hiyo Mhe. Hashul aliitaka serikali kwamba pamoja na mapesa inayopata lakini ichukue tahadhari kubwa. |
Maoni yetu: Umakini wa Wabunge unatia wasiwasi AGIZO LA MANISPAA KUPEWA MAJINA YA
WANAFUNZI WA KIKATOLIKI
Madai ya Ali Ameir kuhusu Chuki yakanushwa
Mwanamuziki Nyota CAT STEVENS asimulia alivyosilimu Watakiwa kuacha kuwatuma watoto mitaani
Kijana wa Kibarbaig aliyejitolea kupigania
dini yake
'Waislamu wenye sisa kali'
MAKALA: Maisha ya ndoa kwa Muislamu
- 2
Mjibuni Mwinjilisti Kusupa msitukane
Vigogo wahusishwa na madawa ya kulevya
Z'bar
Da’awa Handeni yashika kasi
Kongamano la vijana wa
Kiislamu Masjid Nuur Dar
Mashairi - uzawa wa Mtume (S.A.W)
|