AN-NUUR
Na.162 Rabiul Thani 1419, Agosti 14 - 20, 1998
 
Home Links Islam Tanzania Matoleo yaliyopita
 
 Wanafunzi Wakatoliki darasa la saba 1998:
Afisa Elimu akiri kutaka orodha ya wanafunzi

Adai amejieleza Wizarani 

Atekeleza ombi la Katekesi 

Na Mwandishi Wetu, Morogoro 

AFISA Elimu wa Manispaa ya Morogoro Bibi E. Mwangamila amekiri kwamba ofisi yake ilitoa agizo kwa wakuu wa shule za msingi kumpa orodha ya wanafunzi Wakatoliki. 

Afisa Elimu huyo amedai kwamba amefanya hivyo kutekeleza ombi la 

Mkurugenzi wa katekesi Jimbo la Morogoro Sr. M. Bonifacia C.P.S. 

Bibi Mwangamila amesema alipokea ombi hilo alishindwa la kufanya kwani alikuwa mgeni ofisini hapo, hata hivyo alipotaka ushauri kwa wale aliowakuta ofisini, walimhakikishia kwamba halina tatizo na hufanyika kila mwaka. 

Baada ya kupewa maelezo hayo alisema ndipo alitoa maelekezo kwa Bw. E.P. Mpessa kutoa agizo kwa waalimu wakuu kutuma ofisini kwake majina ya wanafunzi wa Kikristo. 

Bibi E. Mwangamila amesema kwamba baada ya wananchi kuonyesha wasiwasi kufuatia zoezi hilo, ameandika barua Wizara ya Elimu kutoa ufafanuzi ambapo amedai kwamba nakala ya barua hiyo ameipeleka kwa Mheshimiwa Rais Benjamin William Mkapa. 

AN-NUUR imebahatika kupata nakala ya barua Na. DM/CAT/MTI-S/M/03/98 inayodaiwa kutoka idara ya Katekesi inayoomba majina ya wanafunzi Wakatoliki. 

Hata hivyo, barua hiyo ikilinganishwa na ile ya Afisa Elimu wa Manispaa inazua maswali mengi kuliko majibu. 

Kwanza barua hiyo ya Sr. M. Bonifacia inaonyesha iliandikwa Machi 2, 1998 na kuomba majina ya wanafunzi Wakatoliki yafike Idara ya Katekesi jimboni Morogoro kabla ya Aprili 30, 1998. Hata hivyo barua hiyo inaonyesha ilipokelewa ofisini kwa Afisa Elimu Manispaa Juni 1, 1998, miezi mitatu baadae, wakati ofisi hizo mbili zinatenganishwa na umbali usiotimia hata robo kilo meta. 

Lakini jingine ni kwamba wakati barua toka Afisa Elimu Manispaa kwenda kwa wakuu wa shule inaonyesha kuandikwa Juni 9, vidokezo juu ya barua toka Idara ya Katekesi inaonyesha kwamba waalimu walipewa maelekezo na kuandikiwa barua Juni 8, 1998. 

 
 

Juu 
 

YALIYOMO
 

TAHARIRI 

Serikali yaipongeza Africa Muslim Agency 
Na Mwandishi Wetu, Moshi 

Wanafunzi Wakatoliki darasa la saba 1998: 
Afisa Elimu akiri kutaka orodha ya wanafunzi 
Na Mwandishi Wetu, Morogoro 

Athari ya milipuko Dar, Nairobi: Waliokufa wafikia 258 
Na Mwandishi Wetu 

Wakuu wa mashule waache ubaguzi 
Na Mwandishi Wetu 

ABU AMEENA: Mwana harakati aliyesilimisha wanajeshi 3000 wa Marekani -2 

Kisiwa cha Karafuu chageuzwa cha ulevi 

Twalaban wadhibiti Afghanistan yote 

Madina yachapisha kitabu cha rejea 

MAPENDEKEZO YA KATIBA YA SHIRIKISHO LA TANZANIA 

Maoni: Nyerere kasema kweli Ujamaa na Ukristo vimeshindwa 
Na Abdul Gullam 

Kina Ngatara na wenzake ndio urithi tulioachiwa na Wakoloni 
Na J. Hussein 

HOJA BINAFSI: Suala la Mwembechai, serikali imeumbuka 
Na Mwinjilisti Kamara Kusupa 

Kupigwa mabomu misikitini: Waislamu tumejifunza nini? 
Na RAJAB RAJAB

MAONI: Hoja za kutofautisha Yesu na Issa ni udhaifu na ni uzushi mtupu!
Na Muhibu Said

Utangazeni Uislamu kwa nguvu zote – Sheikh Jongo
Na Badru Kimwaga

Salafiya wataka wanawake wawe macho na vyombo vya habari
Na Mwandishi Wetu

Waumini Misufini Morogoro waazimia kujenga Msikiti
Na Rajab Rajab, Morogoro

Serikali yatakiwa kuondoa askari Mwembechai
Na Badru Kimwaga

Mafunzo ya Quran 

Barua za wasomaji 

Mashairi 

Masomo 

Chakula na Lishe  

 

 

 

 
 Kutoa maoni yako kuhusu ukarasa huu:
Bonyeza hapa
Au
Andika barua  kwa: webmaster@islamtanzania.org
 
Home Links Islam Tanzania Matoleo yaliyopita