|
![]() |
![]() |
![]() |
![]() |
Adai amejieleza Wizarani Atekeleza ombi la Katekesi Na Mwandishi Wetu, Morogoro AFISA Elimu wa Manispaa ya Morogoro Bibi E. Mwangamila amekiri kwamba ofisi yake ilitoa agizo kwa wakuu wa shule za msingi kumpa orodha ya wanafunzi Wakatoliki. Afisa Elimu huyo amedai kwamba amefanya hivyo kutekeleza ombi la Mkurugenzi wa katekesi Jimbo la Morogoro Sr. M. Bonifacia C.P.S. Bibi Mwangamila amesema alipokea ombi hilo alishindwa la kufanya kwani alikuwa mgeni ofisini hapo, hata hivyo alipotaka ushauri kwa wale aliowakuta ofisini, walimhakikishia kwamba halina tatizo na hufanyika kila mwaka. Baada ya kupewa maelezo hayo alisema ndipo alitoa maelekezo kwa Bw. E.P. Mpessa kutoa agizo kwa waalimu wakuu kutuma ofisini kwake majina ya wanafunzi wa Kikristo. Bibi E. Mwangamila amesema kwamba baada ya wananchi kuonyesha wasiwasi kufuatia zoezi hilo, ameandika barua Wizara ya Elimu kutoa ufafanuzi ambapo amedai kwamba nakala ya barua hiyo ameipeleka kwa Mheshimiwa Rais Benjamin William Mkapa. AN-NUUR imebahatika kupata nakala ya barua Na. DM/CAT/MTI-S/M/03/98 inayodaiwa kutoka idara ya Katekesi inayoomba majina ya wanafunzi Wakatoliki. Hata hivyo, barua hiyo ikilinganishwa na ile ya Afisa Elimu wa Manispaa inazua maswali mengi kuliko majibu. Kwanza barua hiyo ya Sr. M. Bonifacia inaonyesha iliandikwa Machi 2, 1998 na kuomba majina ya wanafunzi Wakatoliki yafike Idara ya Katekesi jimboni Morogoro kabla ya Aprili 30, 1998. Hata hivyo barua hiyo inaonyesha ilipokelewa ofisini kwa Afisa Elimu Manispaa Juni 1, 1998, miezi mitatu baadae, wakati ofisi hizo mbili zinatenganishwa na umbali usiotimia hata robo kilo meta. Lakini jingine ni kwamba wakati barua toka Afisa Elimu Manispaa kwenda kwa wakuu wa shule inaonyesha kuandikwa Juni 9, vidokezo juu ya barua toka Idara ya Katekesi inaonyesha kwamba waalimu walipewa maelekezo na kuandikiwa barua Juni 8, 1998. |
Serikali yaipongeza Africa Muslim
Agency
Wanafunzi Wakatoliki darasa la saba
1998:
Athari ya milipuko Dar, Nairobi: Waliokufa
wafikia 258
Wakuu wa mashule waache ubaguzi
ABU AMEENA: Mwana harakati aliyesilimisha wanajeshi 3000 wa Marekani -2 Kisiwa cha Karafuu chageuzwa cha ulevi Twalaban wadhibiti Afghanistan yote Madina yachapisha kitabu cha rejea MAPENDEKEZO YA KATIBA YA SHIRIKISHO LA TANZANIA Maoni: Nyerere kasema kweli Ujamaa
na Ukristo vimeshindwa
Kina Ngatara na wenzake ndio urithi
tulioachiwa na Wakoloni
HOJA BINAFSI: Suala la Mwembechai,
serikali imeumbuka
Kupigwa mabomu misikitini: Waislamu
tumejifunza nini?
MAONI: Hoja za kutofautisha Yesu
na Issa ni udhaifu na ni uzushi mtupu!
Utangazeni Uislamu kwa nguvu
zote – Sheikh Jongo
Salafiya wataka wanawake
wawe macho na vyombo vya habari
Waumini Misufini Morogoro
waazimia kujenga Msikiti
Serikali yatakiwa kuondoa
askari Mwembechai
|
![]() |
![]() |
![]() |
![]() |