NASAHA
Na. 057 Jumatano  Julai 19 - 25, 2000
Ukurasa wa mwanzo
Islam Tanzania
Matoleo yaliyopita
LISHE

Yanayoweza kumdhuru mtoto tumboni

CHAMOS, H.J 

MIMBA ni kawaida na ni kitu cha asili. Kila mwaka mamilioni ya wanawake hubeba mimba. Ubora wa mimba utategemea na ufahamu wa mwanamke katika kuyaweka mazingira bora kwa kiumbe kinachokuwa (fetus).

Kufahamu matatizo yanayoweza kumdhuru mtoto tumboni kuna wawezesha wajawazito kuwa waangalifu zaidi kuliko kutofahamu lolote. Hii hasa husababishwa na ule udhaifu alionao mtoto kwani hutegemea mama yake kwa karibu asilimia 98. Hivyo basi kitoto kinachokuwa tumboni chaweza kusumbuliwa au kumdhuru kiakili au kimwili kilingana na kiwango alichoumia mwanamke huyo. 

Chakula bora na mazoezi ni muhimu kwa wote yaani mama mtarajiwa na mtoto atakaezaliwa. 

Miongoni vya vitu vinavyoweza kumdhuru mtoto tumboni ni magonjwa, caffaine, madawa ya kulevya, pombe,sigara, mionzi hasa isiyoyalazima. 

Asilimia kuwa ya madawa anayokunywa mjamzito hupitia kwenye "Placenta' na kuingia kwenye mishipa ya damu ya mtoto. Ujauzito una vipindi mbalimbali kufuatana na ukuaji wa mtoto. Si madawa yote hayafai kwa wajawazito na si madawa yote yanafaa wakati wote wa ujauzito. Madawa mengine hayafai miezi ya mwanzo na mengine hayafai miezi ya mwisho ya ujauzito. Iwapo yatanywewa bila kuzingatia hilo, mtoto aliyetumboni anaweza kudhuriwa bila kufahamu. Mjamzito asinywe dawa bila ushauriwa na daktari. Hata kama unaumwa na kunadawa za mtu mwingine, kwanza shauriana na daktari au mtaalamu wa dawa. Madawa ya kulevya ndio hatari zaidi. Wajawazito washauriwe kuacha kabisa utumiaji wa madawa haya haramu. 

Caffeine hupatikana katika kahawa, chai, coka cola na chokoleti. Madini haya japo huweza kuwadhuru hata watu wakubwa huweza pia kusababisha madhara kwa mtoto aliye tumboni. Wajawazito washauriwe kupunguza unywaji wa kahawa, chai, chokoleti au vinywaji na vyakaula vyenye "cola". Iwapo mazoea yameshindikana kuachwa basi kahawa au majani ya chai yaliyotolewa caffein yatumiwe (decafeinated coffee). 

"Tetekuwanga" ni ugonjwa unaowapata hasa watoto wadogo. Lakini yawezakutokea kumpata mtu mzima. Ugonjwa huu huweza kumdhuru mama na mtoto aliyetumboni. Mjamzito atakapoumwa tekekuwanga, anaweza kuzaa mtoto mwenye mtindio wa ubongo, kipofu, mwenye matatizo ya ngozi na aliyedhoofu. Iwapo hujapata sindano ya kinga, ni vizuri kumwona daktari mapema kabla ya tatizo lolote kukuanza. 

Sigara na uvutaji wake huwathiri watumiaji wake popote walipo. Mjamzito pamoja na kujidhuru yeye mwenyewe, humdhuru pia mtoto aliye tumboni. Wajawazito walio wavutaji huweza kuzaa mtoto mwenye uzito wa chini "kabichi" au"njiti', mtoto pia anaweza kupata matatizo ya mapafu "pneumonia" na kudhoofu afya kwa ujumla. 

Vile vile hata kma mjamzito havuti sigara, wanafamilia wengine wanaweza kumdhuru iwapo watakuwa wanavuta. Wanawake na watoto wengi hudhururiwa na moshi wa sigara ndani ya majumba yao. Hasa pale baba anapomaliza nusu paketi akiwa ndani ya nyumba yao! Kina baba msiyachafue mazingira ya nyumbani iwapo hamuwezi kabisa kuacha uvutaji. 

Pombe ni sumu ya viungo vinavyokuwa. Inaponywewa na mjamzito huingia katika mishipa ya damu ya mtoto kupitia "placenta". Pombe hudhuru viungo dhaifu vya mtoto vinavyokuwa. 

Watoto wanaozaliwa na wanawake walevi huwa na tatizo la ukuaji dhaifu wa ubongo hivyo kuwafanya wasiwe na akili "nzuri". Uzito mdogo wakati wa kuzaliwa, matatizo ya moyo,figo na macho, matatizo ya mifupa pia huweza kuwapata watoto hawa. 

Hata kiasi kidogo cha pombe kinatosha kabisa kuwa na madhara kwa mtoto aliye tumboni. Ni vizuri kuacha kabisa vinywaji hivi iwapo unampenda atakayekuwa mwanao siku zijazo. Kwa wajawazito achana na marafiki walevi na kuwa mkali kwa mume au jamaa atakayekuletea zawadi ya pombe. Usitembelee kabisa sehemu zinazouzwa pombe, wala usikodolee macho matangazo ya pombe. 
 

Juu
 

YALIYOMO
 

Tahariri
Tume, PCB na vyama vya siasa mmekiona mliochoandaliwa Oktoba?

Cheyo kuendeleza  ‘mfumo Kristo’

Rushwa katika kura za maoni: 'CCM isitafute mchawi'

CUF yakanusha propaganda za waraka

Wanachama wa  CUF kortini  Kilwa

Waumini waapa kulinda Msikiti

KINYANG’ANYIRO CHA UBUNGE: CCM Temeke wamtaka Bazaar

'Wanafunzi Lindi wamshughulikia Mkuu wa Shule aliyewazuia kuswali'

Milioni moja zachangwa kujenga madrasa

Hata na mimi sijala

USHAURI NASAHA
Jinamizi la ukewenza

MAKALA
Kushindwa kujitegemea ni laana

MAKALA
UDP, TLP wathibitisha hisia za Waislamu kuwa Uislamu ni kero Tanzania

MIPASHO NASAHA
Mwanasiasa wa kisasa

Kalamu ya Mwandishi
Mamluki wa mageuzi

MAKALA
Mrema na Cheyo wajihadhari wasije wakatumiwa kuwavuruga wananchi

MAKALA
Viongozi wa vyama vya siasa na udini nchini Tanzania

Mandela ni mfano wa kuigwa

Burudani/Muziki
Cat Stevens: Historia kwa Ufupi

Habari za Kimataifa

LISHE
Yanayoweza kumdhuru mtoto tumboni

MASHAIRI

MICHEZO

  • Jenerali Ulimwengu amgonga nyundo Mkapa
  • Hassan Affif aitabiria Simba Ubingwa

  •  


       Kutoa maoni yako kuhusu ukarasa huu:Bonyeza hapa
    Au
    Andika barua  kwa: nasaha1420@yahoo.com

    Ukurasa wa mwanzo
    Islam Tanzania
    Matoleo yaliyopita