|
|
|
QUR’AN Tukufu inatuambia kwamba: "Atakayeua mtu bila ya yeye kuua mtu, au kufanya fisadi katika nchi, basi ni kama amewaua watu wote " (5:32). Maantiki ya kauli hii ya Qur’an ni kwamba akiuliwa japo mtu mmoja, mtu huyo ni sawa na binadamu mwingine yeyote; sio paka. Binadamu ambaye uhai na utu wake unapaswa kulindwa na kuheshimiwa sawa na binadamu mwingine yeyote. Binadamu ana hadhi yake na haki zake zinazoandamana na hadhi hiyo. Mwisho hata kama mtu anahukumiwa kifo kwa hukumu ya mahakama, haiwi kifo hicho iwe ni kuanza kumkata sikio, pua, kumtoboa jicho n.k., hadi afe. Zipo njia za kiungwana zinazokubalika duniani kote kutekeleza adhabu hiyo. Serikali imewachomea nyumba wananchi wa Nzasa kwa madai kwamba wamevamia na kuweka makazi ndani ya eneo la hifadhi ya msitu. Yawezekana wengi wa wananchi hao bado wapo nje wakiwa hawana makazi wala chakula. Lakini tatizo hivi sasa si lao, ni sisi. Ni kweli wao wataendelea kuteseka, lakini tatizo ni je, sisi tunafanya nini. Kudhalilishwa kwa mwananchi mmoja ni sawa na kudhalilishwa mwananchi mwingine yeyote. Hakudhalilishwa yule kwa vile yeye ni nusu mtu. Ni binadamu kama mimi au wewe. Tofauti kama ipo ni kwamba yeye kadhalilishwa leo, kesho yaweza kuwa zamu yako. Ikiwa ilikuwa kwa yule mama Kanda ya Ziwa aliyevuliwa nguo akawekwa pilipili puani na sehemu zake za siri. Juzi ikawa zamu ya akina mama wa Mwembechai kudhalilishwa. Waliuliwa wananchi huko Kilombero. Wale walikuwa wananchi sawa na wananchi wengine. Inawezekana kwamba wengine wakidhani ni wale si sisi. Juzi ikawa Mwembechai. Ubungo walivurumishwa bila fidia wala kupewa viwanja vingine, ikadhaniwa ni wale si sisi. Leo ni zamu ya Wana-Nzasa, hatujui kesho ni wapi. Matukio haya na jinsi yanavyopokewa na wananchi hapana shaka ni ishara mbaya ya huko tuendako. Iwapo tutaona ni sawa tu, kila mmoja anapita na zake huku mwenzao pembeni akikabwa na kibaka kuporwa saa yake; basi tujue hakitapita kitambo, vibaka hata wakiwa wachache kiasi gani utadhani wao wamekuwa wengi kuliko raia wazuri. Sote hatutakuwa na salama, tutatamani tuhame mji na tukose
pa kukimbilia.
|
YALIYOMO
TAHARIRI Tutaendelea kudhalilishwa mpaka lini ? Waislamu wasisitiza: Nyumba ya Waziri
Mkuu ni ya Waislamu
Kuchomwa nyumba za wananchi
Maoni Yetu:
Nguruwe marufuku Kinondoni – Tume
Watanzania waanzisha Baraza la Waislamu
Marekani
Wanawake Hai wamtaka Rais azungumzie
mauaji ya Mwembechai
‘Serikali haiwezi kuzuia rushwa’
Makala ya Kimataifa
Afghanistan washindi dhidi
ya uvamizi karne zote
MAKALA:
Tujikwamue na janga la utwaghuti
MAONI:
MAKALA:
Tufuate Uislamu kwa vitendo
na siyo kwa maneno -2
Tusihalalishe mauaji ya
raia kwa kisingizio cha ‘wananchi wenye hasira’
Historia ya sayansi na tiba
Msiwageuze watoto ombaomba
MAKALA YA JAMII:
Sensa ya majaribio: Wananchi watofautiana
na serikali
Uislamu ulivyoingia Zanzibar -3 Mwembechai wageuka Hame,
Bado walindwa na polisi
Waislamu Moro waendelea kusaidia
wagonjwa
Mjadala wa Katiba ya Shirikisho
kuzinduliwa Dar Jumapili
Walimu wa dini Tanga wapokea
Baiskeli
Mafundisho ya Quran
Chakula na Lishe
|