|
|
| MASHAMBULIZI
YA MAREKANI NCHINI IRAQ
Dhuluma ya Marekani dhidi ya Waislamu Yafuatayo ni " Mazungumzo ya Ijumaa toka Masjidi Al-aqsa-Al.Quds"
ambayo hutolewa na wanachama wa Hizb ut Tahrir. Mazungumzo hayo
kwa e-mail:
Mazungumzo haya pia yanaweza kusikilizwa katika lugha ya Kiarabu kupitia mtandao wa komputa ulimwenguni www.al-aqsa.org. Mazungumzo yafuatayo yalitolewa Ijumaa 25/12/98 na yalichukua muda wa dakika 11. Sifa njema zinamstahiki Allah. Tunaomba uongofu na ushindi toka Kwake (Allah) pekee, "Yule ambaye Allah amemuongoza basi huyo ameongoka barabara; Lakini yule ambaye Allah amemuacha apotee, wewe hutampatia mlinzi mwingine (zaidi ya Allah) wa kumuongoza katika Njia Iliyonyooka". Ninashahidia kuwa hapana mungu apasaye kuabudiwa kwa haki ila Allah na kwamba Muhammad mja wake (Allah) na ni Mtume wake (Allah). Enyi Waislam, Katika Ijumaa ya kwanza ya Ramadhani mwaka huu, tunakukaribisheni mahali pa safari ya usiku (Istar) iliyofanywa na Mtume Muhammadi (s.a.w.). Tunakutoleeni salaam na tunamshukuru Allah kuwa ametuwezesha sisi sote kuushuhudia tena mwezi wa Ramadhani. Tunamuomba Allah atuwafikishe katika funga zetu wakati wa mwezi huu uliojaa baraka, na tunamuomba Allah atughufirie madhambi yetu yaliyopita na atuepushe mbali na moto wa Jahannam. Enyi Waislam, Leo tutazungumza kile ambacho kila mwislam kwa sasa anakizungumzia - matukio ya huko Iraq. Tutazungumzia ni kwanini Marekani imeipiga mabomu Iraq; kwanini Marikani imekoma; kwa nini ichague kufanya mashambulizi mwanzoni mwa Ramadhani; na iwapo Marekani itaipiga tena mabomu Irag au la. Hivi mpaka lini Mrekani itaendelea na ubabe wake, kiburi chake, kujifaharisha na uharibifu wake katika ardhi hii? Je, muda haujafika tu (kwa ulimwengu) kukomesha vitendo vyake [Merekani] ? Je muda haujafika wa kuing’oa Marekani toka katika ardhi yetu na kusimamisha, badala yake, dola ya haki - Dola ya Khalifa wa Kiislam? Enyi Waislam Marekani inataka kuendeleza "uhodhi" yake na utawala wake wa mabomu juu ya mataifa mengine yote. Inataka kuzuia njia na taratibu za nchi zingine ambazo zinajaribu kushirikiana na Iraq na kunufaika kutokana na biashara ya mafuta. Ikaamua kwamba kwa msaada wa makombora ya Tomahawak, makombora ya Cruise na mabomu ya B-52, yenyewe [Merekani] ndiyo itakuwa mla nyama!. Marekani ikaandaa aina zote za silaha na ikachagua mwanzo wa (mfungo ) Ramadhani kuanzisha mashambulizi yake - mudo mfupi sana baada ya Rais wake (Clinton) kurejea mikono mitupu toka Israel. Mji wa Baghdad ulipigwa mabomu, kama ulivyofanywa mji wa Al-Basra. Hao wanaoitwa watetezi wa haki za binaadam waliandika ujumbe katika makombora hayo kama vile " This is the American Present to the Muslims in Iraq on the occassion of Ramadhani" ( Tafsiri hii ni zawadi toka Marekani kwa Waislam wa Iraq kufuatia kuanza kwa mfungo wa Ramadhani). Zawadi hizo za ‘Uncle