|
|
|
KUNA suala linalonishinda kuelewa. Shangazi yangu Fatuma haendi kuuza chakula. Nilipomwuliza, kwa nini, akaniambia ameacha kwa sababu chakula chake humwagwa. Nilipomwuliza, na nani? Akaniambia "na SERIKALI". Siku nyingine, nikamuliza mama, mbona siku hizi hatuendi Ubungo kwa Anko. Akaniambia, nyumba ya Anko imevunjwa. Nikamuuliza, na nani? Akaniambia, "na SERIKALI". Halafu. Nikaamuliza baba, lini tutaenda Nzasa kwa babu ? Akaniambia, nyumba ya babu yako imechomwa moto. Nikamuuliza na nani ? Akaniambia, "na SERIKALI". Nikamuuliza mama, mbona siku hizi tunakula mara moja tu, na baba haleti vile vyakula vizuri vizuri, na baba amekuwa mkali kama nini. Mama akaniambia, baba yako kapunguzwa kazi na hajalipwa pesa zake. Nikamuuliza na nani? Akasema "na SERIKALI". Nikamuuliza kaka Sudi kwa nini hakuninunulia nguo za sikukuu kama alivyoahidi. Akaniambia walimu hawajapewa hela zao miezi mitatu. Nikamuuliza wanatakiwa wapewe na nani ? Akaniambia, "na SERIKALI". Nikamuuliza kaka Hashimu, mbona siku hizi hatuendi kuswali Mwembechai ? Akaniambia, Waislamu wanaogopa kuvamiwa na kupigwa mabomu, na sisi hatuwezi kwenda. Nikamuuliza mvamizi huyo ni nani ? Akaniambia, "ni SERIKALI". Nikashangaa hata kaka Athumani naye hapeleki tena karanga zake na pipi Mwenge. Naye pia aliniambia kibanda chake kimevunjwa na huyo huyo SERIKALI. Kha! Ninachoshangaa ni kwamba, huyu SERIKALI, hata kama ni jitu kubwa, hakuna mtu anayeweza kupambana nalo ? Rais wetu hawaambii polisi wamsake huyo SERIKALI? |
YALIYOMO
TAHARIRI Tuacheni na njaa yetu msituongezee silaha Serikali
yakumbushwa kujiunga OIC
Polisi walizingira nyumba yangu usiku wa manane - Sheikh Mbukuzi Wafungwa waomba Futari na Vikoi Macho
ya shutuma
Hoja
pofu
Ubaguzi katika mfumo wa elimu nchini: Chuo Kikuu chasikia kilio cha wanawake 'Vichupi'
vya nini Kimiti?
Mjadala
wa Katiba na haki za Waislamu
Mdahalo
kati ya Waislamu na Wakristo- 3
Waliochukuliwa
utumwa Uarabuni
Teknologia:
Jifunze Kuunganisha Kompyuta (4)
Kuweni wabunifu muinue taaluma - Wito TVZ na kipindi cha 'Wasemavyo' Kesi ya Waislamu Mwembechai: Mashahidi washindwa Wanyimwa fursa ya kuswali Ijumaa Mwanza Shule ya Bakwata yafungiwa Tanga Mafunzo
ya Qur'an
|