AN-NUUR 
Na.184 Ramadhan 1419, Januari 15 - 21, 1998 
 
Home Links Islam Tanzania Matoleo yaliyopita
 
Thamani ya mlo wa Uyoga
 
Na Mujahid Mwinyimvua

KWA kipindi kirefu Uyoga (Mushrooms) ulijulikana kama kiumbe sawa na mimea. Hata hivyo, uchunguzi wa kisasa wa sayansi umebaini kuwa uyoga ni tofauti kabisa na mimea (plants). Kwa maneno mengine tunaweza kusema kuwa uyoga una baadhi ya sifa ambazo ni sawa na zile za mimea na pia una baadhi ya sifa ambazo ni sawa na zile za wanyama (animals). Kutokana na utata huo, wanasayansi wa sasa wameuweka uyoga na "ndugu" zake katika kundi lao ambalo ni "Kingdom Myceteae". 

Kwa asili, uyoga huota katika ardhi, miti iliyooza na katika takataka mbalimbali. Kwa mujibu wa teknolojia ya kisasa, uyoga unazalishwa bila ya kutumia udongo. Kinachohitajika ni kitu kama mabaki ya mimea ambayo huitwa "Substrate" na hali ya hewa yenye kuruhusu ukuaji wa uyoga. Si makusudio ya makala hii kuelezea namna ya kilimo cha uyoga kinavyoweza kufanyika. 

Uyoga umeanza kutumika kama chakula (mboga) miaka zaidi ya elfu mbili iliyopita. Lakini kuna baadhi ya aina za uyoga ambazo zina sumu na hivyo zinaweza kumuatihri mlaji. 

Uyoga kama mlo una thamani kubwa katika mwili wa mwanaadamu. Thamani ya kwanza ni kuwa, uyoga unaupa mwili virutubisho (nutrients). Na thamani ya pili, uyoga una upa mwili ‘dawa’ ambayo inasaidia kuponya baadhi ya maradhi (mfano saratani) na pia unatoa dawa (interferon) ambayo inaupa mwili kinga ya magonjwa yanayosababishwa na virusi ( lakini siyo ukimwi). 

Virutubisho vinavyopatikana katika uyoga ni kama vile protini, madini, vitamini, maji na kabohaidreti. 

Uyoga una protini kiasi cha asilimia 8.1 - 43.0 kutegemea na aina ya uyoga na mahali (substrate, hali ya hewa n.k.) ulipoota au ulipozalishwa. 

Vile vile uyoga ni chanzo kizuri sana cha vitamini ya kundi B. Kwa mfano Thiamine (B1), Riboflavin (B2), Nicotinic acid, Pantothenic acid na kiasi kidogo cha vitamini B12. Pia uyoga una vitamini C (Ascobic acid) na vitamini K. Vitamini A, D, na E pia zinapatikana katika uyoga, lakini kwa kiasi kidogo sana. 

Madini mbalimbali pia zinapatikana katika uyoga. Mfano wa madini hizo ni Potassium, Sodium, Phosphorus, Culcium, Magnesium, Iron (chuma) na Copper (shaba). 

Uyoga vile vile una kiasi cha asilimia 3 - 28 ya Kabohaidreti (sukari, glycogen, nyuzi nyuzi, n.k.). Zaidi ya hayo, uyoga una kiasi fulani cha maji. 

Tukizingatia thamani kubwa tunayoweza kuipata kutokana na mlo wa uyoga, nawahimiza wananchi kuongeza uzalishaji wa uyoga na pia ninawaomba waongeze utumiaji wa uyoga kama mlo. 
 

Juu 
 

YALIYOMO 
 
 
Tahariri 
Baada ya futari nzuri: Tuwatupie macho wenye njaa 

Rais Mkapa kuwa mgeni rasmi Baraza la Idd 

Ubungo yakumbwa na ukame 

Waumini, Masheikh Arusha wasutana kwa futari ya Mrema 

Dondoo za saikolojia 
Na. Abu Halima Sa Changwa 

Waislamu turejee kwa Allah 

MSADAT yazidi kutia moyo Tanga 

Mjue Usama bin Ladin 

MAFUNZO KUHUSU FUNGA YA RAMADHANI 

Michezo isiyoruhusiwa katika Uislamu 

Ustadh Farid: Kijana aliyejitolea kuwapa Da'awa watalii 

Hakuna Magharibi wala Mashariki: Uislamu ni ubinaadamu 
Na Abubakari S. Marwillo 

Ijue madrasati Mar-wa ya Dodoma mjini 
Na Abu Zuberi, Dodoma 

Ijue Madrasat Jadidul Fiqhyyat - Tabata Kimanga 
Na B. Mwakangwale 

Madrasat Hidayatul Muumini Mwadui 

Washindi wa mashindano ya Hadithi za Mtume (s.a.w.) wapatikana 

Madrasa Shafii Ujiji Kigoma yaonyesha umahiri wake 

Waanzisha mifuko kusaidia wagonjwa Dodoma 

Waislamu Kondoa waomba msaada kumalizia Msikiti 

Mnyororo wa imani-2 
Na Sheikh Bernard P. Nyangasa 

Kutoka magazeti ya zamani: 
Wanaoshitakiwa kwa uhaini kortini leo 

Jengo la Waislamu Moshi lageuzwa Kanisa la Walokole 
Na Mwandishi Wetu, Moshi 

Masjid Nurania yaswaliwa Ijumaa 
Na Rajab Rajab, Morogoro 

Jabal Hira kutoa mafunzo ya Kompyuta Morogoro 
Rajab Rajab na Mussa Ally, Morogoro 

Sayansi na Teknolojia 
[Internet ni nini?] 

Masomo ya Dini ya Kiislamu 

Barua za Wasomaji 

Mashairi 

Chakula na lishe 
[Thamani ya mlo wa Uyoga] 
 


Bonyeza hapa
kushriki mjadala au kutoa maoni juu ya habari hizi na masuala mengineyo ya Kiislamu kwenye Baraza ya Wasomaji

   Kutoa maoni yako kuhusu ukarasa huu: Bonyeza hapa
Au
Andika barua  kwa: webmaster@islamtanzania.org
 
Home Links Islam Tanzania Matoleo yaliyopita