AN-NUUR  Na.174 Rajab 1419, Novemba 6 - 12, 1998 
 
Home Links Islam Tanzania Matoleo yaliyopita
 
Hoja pofu
 
Na Abu Halima Sa Changwa
 

KUNA watu ambao wana kawaida ya kutoa hoja pofu dhidi ya jambo walisilolipenda au wasilolijua undani wake. Hoja pofu ni hoja inayotolewa kwa kuangalia upande mmoja tu wa jambo bila ya kuzingatia upande mwingine. Watu wenye hoja pofu huona weusi (ubaya) wa jambo bila ya kuona weupe (au uzuri) wake. 

Angalia taswira iliyoambatanishwa hapa. Unaona viduara vitatu vyeusi vilivyokatwa. Je, unaona taswira yoyote nyingine zaidi ya viduara ? Kwa wengi ni vigumu kuona kitu kingine. 

Hebu weka fikra yako katikati ya viduara hivyo na utagundua kuwa mchoraji ametaka uone umbo la pembetatu nyeupe iliyochomekwa katikati ya viduara vitatu. Umeiona ? 

Mfano mzuri wa watu wanaoona weusi wa kitu bila ya kuona weupe wake ni wale wanayoishangaa amri ya Mungu, ya kuwataka wezi kuwakata mikono. Watu hawa hukurupuka na kudai kuwa Uislamu ni dini ya kikatili isiyo na upendo wala huruma. 

Hii ni hoja pofu. Ni kweli kwamba kumkata mwizi mkono sio tendo zuri, lakini kuiba nako sio kuzuri, na ni kwa sababu hii ndio maana wale wanaoitwa "wananchi wenye hasira" huwaua watuhumiwa wa wizi kwa kuwabonda na kuwachoma moto. 

Sheria ya kukata mkono haitekelezwi mpaka tuhuma iwe ya kweli, na kuna kiwango cha wizi kinachoruhusu sheria hii itekelezwe, sio kama hii ya kuwaoka vibaka wa mikufu mitaani na kuwahifadhi wa ‘benki’ na mamilioni ya fedha za umma kwa kesi zisizokuwa na mwisho mpaka zinasahaulika na watuhumiwa kuonekana wakiendelea ‘kupeta’ na ‘kutanua’. 

Nenda kaone mambo yalivyo kule ambako sheria ya kukata mkono imesimama. Kitakachokushangaza ni kwamba hutakutana na mtu mwenye kigutu hata mmoja, kwa sababu hakuna mwenye hata fikra ya kunyoosha mkono wake kuchukua cha mwenzie au cha umma. 

Uislamu unaihurumia jamii nzima, na sio mwizi mmoja mmoja. Izingatiwe pia kwamba hoja dhidi ya Uislamu si hoja dhidi ya Waislamu, bali ni hoja dhidi ya mwenye ulimwengu wake na viumbe wake, yaani Mwenyezi Mungu, ambaye anasema: 

"Je, anayejua ya kwamba yaliyoteremshwa kwako kutoka kwa Mola wako ni haki (akayafuata) ni kama aliyekuwa kipofu ? Wenye akili ndio wanaozingatia". (Qur’an 13:19) 

Juu 
 

YALIYOMO 
 
 
TAHARIRI  
Tuacheni na njaa yetu msituongezee silaha 

Serikali yakumbushwa kujiunga OIC 
Na Mwandishi wetu 

Polisi walizingira nyumba yangu usiku wa manane - Sheikh Mbukuzi 

Wafungwa waomba Futari na Vikoi 

Macho ya shutuma 
Na Abu Halima Sa Changwa 

Hoja pofu 
Na Abu Halima Sa Changwa 

Tafuteni ufalme wa kisiasa 

Ubaguzi katika mfumo wa elimu nchini: Chuo Kikuu chasikia kilio cha wanawake 

'Vichupi' vya nini Kimiti? 
Na. Said Rajab 

Mjadala wa Katiba na haki za Waislamu 
Na Masoud Mohammed Mbogo 

Mdahalo kati ya Waislamu na Wakristo- 3 
Na Nandenga wa Mkomidachi 

Waliochukuliwa utumwa Uarabuni 
Na Hassan Omar 

Madrasatul Maamury Islamiya 

Teknologia: Jifunze Kuunganisha Kompyuta (4) 
Na Hassan Omar 

Kuweni wabunifu muinue taaluma - Wito 

TVZ na kipindi cha 'Wasemavyo' 

Kesi ya Waislamu Mwembechai: Mashahidi washindwa  

Wanyimwa fursa ya kuswali Ijumaa Mwanza 

Shule ya Bakwata yafungiwa Tanga 

Mafunzo ya Qur'an  
Shetani anawaogopesha wenye mali kutoa 

Barua za wasomaji  

Masomo ya dini ya Kiislam  

Chakula na lishe 

Mashairi 

Matangazo 
 

   Kutoa maoni yako kuhusu ukarasa huu: Bonyeza hapa
Au
Andika barua  kwa: webmaster@islamtanzania.org
Home Links Islam Tanzania Matoleo yaliyopita