Sam’ zimepelekea wanawake na watoto kuunguzwa na kuuawa. Wamerekani hao walirusha makombola katika hospitali za mji wa Baghdad. Hivi watoto wachanga katika hospitali hizi walifanya uhalifu gani kiasi wao kustahili kuuawa namana hiyo? Ni namna gani vichanga hawa waliidhuru kiasi wao kustahili kuuawa pamoja na mama zao, wazazi wao na matabibu wao. Kwani hospitali hizi zilipata kutengeneza silaha za sunu? Kwani hospitali hizi ndizo zilizoishutumu Marekani au ndizo zilizomshutumu Bw. Butler (Mwenyekiti wa Tume ya Umoja wa Mataifa ya Ukaguzi wa Silaha za Iraq) kuwa ni ‘agent’ wa C.I.A. (Shirika la Kijasusi la Marekani)?. Kwa nini katika mwanzo wa Ramadhani ghala zza ngano zipigwe mabomu? Kwa nini ngano na mchele vilichomwe moto huko Iraq ? Nchi ya Iraq ambayo imetengwa! Iraq yenye NJAA! Je? Jii ndiyo haki kwa Merekani na Uingereza? Enyi Waislamu, Kwa nini kiwanda cha kusafisha mafuta huko Al-Basra kililipuliwa? Kwani hapo kuwandani kulikuwa na silaha za nyukilia au silaha za sumu au vifaa vya kutengenezea silaha? Ni katika namna gani kwamba Kiwanda hiki cha mafuta kiliiathiri Marekani? Enyi watu, Utawala wa Marekani ulitangaza kuwa lengo lake lilikuwa ni kuung’oa utawala wa Suddam Hussein. Lakini badala yake, makombora na mabomu yalitupwa juu a vichwa vya (raia) wenye njaa na wenye kuhitaji msaada. Marekani imeshindwa kukamilisha lengo lake la kuipiga mabomu Iraq. Haikuweza kuwakusanya washirika wake kama ilivyokuwa imepangwa. Marekani ilirusha angani makoratasi yenye kuwachochea wananchi wa Iraq kufanya uasi dhidi ya utawala wa Iraq kama hatua ya awali ya kuiangusha serikali ya Iraq. Lakini wananchi hawakuitika wito huo, badala yake, makundi kwa makundi ya Waislaam uliwengu mzima yaliungana kuipinga Marekani. Waliandamana kwa uchungu mkubwa wakipinga matashi ya Serikali za kidhalimu. Kisha hiyo Marekani ikadai eti inaheshimu utukufu wa mwezi wa Ramadhani. (Baada ya kutuma zawadi zake kwa Waislam wa Iraq). Hivyo[Merekani] ikasitisha upigaji mabomu ipate kutathimini upya hayo matukio. Hii ni moja ya sura katika sura kadhaa zinazokuja (tutakazowaletea) kati ya Marekani na Iraq. MWISHO
|
YALIYOMO
Tahariri Onyesheni ushujaa wa Badri Daniel kuwatimua waumini Msikitini Waislamu Moshi: Wadai kulishwa nguruwe, vibudu Dondoo za Kisakolojia
Maulana Sayyid Jamal-Din Afghan 1214 - 1254 (1838-1897) - 2 MASHAMBULIZI YA MAREKANI NCHINI IRAQ Njia bora zitakazotusaidia kuwalea
watoto
Ijue Madrasatul-Qaadiriya Sokoni
I Arusha.
Tutafute kwanza ufalme wa Allah (s.w.)
Chuo cha Kilimo Ukiriguru kupata
Msikiti mpya
Huduma za maji Kondoa haziridhishi
Mnyororo wa imani
Je, Yesu alibatizwa?
Kufuatia Waislamu kuritadishwa Merela Morogoro: Masheikh wa mjini watupiwa lawama Abiria walaani kumwagiwa pombe Kondoa Sheikh Bafadhil ateuliwa
kudhamini waandishi wa habari Morogoro
Sayansi na Teknolojia
Chakula na lishe
|