BAKWATA kushitakiwa

Baraza Kuu la Waislamu Tanzania huenda likafikishwa mahakamani kufuatia taarifa yake kwa vyombo vya
habari inayomshutumu Mhe. Kitwana Kondo kwamba kala shilingi milion 28 za Waislamu

Tuhuma hizo nzito zimetolewa na Msemaji Mkuu wa BAKWATA Bw. Yahya Hussein wakati akiongea na
waandishi wa habari, kufuatia hatua ya Mh. Kondo kuikosoa Serikali juu ya mwenendo wake uliodhidi ya
Waislamu

Mheshimiwa Kitwana Kondo amesema kwamba tayari anawasiliana na wakili wake ili aandae taratibu za
kuipeleka BAKWATA mahakamani ikathibitishe juu ya madai yao ya milioni 28.

Akizungumza na waandishi wa habari Mhe. Kondo alisema kwamba ingekuwa Bw. Yahya Hussein ametoa
shutuma hizo kama mtu binafsi, asingejali. Lakini maadhali amesema kama BAKWATA chombo ambacho
anaujua uhusiano wake na Serikali, ni lazima ashitaki.

Akiongea na waandishi wa habari kama Mwenyekiti wa Idara ya Habari ya BAKWATA, Yahya Hussein
alimtuhumu Mhe. Kitwana Kondo kuzihini sh. Milioni 28 fedha za mfuko wa Sheikh Kassim Foundation

Akizikanusha tuhuma hizo Mhe. Kondo alieleza kwamba yeye ni mdhamini tu wa mfuko huo na hajawahi
kushika hata senti moja ya mfuko huo.

Aliwataja viongozi wa mfuko huo kwamba ni Sheikh Ismail Mohamed (Mwenyekiti), Brigedia Hashim Mbita
(Makamu Mwenyekiti);Idd Simba (MP) ambaye ni katibu Mkuu na Sheikh Khalifa Hamisi (Naibu Katibu
Mkuu).