|
|
|
Mavuno yangu yasiwe... KABLA ya hali hii niliyonayo sasa nilikuwa mstari wa mbele kuwaita watu kwenye kheri. Wakati huo hali yangu kimaisha haikuwa nzuri kama ilivyo sasa. Nilishirikiana na ndugu zangu kwa wema na ucha Mungu. Wote walinipenda na kunifurahia kwa moyo wangu. Mwenendo wangu ulianza kubadilika kidogo kidogo baada ya shilingi na nduguze kupiga hodi mara kwa mara nyumbani. Hatimaye wakazoea nyumbani kwangu wakanishawishi niwanyanyapae wale niliotoka nao mbali. Ukapa na mimi tukawa maadui wasio karibiana. Njaa na mimi tulifikishana njia panda, kila mmoja akenda njia yake. Taratibu, rafiki yangu mpenzi Ucha Mungu akaanza kunikimbia, hodi hodi zikawa kero kwangu, nilipogongewa mara nyingine niliweza kukaa kimya ndani mpaka huyo aliyegonga alipoondoka. Maskini nafsi yangu! Nilijiona Malkia katika himaya ya kusadikika ndani ya kasri la kupendeza. Nilikuwa Malkia niliyejali kitu kuliko utu. Mawaidha kadhaa yalinipitikia lakini hayakuweza kuupinda moyo wangu. Niliyakusanya mema niliyoyatenda nikayarusha jaani! Watu wote, wakubwa kwa wadogo niliwaweka kiganjani, hakuna aliyethubutu kunikabili, kuninasihi na kunishawishi. Walijikunja kama jongoo mbele yangu! Jamani wapi naelekea, njooni, msinikimbie, haya ndiyo maumbile yangu. Nahitaji ushauri wenu, nahitaji nasaha zenu. Mavuno yangu yasiwe mtihani kwangu na kwenu. Nishikeni bega, nivumilieni kwa kauli zangu za kuudhi na maneno yangu ya karaha. Nisameheni kwa yote. Mwenyezi Mungu anatukumbusha sote: "Na ajisalimishaye uso wake kwa Mwenyezi Mungu, na hali yakuwa anawafanyia wema (viumbe wenziwe), bila shaka amekwishakamata fundo lililo madhubuti; na mwisho wa mambo yote ni kwa Mwenyezi Mungu". (31:22) |
YALIYOMO
Tahariri Kingunge, kweli upo uonevu na dhulma Wananchi wahoji kuhusu polisi aliyeua Arusha Dondoo za Saikolojia
Kona ya Wacha Mungu
Jicho la Uzalendo: Bhabhoo! Muungwana
huyoo!
Maulana Sayyid Jamal-Din Afghan 1214 - 1254 (1838-1897) Mafunzo kuhusu funga ya Ramadhani
Marekani ni mtetezi au adui wa haki?:
Umoja wa Mataifa upo upande gani?
Dawa ya ukimwi ni mwenendo mwema
Mwalimu Maif: Mwanamke aliyetumia maisha yake kufundisha Qur'an Wazazi waaswa kutoshabikia maovu Je, hivi tuendelee kushika amri za
Mungu tena? (jibu)
Mapinduzi, Muungano kwa manufaa ya nani? Fufueni EAMWS - Sheikh Amana
Msiitupie lawama serikali - Dk. Omar Baada ya kuvunjiwa nyumba,
kuchomewa vyakula na Serikali: Nzasa sasa wafuturu Maembe
Acheni mifumo mibovu, fuateni Qur'an - Sheikh Kilemile Sayansi na Teknolojia
Chakula na lishe
|