|
|
| Home |
TAHARIRUkawamu gani huu!Mwenyezi Mungu anatuambia katika Qur'an kwamba wanaume ni Walinzi (Qawamuna) au wasimamizi wa wanawake. Marais na Wafalme katika nchi huteuwa watu katika nyadhifa mbalimbali ili kutekeleza kazi na majukumu ya kiserikali. Wanaume hawa Waislamu hawateuliwi na Rais wa Taifa kubwa wala Mfalme mwenye utajiri na nguvu kubwa za kijeshi. Wanateuliwa na Mungu Muumba wa Wafalme na Marais kwamba wawe walinzi wa wanawake. Lakini mabinti, wake na akina mama wanalalamika na kumshitakia Mwenyezi Mungu kwamba Qawamuna" hawa wamebakia kuvaa kanzu safi na kujitia manukato tasbihi mkononi huku akina mama hao wakivuliwa nguo na kudhalilishwa! Wengine hodari wa kutoa mawaidha, kudarasisha na mahiri wa kunukuu aya na hadith. Lakini akina mama wanalalamika kwamba umahiri wao huo hauna tija yoyote kwao. Wanahoji "Qawamuna"gani asiyestuka mkewe akivuliwa nguo! Qawamu gani asiyestuka binti yake akidhalilishwa! Tunawashukuru akina mama kwa ujasiri wao kwamba pamoja na mateso waliyopewa na kutishwa hawakuhofu wala kunyamaza. Hii inatupa faraja kwamba tunapata Waalimu wazuri katika jamii yetu ya Waislamu. Hata hivyo tungependa kuwakumbusha akina mama wasisahau kwamba bado wako Waislamu wengine ndani, wengine bado majeraha kupona na tunao bado akina Chuki Athumani. Tuwasaidie na kuwafariji ndugu na jamaa za wale ambao bado wako ndani.
Tuwasaidia gharama za matibabu ambao bado wanauguza majeraha. Na tusikose
kuwajulia hali waliopo bado hospitalini.
|
Maoni yetu:
Unafiki si suala la wakati fulani
Historia ya harakati za ukombozi wa Kashmir Sheikh wa Wilaya Same ahimiza Waislamu kushiriki tamasha Sheikh awataka wanawake wajistiri Madrasat Al-Hujuun washerehekea
mwaka mpya
Uislamu ni mfumo wa maisha - Mbukuzi Pole ya Mwinjilisti Kusupa ni kejeli
|
| An-nuur Home | Links | Islam Tanzania | Matoleo yaliyopita |