AN-NUUR 
Na.170 Jamadul Akhir 1419, Oktoba 9 - 15, 1998 
 
Home Links Islam Tanzania Matoleo yaliyopita
 
 
Kuchomwa nyumba za wananchi; serikali yasema: 

Wanauza viwanja ndani ya Msitu 
 

  • Yadaiwa wameng’oa Beacon
  • Wanachoma mkaa na kupasua mbao
Na Mwandishi Wetu

TAARIFA ya serikali ambayo ilitolewa hata kabla ya wananchi wa Nzasa kuchomewa nyumba zao imeeleza kwamba wananchi hao wamevamia na kuingia ndani kabisa ya eneo la hifadhi ya msitu. 

Wananchi hao imedai taarifa hiyo kwamba mbali ya kujenga nyumba, wanachoma mkaa, kupasua mbao, kung’oa maboya (Beacon) za mpaka wa eneo hilo la hifadhi na hata kuuza viwanja na mashamba. 

Taarifa hiyo ya serikali ilitolewa na Mkuu wa Wilaya ya Kisarawe Capt. J. C. Yamungu baada ya wananchi wa Nzasa kupeleka malalamiko yao kwa Kamati ya Msaada wa Sheria ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam. 

Awali, baada ya wananchi hao kuamriwa kuhama, waliomba msaada kupitia vyombo vya sheria. 

Kamati ya Msaada wa Sheria ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam ililifikisha suala hili katika Wizara husika (Wizara ya Maliasili na Utalii). 

Wizara hiyo iliiarifu Kamati hiyo kwamba wananchi hao wasingeondolewa kwani vijiji vyao viko nje ya mipaka ya hifadhi ya msitu. 

Hata hivyo, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mh. Yusuf Makamba aliripotiwa na vyombo vya habari Julai 25, 1998 akitoa tishio kwamba wananchi hao watahamishwa bila kujali habari za mahakama. 

Agosti 1, 1998 Mkuu wa Wilaya Capt. Yamungu alitoa ilani ya kuwataka wananchi hao waondoke. 

Kufuatia ilani hiyo, wananchi wa Nzasa walikwenda kutaka msaada katika vyombo vya sheria. 

Uchunguzi wa gazeti hili umegundua kwamba Jumanne Oktoba 6, 1998, wajumbe wa Kamati ya Msaada wa sheria walikwenda kuonana na Mkuu wa Wilaya Capt. Yamungu ambapo aliwaonyesha ramani inayoonyesha eneo lililovamiwa na wananchi. 

Hata hivyo, wajumbe hao hawakuweza kuandamana na Mkuu huyo wa Wilaya kwenda kushuhudia eneo linalodaiwa kwamba wananchi wamevamia mpaka ndani kabisa ya Msitu. 

Kilichofuatia baada ya hapo ni zoezi la uchomaji moto nyumba za wananchi hao. Zoezi ambalo limeteketeza nyumba na akiba ya chakula. 

 

 
Juu 
 

YALIYOMO 
 
 

TAHARIRI 
Tutaendelea kudhalilishwa mpaka lini ? 

Waislamu wasisitiza: Nyumba ya Waziri Mkuu ni ya Waislamu 
Na Mwandishi Wetu 

Kuchomwa nyumba za wananchi 
Na Mwandishi wetu 

Maoni Yetu: 
Maisha ya Mtanzania yanapokosa thamani 

Nguruwe marufuku Kinondoni – Tume 
Na Kassim Juma 

Watanzania waanzisha Baraza la Waislamu Marekani 
Na Mwandishi Wetu 

Wanawake Hai wamtaka Rais azungumzie mauaji ya Mwembechai 
Na Mwandishi Wetu 

‘Serikali haiwezi kuzuia rushwa’ 
Na Kassim Msuya 

Makala ya Kimataifa 
Nani gaidi: Slobodan Milosovic au Usama bin Laden 
Na Mwandishi Wetu 

Afghanistan washindi dhidi ya uvamizi karne zote 
Na Faiza bint Abubaka 

MAKALA: 
Demokrasia ya rushwa ! 
Na Mwapwani Mohamed 

Tujikwamue na janga la utwaghuti 
Na I. Kikong’ona 

MAONI: 
Nini Jihad na nani Mujahidina ? 

MAKALA: 
Marekani ni magaidi wa haki za binadamu 
Na MUSSA ALLY 

Tufuate Uislamu kwa vitendo na siyo kwa maneno -2 
Mwandishi: Maalim Ali Bassaleh 

Tusihalalishe mauaji ya raia kwa kisingizio cha ‘wananchi wenye hasira’ 
Na Mwandishi Wetu 

Historia ya sayansi na tiba 
Na Dk. Amur A.A. 

Msiwageuze watoto ombaomba 
Na H.E. Omar 

MAKALA YA JAMII: 
Profesa Malise Kaisi acha uzushi dhidi ya Mtume Muhammad 

Sensa ya majaribio: Wananchi watofautiana na serikali 
Na Rajab Rajab - Morogoro 

Uislamu ulivyoingia Zanzibar -3 

Mwembechai wageuka Hame, Bado walindwa na polisi 
Na Badru Kimwaga 

Waislamu Moro waendelea kusaidia wagonjwa 
Na Rajab Rajab - Morogoro 

Mjadala wa Katiba ya Shirikisho kuzinduliwa Dar Jumapili 
Na Mohamed Othman 

Walimu wa dini Tanga wapokea Baiskeli 
Na Abu Said 

Mafundisho ya Quran 
Kutoa katika njia ya Allah: Al-Baqarah aya  264 

Barua za wasomaji 

Masomo ya dini ya Kiislam 

Chakula na Lishe 
Vitu vinavyoweza kuwemo katika vyakula 

  

   Kutoa maoni yako kuhusu ukarasa huu: Bonyeza hapa
Au
Andika barua  kwa: webmaster@islamtanzania.org
 
Home Links Islam Tanzania Matoleo yaliyopita